Ununuzi na uuzaji wa hisa

Neytemu

Member
Nov 7, 2010
83
1
Wakuu naomba msaada kwa wenye ufahamu kuhusu ununuzi na uuzaji wa hisa.Nitashukuru kama mtaniwezesha kujua kampuni ambazo hisa zinanunulika na kuuzika kwa urahisi, kwa muda mfupi na kwa faida nzuri.

Ningependa kufahamu pia ni kwa jinsi gani naweza kufaidika kwa ununuzi wa vipande vya UMOJA FUND
 
Ya ununuzi wa hisa ni mzuri iwapo una fedha nyingi za kutosheleza, pia ina faid iwapo utaweza kununua hisa katika bei ndogo lakini kwa miaka ya baadae thamani yake ipande na hii mara nyingi hutokea baada ya miaka kadhaa iwapo kampuni inapokuwa inapata faida na mafanikio. Kama uko Dar ni vizuri zaidi ukienda pale dar stock exchange watakulelezea vizuri zaidi hawana longolongo ukifaika watakuelezea from A to Z mpaka makapuni na bei zao za hisa. Ukisha nunua hisa utapewa cerificate baada ya wiki kadhaa lakini pia utaweza kuuza hisa hisa zako iwapo utatak kufanya hivyo. Pia unaweza tembelea website yao ina information juu ya makapuni na bei zao.
 
Back
Top Bottom