mhhh Ngoja hii nimuulize mke wangu mama gaude akirudi kazini nijue kama angelikuwa yeye angefanyaje
Upofu sana tu yaani
cha kwanza kabisa mimi sijasema kitu chochote kuhusu nyumba ndogo... haiwezi kuwa nyumba ndogo kama bado hamjaoona...... na kuishi na mwanaume kama kwako ni big NO basi kwangu ni big YES. kuna mambo mengi sana ambayo mnaweza jifunza kuhusu wote kabla ya ndoa...sex, financial situation ,love life ....... etc. kwa kweli naamini kila mwanamke ni tofauti..
sasa wewe ulimshaurije? mwambie hakunaga mapenzi mtu anapokutamkia kwa mdomo wake kwamba muachane, hamuwezi kwenda sambamba hata ulazimishe kivipi, ni kupotezeana muda tu na maumivu ya muda mrefu...mwambie ashike njia kwa sasa.
na wadada cc tuna mambo sana, yaani unakusanya vi chupi na vi bra vyako huyoooo mbio kwa mwanaume ukajihifadhi....ndio matokeo yake haya.
kwangu ni BIG NOO rejea mada ya DENA ameongelea nyumba ndogo tutakuwa marafiki mpaka uchumba lakini sitaishi na wewe huo ndo msimamo wangu bahati nzuri nilishaolewa na sikuwahi kuhamia kwa Mr tulikuwa kwenye relationship for three years kwenda na kuondoka sawa lakini funga virago au yeye ahamie kwangu ilikuwa hapana
Asante nyamayao ndo maana nakupenda sema tena kwa sauti kubwa watu wakusikie huku ndani yeye kuhamia kwangu au mie kubeba kisambusa na kuhamishia kwake hapana bado
Navyofahamu jamaa ndio alimlazimisha binti ahamie kwake na nyumba aliyokuwa amepanga akairudisha sasa kashakolezwa anabwagwa wanaume hawa jamani mie hata hamu nao sina kabisa