Unamzungumziaje Baba Yako

Unamzungumziaje Baba Yako

Mrs Gudman

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2015
Posts
613
Reaction score
1,300
Habari zenu wanna jf
Katika kuazimisha siku ya kina baba duniani Leo tujadili kidogo namna unavyoweza kuzungumza juu ya baba yako.
Binafsi kwa upande wangu toka nikiwa mtoto namfahamu baba yangu Kama mtetezi ,mlinzi na mtunzaji ,kiongozi,mwalimu na msemaji mkuu wa familia

Sitaki kuimagine maisha bila baba(though Kuna wengine wamepitia maisha hayo Mungu awatie nguvu sana ,R.I.P).

Nakumbuka nilifika darasa la tatu bila kujua kusoma ila baba aliamua kuanzisha darasa maalum nyumbani Hadi nikajua kusoma.

Katika maisha yangu yote ya kusoma baba alisimama Kama advicer,mwelekezi ilikuwa ni ngumu Mimi kuanza mitihani wowote kuanzia secondari Hadi chuo baba asifahamu na asijue nimepata ufaulu gani.

Ukisafiri kutoka mkoa mmoja Kwenda mwingine simu za baba zinakuwa hazipumziki dar chalinze anaweza kuwa amekupigia Mara tatu zote kutaka kujua Safari inaendeleaje na kujua tu usalama wako , wakati mwingine inachoshaga,Kuna wakati watoto tukiwa na Safari tunaamua tusimjulishe baba(kwa kuwa wote hatupo mikononi mwake Tena) ili tu awe na amani asisumbuke kutupigia pigia simu ,Ni Hadi nilipoanza kuwa mama ndipo nimeanza kumuelewa babangu,nami nikiwa job naweza piga simu zaidi ya Mara nne kujua mwanangu ana Hali gani

Namshukuru Mungu kwa ajili ya uwepo wa baba yangu duniani,umenifundisha upendo kujali Mungu akinijalia mtoto wa kiume Basi Nitakuwa na mengi ya kuwaambia Kama wababa watarajiwa,waume za watu nk.

Katika kusherekea siku hii muhimu namwombea sana Mungu aendelee kumtunza, maisha bila baba sijui itakuwaje ,Mungu wa mbingu na nchi msaidie baba yangu aishi miaka ya kutosha.


Happy Father's day
#Unamzungumziaje baba yako?!
#Poleni Sana watoto mliozaliwa na wababa Vimeo Mungu awe baba yenu
 
My dearest father..
Pamoja na machungu mengi na kufanya maisha yetu kuwa magumu, tukinyanyasika na kupigwa danadana na ndugu ilhali wewe ulikuwa hai ukitumbua na vimada wa kila aina....

Pamoja na kumtesa mama, kumpiga kumnyanyasa, kumdharau, kumdhalilisha na hatimae mauti yakamkuta na wala usiende kumzika.....

Bado ninacho cha kukushukuru, asante kwa kunileta duniani. Asante kwa kunipitisha kwny tanuri la moto toka nikiwa mdogo, imenisaidia kuishi na watu wa kila aina.

Thank u for shaping my life father. I hope upo mahali palipokustahili. May u rest in peace.....

Happy fathers day.
 
My dearest father..
Pamoja na machungu mengi na kufanya maisha yetu kuwa magumu, tukinyanyasika na kupigwa danadana na ndugu ilhali wewe ulikuwa hai ukitumbua na vimada wa kila aina....

Pamoja na kumtesa mama, kumpiga kumnyanyasa, kumdharau, kumdhalilisha na hatimae mauti yakamkuta na wala usiende kumzika.....

Bado ninacho cha kukushukuru, asante kwa kunileta duniani. Asante kwa kunipitisha kwny tanuri la moto toka nikiwa mdogo, imenisaidia kuishi na watu wa kila aina.

Thank u for shaping my life father. I hope upo mahali palipokustahili. May u rest in peace.....

Happy fathers day.
Jamani pole sana ,pumzika kwa amani mama na baba
 
Back
Top Bottom