Unapotafuta marafiki/mchumba/mwenza mtandaoni, kumbuka haya!

Thad

JF-Expert Member
Mar 14, 2017
13,363
31,504
Wasalaam wanajf!
Kumekuwa na wimbi kubwa la watu kutafuta marafiki,wachumba na wenza mitandaoni kila kukicha. Hivyo ni vyema tukakumbushana mambo mbalimbali yanayojitokeza kabla,wakati na baada ya kutafuta mtandaoni.

SABABU:

Watu wengi wamekuwa wakiwashangaa watu wanaotafuta marafiki,wachumba au wenza mitandaoni. Jamii imejenga mtazamo hasi kwa watafutaji hawa wakisahau kuwa kuna sababu mbalimbali zinazopelekea watu kutumia mitandao kwa utafutaji huo. Zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazopelekea:-

a) Kubanwa sana na kazi (u busy)
Kuna watu ambao muda wao mwingi wanautumia kufanya kazi kiasi kwamba hawapati nafasi ya kujichanganya na watu wanaowazunguka kama marafiki na majirani. Hivyo ni rahisi kwao kutumia muda mfupi kama saa moja kuwasiliana na kubadilishana mawazo na watu mbalimbali mitandaoni. Lakini pia ni rahisi kuwasiliana na kufanya kazi kwa wakati mmoja.

b)Mazingira ya ugenini.
Wakati mwingine mazingira ya ugenini huwafanya watu wajione wapweke na hivyo huamua kutumia mitandao kupata marafiki kirahisi sana. Mfano,mmoja kati ya marafiki zangu alikiri kuwa aliamua kutumia mtandao wa badoo alipokuwa nchini China kwasababu ya upweke aliokuwa nao.

c)Hulka ya kutojichanganya.
Kuna watu hawapendi mitoko wala sio watu wa kujichanganya na jamii. Hivyo watu hawa hukosa marafiki/wachumba au wenza kutoka katika jamii inayowazunguka badala yake ni rahisi kwake kupata marafiki wa kubadilishana nao mawazo akiwa ndani kwake.

d)Udomo zege
Kuna watu hutafuta wachumba na wenza mitandaoni kwa kuwa hawana ujasiri wa kumfuata mtu na kumtongoza/kumwambia kuwa anampenda ana kwa ana. Hivyo kupitia mtandao ni mambo yanakuwa rahisi zaidi. Hii pia imerahisisha sana kwa wanawake kupata wachumba/wenza pale anapokuwa anahitaji.

FAIDA

Kuna faida nyingi sana za kutafuta marafiki/wachumba/wenza mitandaoni. Hizi ni baadhi tu ya faida hizo:-

i)Kupata watu wangi kwa wakati mmoja.
Mtandaoni ni sehemu pekee unayoweza kupata marafiki au wachumba wengi kwa wakati mmoja. Hivyo ni rahisi sana kuchekecha na kupata marafiki au mchumba um/watakao.

ii)Kupata marafiki/wachumba /mwenza kutoka sehemu yoyote ile duniani.
Mitandao inatoa wigo mpana wa kupata marafiki kutoka sehemu mbalimbali na wenye hadhi mbalimbali kuliko hao wanaokuzunguka. Nakiri kuwa kupitia mitandao nimepata marafiki ambao katika mazingira yanayonizunguka kamwe nisingewaza kukutana nao. Mara nyingi rafiki zangu ninaoishi nao, huniuliza nimefahamiana vipi na hao marafiki kwani mazingira yao na yangu na hadhi zao hazituruhusu kukutana kirahisi.

iii)Kupata mawazo mapya.
Wakati mwingine marafiki wanaotuzunguka, wanakuwa na mawazo sawa na yetu. Hivyo marafiki kutoka mitandaoni huwa na mawazo mapya na pengine yenye kutoa changamoto. Kwa sisi wajasiriamali tunajua umuhimu wa kuwa na wazo jipya kila iitwapo leo.

CHANGAMOTO

Penye faida hapakosi changamoto.Baadhi ya changamoto zinazojitokeza katika utafutaji wa marafiki/wachumba /wenza mitandaoni ni pamoja na:-

1.Uongo
Watu hudanganya sana mitandaoni,hudanganya umri,kazi wanazofanya,hali zao kimahusiano (marital status),urefu, uzito n.k. Wengine hutuma hata picha zisizo zao. Hivyo unapotafuta kuwa makini sana.

