Ununuzi wa Tv Zanzibar

Ununuzi wa Tv Zanzibar

NALO LITAPITA

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2011
Posts
333
Reaction score
90
Heshima kwenu wakuu,Tafadhali naomba kusaidiwa jambo.Ninahitaji kununua TV flat screen yenye bajet ya 1,100,000.

Sasa kuna mdau mmoja aliwahi kuniambia kuwa Zanzibar TV ni bei nafuu zaidi ya Dar.

Mwenyeuzoefu naomba kusaidiwa je ikiwa nikienda kununua Zanzibar hakuna vikwazo vyovyote kuvuka nayo kuja huku bara?

Pia kama kuna mtu anauzoefu na bei za TV upande wa visiwani tafadhali naomba abcd juu ya suala hili.

Natanguliza shukrani wakuu.
 
Hii inanihusu, nahitaji tv toka zanzibar 32" bei usizidi 300,000 kama nabheza bata mniambie
 
Tatizo lipo bandarini Dar tu, kama walimsikiliza Rais aliposema kuna watu wanawazidishia ushuru watu na kama wameacha basi utaivusha salama na utafurahia.
Nimevusha tv mara 2 na mara zote nimeishia kusumbuana nao, mfano nilikuwa na tv inch 43 wakataka eti niwape 180,000 kama ushuru nikagoma na kuiacha hapo baadae wakaniita nikalipa elfu 57 tu, mara ya pili nimevusha inch 32 wakasahau tena wakaniambia nilipe 170,000 nikaiacha baadae nikalipia elfu 37.
Pale bandarini wanakupigia ushuru wa kutoka nje yaaani ile VAT iliyotakiwa kulipwa wakati bidhaa inatoka let say China, ukiwauliza mbona hoi bidhaa ishalipiwa ilipoingia Zanzibar hapo ndio hawatakupa majibu sahihi, watalazimisha ulipie 18% VAT, ukiwagomea na kuwaomba muongozo wa TRA hapo ndio mtalipana kishkaji. Unachotakiwa kulipa ni ile pungufu ya VAT, yaani kama bidhaa ililipiwa VAT 15% ilipofika Zanzibar na huku bara ilitakiwa kulipiwa 18% basi wewe unatakiwa kulipa 3% ilibaki.
Usisahau kuna gaharama za kupita bandarini zanzibar ambayo ni kama elfu 7 na Dar nao wanataka elfu 10, hiyo ni tofauti na ushuru, pia kwenye boti za Kilimanjaro wanataka ulipie kama elfu 30 kwa tv kuazia inch 32.
Njia nyingine ambayo sio salama sana ni kupitia meli za mizigo, hapo unaitoa bure, ila usalama ndio majaaliwa.
 
Tatizo lipo bandarini Dar tu, kama walimsikiliza Rais aliposema kuna watu wanawazidishia ushuru watu na kama wameacha basi utaivusha salama na utafurahia.
Nimevusha tv mara 2 na mara zote nimeishia kusumbuana nao, mfano nilikuwa na tv inch 43 wakataka eti niwape 180,000 kama ushuru nikagoma na kuiacha hapo baadae wakaniita nikalipa elfu 57 tu, mara ya pili nimevusha inch 32 wakasahau tena wakaniambia nilipe 170,000 nikaiacha baadae nikalipia elfu 37.
Pale bandarini wanakupigia ushuru wa kutoka nje yaaani ile VAT iliyotakiwa kulipwa wakati bidhaa inatoka let say China, ukiwauliza mbona hoi bidhaa ishalipiwa ilipoingia Zanzibar hapo ndio hawatakupa majibu sahihi, watalazimisha ulipie 18% VAT, ukiwagomea na kuwaomba muongozo wa TRA hapo ndio mtalipana kishkaji. Unachotakiwa kulipa ni ile pungufu ya VAT, yaani kama bidhaa ililipiwa VAT 15% ilipofika Zanzibar na huku bara ilitakiwa kulipiwa 18% basi wewe unatakiwa kulipa 3% ilibaki.
Usisahau kuna gaharama za kupita bandarini zanzibar ambayo ni kama elfu 7 na Dar nao wanataka elfu 10, hiyo ni tofauti na ushuru, pia kwenye boti za Kilimanjaro wanataka ulipie kama elfu 30 kwa tv kuazia inch 32.
Njia nyingine ambayo sio salama sana ni kupitia meli za mizigo, hapo unaitoa bure, ila usalama ndio majaaliwa.
Asante sana mkuu,Mfano hiyo ya nch 43 ilikuwa ni TV aina gani na kule uliinunua kwa shilingi ngapi?kadhalika hiyo ya nch 32 nikipata ufafanuzi wake itapendeza zaidi mkuu.
 
Asante sana mkuu,Mfano hiyo ya nch 43 ilikuwa ni TV aina gani na kule uliinunua kwa shilingi ngapi?kadhalika hiyo ya nch 32 nikipata ufafanuzi wake itapendeza zaidi mkuu.
Hizi zote zilikuwa star x, 43 nilinunua 610,000 na 32 kwa 320,000
 
Back
Top Bottom