Wengi wetu tuna mawazo mazuri sana ya kujiendeleza, tatizo kubwa ni mitaji na masoko. Serikali hii haina mipango thabiti ya kurasimisha sekta isiyo rasmi ili mlalahoi (watu wa chini) aweze kukopesheka na mabenki yaliyopo hapa nchini badala yake wenye nafasi kubwa kiuchumi ndio wanaokopeshwa fedha ndogo ndogo za walalahoi zilizowekwa ktk mabenki ikiwemo mifuko ya jamii.