2.Utapeli na wizi
Kuna watu hutumia sana mianya hiyo kutapeli na kuibia watu mali zao. Hii imenikuta mara mbili. Nilitapeliwa na watu niliokutana nao mitandaoni.

3.Kupoteza muda
Wakati mwingine huu utafutaji hupelekea kupoteza muda mwingi kuwasiliana na watu. Hii ni kutokana na kuwa na watu wengi mno wa kuwasiliana nao.

Hizo ni baadhi tu ya sababu,faida na changamoto za utafutaji wa marafiki/wachumba/wenza mitandaoni. Karibuni muongezee nyingine.....
 
Duuh,yataka moyo wakipekee kupenda mtu usiyemjua wala kujua anafananaje.
Mkuu,sio swala la kusema natafuta mwenza kisha baada ya wiki moja mnakutana na kufunga ndoa.
Unapotafuta kuna hatua kadhaa zinafauata mpaka kuchipuka kwa penzi! Mnawasiliana kwanza kwa kuchat na kupigiana simu,baadae mnatumiana picha kisha mnaonana ana kwa ana.
Kwahiyo,wakati mwingine kuna mtu mnaishia hatua ya awali kabisa ya kuchat hata bila picha yake unajua tu kuwa huyo mtu anamtazamo gani!
 
Mkuu,sio swala la kusema natafuta mwenza kisha baada ya wiki moja mnakutana na kufunga ndoa.
Unapotafuta kuna hatua kadhaa zinafauata mpaka kuchipuka kwa penzi! Mnawasiliana kwanza kwa kuchat na kupigiana simu,baadae mnatumiana picha kisha mnaonana ana kwa ana.
Kwahiyo,wakati mwingine kuna mtu mnaishia hatua ya awali kabisa ya kuchat hata bila picha yake unajua tu kuwa huyo mtu anamtazamo gani!
Nmekuelewa mkuu,lakini mi nazungumzia hyo hatua ya kwanza kabisa ya kuchat,unaanzaje kudevelop hisia kwa mtu humu,mind you wengi tunatumia fekero kuanzia majina mpaka avatar so najaribu kudadisi wenzangu wanawezaje, namie nijaribu bahati yangu
 
Nmekuelewa mkuu,lakini mi nazungumzia hyo hatua ya kwanza kabisa ya kuchat,unaanzaje kudevelop hisia kwa mtu humu,mind you wengi tunatumia fekero kuanzia majina so najaribu kudadisi wenzangu wanawezaje, namie nijaribu bahati yangu
Hujaona members wanavyodai kupendana humu kwa sababu tu ya michango ya aina fulani inayotolewa. Ili umpende mtu lazima muwe mna share interest,kwa kuchat tu mnaweza kujua kama mna interest sawa au la!
Nmekuelewa mkuu,lakini mi nazungumzia hyo hatua ya kwanza kabisa ya kuchat,unaanzaje kudevelop hisia kwa mtu humu,mind you wengi tunatumia fekero kuanzia majina mpaka avatar so najaribu kudadisi wenzangu wanawezaje, namie nijaribu bahati yangu
 
inawezekana mkuu.. wapo wanaofanikiwa 100% na ndoa zinafungwa bila shida.. ila sasa changamoto ni kumjua vizuri mwenzio huko alikotoka... mtu anaweza kukaa na siri mpaka unafunga ndoa ndo unajua!
 
inawezekana mkuu.. wapo wanaofanikiwa 100% na ndoa zinafungwa bila shida.. ila sasa changamoto ni kumjua vizuri mwenzio huko alikotoka... mtu anaweza kukaa na siri mpaka unafunga ndoa ndo unajua!
Kufichana siri na kufeki maisha ni hulka tu ya mtu,wapo wanaokutana kazini,kanisani n.k lakini wanaishi kwa kuficha makucha hadi baada ya ndoa ndo huyaonesha makucha yao. Kuna jirani yangu alimpata mchumba anayefanya nae kazi,siku ya harusi akaibuka jamaa kupinga ndoa kwakuwa bibi harusi ni mkewe wa ndoa na alikuja na ushahidi uliokamilika.
Kwahiyo hata tunaokutana nao mtaani pia wanamadhaifu mengi tu. Kikubwa ni kuwa makini na kumwomba Mungu akuongoze katika hilo.
 
