Unapoulizwa swali hili kwenye mahusiano "Unafanya kazi gani?"

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,489
40,506
Ukiwa uko kwenye mchakato wa kuanzisha mahusiano, na ikatokea mmoja wenu anakuuliza unafanya kazi gani? Moja kwa moja jua huyo anataka uhusiano wenye faida hasa wa kipesa na si mahusiano ya shida na raha.

Ni vizuri zaidi unapotafuta mwenzi wa maisha hata kama kiuchumi uko vizuri jaribu kuwa kama choka mbaya ili uweze kumpata mtu sahihi lasivyo utapendewa vitu vyako na hivyo vitu vikiisha kunakuwa hakuna mapenzi tena.
 
Sasa utadeal vipi na mtu usiyejua anachojishughulisha nacho?

Kama hawezi kujitunza anawezaje kuungana nawe mkajitunza wote?
Kwa hiyo mkuu,inamaana mwenzako akiwa hana kipato mahusiano yanaweza yasiwepo?
 
Kwa hiyo mkuu,inamaana mwenzako akiwa hana kipato mahusiano yanaweza yasiwepo?
Nadhani sielewi uzi unataka nini....

Uzi unasema ukiulizwa swali la unajishughulisha na nini jua kuna kuliwa.

Sio kweli kwasababu kuna kazi ambazo siwezi kuwa nazo karibu maishani mwangu na nisingetamani wawe wapenzi wangu.


Swali la pili...inategemea.....kwa Jane inaweza kuwa jibu ni ndiyo ila kwa Rowin jibu likawa hapana.
 
Katika mazingira hayo,tunaweza kusema aina ya kazi huchangia kiwango kikubwa kwenye mahusiano. Mtu anapendwa kutokana na kazi yake
 
Kwa mfano nikimwambia hiyo manzi,kuwa Mimi msukuma mikokoteni atakua hanipendi kwa kuwa msukuma mikokoteni?
Inanikumbusha bongo move moja alicheza cheki budi inaitwa mapito.inahusu mada hapo juu.
ha ha ha ha ukimuambia hivyo lazima upigwe chini, tofauti na hapo labda awe amekupenda toka moyoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…