Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Mahusiano na mapenzi ni vitu viwili vinavyoshabihiana lakini havifanani ingawa vinabebana. Unaweza kumpenda mtu lakini usiwe na mahusiano naye na unaweza kuwa na mahusiano na mtu lakini usimpende. Kama alivyowahi kusema Whoop Goldenberg akimtetea Tiger Woods dhidi ya kashifa yake ya ufuska, kwamba wanandoa wengi huwa wanatoka nje ya ndoa zao lakini mbele ya kadamnasi ni wanafiki wanaowashutumu wenzao kwa kutoka nje ya ndoa zao, nami kwa kiasi fulani naamini huo ndiyo ukweli.
Lakini kwa wale walioko kwenye mahusiano na watu walio kwenye ndoa wanapodai uaminifu toka kwa wapenzi wao hao wanajitendea haki? Unatembea na Boy Friend, Girl Friend, Mke au Mume wa mtu halafu unataka eti awe "muaminifu" inakuwaje wewe unajua kwamba mnafanya udanganyifu na mwenzio halafu wewe unataka awe muaminifu?
sielewi sawasawa!!
Lakini kwa wale walioko kwenye mahusiano na watu walio kwenye ndoa wanapodai uaminifu toka kwa wapenzi wao hao wanajitendea haki? Unatembea na Boy Friend, Girl Friend, Mke au Mume wa mtu halafu unataka eti awe "muaminifu" inakuwaje wewe unajua kwamba mnafanya udanganyifu na mwenzio halafu wewe unataka awe muaminifu?
sielewi sawasawa!!