kwisha
JF-Expert Member
- Sep 9, 2021
- 1,788
- 5,027
Kuna mwanamke wa Uganda nilitokea kumpenda sana kazini kwetu, na kwa bahati nzuri nikampa ukweli wangu lakini maskini ya Mungu akanipotezea. Nilijaribu njia nyingi kumfanya anipende lakini alikataa kabisa
Ila akatokea kumpenda Mhispania fulani hivi ambaye tunafanya naye kazi hapo kazini. Nikaona siyo kesi acha ni potezee tu, labda siyo riziki.
Sasa leo tulikuwa kwenye mapumziko, nilikuwa nimeweka 'headphones' masikioni kwangu, lakini nilikuwa sisikii mziki, wao wakafikiri mimi nasikiliza muziki. Nikaskia huyo mwanamke akawa anamwambia huyo mwenzake kuwa mimi nina tabia za kishamba sana.
Aliongea maneno mengi ya kunidharaulisha kwa huyo mpenzi wake. Nilivyokwenda kumwambia ukweli, ananijibu jeuri kuwa sina cha kumfanya!
Ungekuwa wewe ungefanyaje?
Ila akatokea kumpenda Mhispania fulani hivi ambaye tunafanya naye kazi hapo kazini. Nikaona siyo kesi acha ni potezee tu, labda siyo riziki.
Sasa leo tulikuwa kwenye mapumziko, nilikuwa nimeweka 'headphones' masikioni kwangu, lakini nilikuwa sisikii mziki, wao wakafikiri mimi nasikiliza muziki. Nikaskia huyo mwanamke akawa anamwambia huyo mwenzake kuwa mimi nina tabia za kishamba sana.
Aliongea maneno mengi ya kunidharaulisha kwa huyo mpenzi wake. Nilivyokwenda kumwambia ukweli, ananijibu jeuri kuwa sina cha kumfanya!
Ungekuwa wewe ungefanyaje?