Kufichana siri na kufeki maisha ni hulka tu ya mtu,wapo wanaokutana kazini,kanisani n.k lakini wanaishi kwa kuficha makucha hadi baada ya ndoa ndo huyaonesha makucha yao. Kuna jirani yangu alimpata mchumba anayefanya nae kazi,siku ya harusi akaibuka jamaa kupinga ndoa kwakuwa bibi harusi ni mkewe wa ndoa na alikuja na ushahidi uliokamilika.
Kwahiyo hata tunaokutana nao mtaani pia wanamadhaifu mengi tu. Kikubwa ni kuwa makini na kumwomba Mungu akuongoze katika hilo.
mi naona ni vizuri kama una siri uifiche moja kwa moja sababu kama ukapata bahat ya kuolewa halaf ukaonyesha makucha ujue umejiharibia mwenyewe!!!!
 
Hujaona members wanavyodai kupendana humu kwa sababu tu ya michango ya aina fulani inayotolewa. Ili umpende mtu lazima muwe mna share interest,kwa kuchat tu mnaweza kujua kama mna interest sawa au la!
Anhaa nmekusoma,tatizo sie wengine matomaso.
 
woga pia ni akili! Maana mitandaoni ni kama baharini unaporusha nyavu chochote waweza kukivua,wawezapata samaki au joka
Kweli dadaangu.online dating nimeanza kitambo sana nadhani 2003 au 2002,nlikuwa kadogo lakini tulikuwa na access ya internet 24/7,enzi hizo ilikuwa yahoo mesenger ndo habari ya mjini,ikaja myspace,msn,Aol,bongo nao wakaanzisha marafiki dot com. Ikaja tagged baadae tukahamia kwenye simu migg33,facebook 2007 etc.uzoefu ninao wa muda mrefu tu.mara ya mwisho nlikuwa natumia tinder.ila naona uzito kweli kuchat skuiz sjui ndo uzee.nahisi nisababu nlianza kuchat kabla hata sijabalehe so I have never been there looking for love,just foolin around and whatnot
 
Kweli dadaangu.online dating nimeanza kitambo sana nadhani 2003 au 2002,nlikuwa kadogo lakini tulikuwa na access ya internet 24/7,enzi hizo ilikuwa yahoo mesenger ndo habari ya mjini,ikaja myspace,msn,Aol,bongo nao wakaanzisha marafiki dot com. Ikaja tagged baadae tukahamia kwenye simu migg33,facebook 2007 etc.uzoefu ninao wa muda mrefu tu.mara ya mwisho nlikuwa natumia tinder.ila naona uzito kweli kuchat skuiz sjui ndo uzee.nahisi nisababu nlianza kuchat kabla hata sijabalehe so I have never been there looking for love,just foolin around and whatnot
Bila shaka una uzoefu wa kutosha. Naomba u share nasi uzoefu wako ili kusaidia watumiaji wapya. Vp kuna changamoto zozote ulizokutana nazo au kuna manufaa yoyote uliyoyapata kupitia huko,na mengineyo!
 
Bila shaka una uzoefu wa kutosha. Naomba u share nasi uzoefu wako ili kusaidia watumiaji wapya. Vp kuna changamoto zozote ulizokutana nazo au kuna manufaa yoyote uliyoyapata kupitia huko,na mengineyo!
Ngoja nmalize kupata lunch nakuja
 
Bila shaka una uzoefu wa kutosha. Naomba u share nasi uzoefu wako ili kusaidia watumiaji wapya. Vp kuna changamoto zozote ulizokutana nazo au kuna manufaa yoyote uliyoyapata kupitia huko,na mengineyo!
Am back changamoto ziko nyingi sana kwenye online datin1.ntajntabu kuziorodhesha baadhi

1.Catfishing.mtu kutumia persona ya mtu mwengine,mfano mwakukke uko online unajua unachat na hamorapa kumbe unachat na rayvanny mwisho wa siku mnakuja kukutana inakuwa tafrani.au unajua unachat na Tulia A kumbe unachat na kidoti.
 
Back
Top Bottom