Unamkumbuka yule ex?

Unamkumbuka yule ex?

Analyse

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2014
Posts
17,641
Reaction score
47,660
Mahusiano yakifa, kila mmoja huwa anaelezea habari mbaya za aliyekuwa mpenzi wake, yale mazuri yote yalifutika mapenzi yalipoisha.

Jamaa analalamika jinsi gani ameweza kumpangishia nyumba mpenzi wake, alaf mpenzi wake nae ameleta mpenzi wake wanaishi kwa kodi ya jamaa.

Kuna dada analalamika kuhusu yule boyfriend wake ambae walikuwa washatambulishana hadi kwa wazazi, ila ghafla jamaa amebadili mawazo na kuwa kivuruge.

Kwa ufupi kila mtu anajaribu kuelezea jinsi mapenzi yalivyomtenda. Ila ngoja nikuulize swali mkuu:

UNAMKUMBUKA YULE EX WAKO?

Yule ambae pamoja na upendo wote aliokuwa nao kwako, ila ulimuona hafai ukampiga chini bila sababu ya msingi? Namaanisha yule ambae ni muda mrefu sasa tokea muachane nae, ila mpaka leo akiulizwa kwanini mliachana wala hajui sababu, maana hukumpa sababu ya kueleweka? Yeah huyo ndio nakuuliza, UNAMKUMBUKA?

Sasa basi, jinsi ambavyo unasota katika mahusiano ya sasa, au jinsi ambavyo unaumia kwa uliyopitia hivi karibuni, basi kipindi kile pengine aliumia zaidi ya hivi.

Mkuu nakuuliza tena, Unamkumbuka yule ex wako? Yeah yule ambae alijituma kama mke kwako japo hakujulikana kwenu wala kwao hawakukujua. Eti dada angu, hivi bado unamkumbuka yule aliyekuwa anasimamia shoo za mahitaji yako as if ni mzazi wako ila ghafla ukaamua kutemana nae. Analyse nimemkumbuka leo ndio maana nimeonelea nikuulize na wewe:

Unamkumbuka yule ex wako?

Quick reminder wakuu ni kwamba : "We are all bad in someone's story" so punguza kulalamika yakikukuta, hata wewe ulishawahi kumliza mtu.

Stop live in time, live in moments. Ukiumia lia, ila ikija happy moment basi fatana nayo furahia to the max. Ila ukijifanya unazikwepa good moments eti kwavile upo kwenye bad time, YOU WONT BE HAPPY FOREVER

Hakuna anayefanya ubaya akiwa anaamisha kufanya hivyo, watu wanakuwa wanajaribu kutafuta furaha.

Analyse

#Baharia_wa_nchi_kavu
 
Hatari man, mm namkumbuka ma x kibao hata sina idadi kamili lakini kuna mmoja huyo Happy daaah huyu mtoto sintamsahau kamwe. tulikuja kuzinguana yeye akasepa ila namkumbuka sana
Namzungumzia yule ambae ulimuumiza bila kujali.
 
Iko poa kwa namna yake uzi umetulia UNAMKUMBUKA YULE EX WAKO

Sasa najiuliza kuna wale mnachana wala amjambiana mnakuta tyu mmeachana iyo inakaaje kitaalam
 
Iko poa kwa namna yake uzi umetulia UNAMKUMBUKA YULE EX WAKO



Sasa najiuliza kuna wale mnachana wala amjambiana mnakuta tyu mmeachana iyo inakaaje kitaalam
Na ilo ndio swali mkuu, unamkumbuka?
 
Uyo kweli umemkumbuka mkuu aseee
Aise kuna wanawake Mungu anakupa kama bure hivi sema ujinga wetu wanaume tunaharibu wenyewe, Happy wangu alinifanya nikaona mapenzi ni matamu yani nipo mimi tu katika hii dunia . Aise sijui kama ntapata mwanamke kama Happy .

Happy whatever your nakupenda sana Mungu akubariki kwa uliyonitendea ila mimi ndio niliharibu mwenyewe .
 
Namzungumzia yule ambae ulimuumiza bila kujali.
Yaani nilimpiga matukio kila siku mpaka ikafikia hatua siku moja alikuja ghetto akanitegea nimeenda kuoga akachukua simu zangu zote mbili, akaondoka nazo nilijaribu kumuomba lakini alikataa , alikaanazo wiki moja nzima hata nywila zake alikuwa anazijua vyema (password)

Kilichofuata akanirudishia wiki moja baadae nikashangaa sijapigiwa simu wala text siku mbili kumbe kila mtu alitukanwa kwenye simu kwanzia masela mpaka mademu wote alikuwa anapiga msela anamuuliza huyu mwenzenu anamademu wangapi msela asipojibu anaogeshwa matusi mpaka basi yaaaaan balaaah ......
 
Yaani nilimpiga matukio kila siku mpaka ikafikia hatua siku moja alikuja ghetto akanitegea nimeenda kuoga akachukua simu zangu zote mbili, akaondoka nazo nilijaribu kumuomba lakini alikataa , alikaanazo wiki moja nzima hata nywila zake alikuwa anazijua vyema (password)

Kilichofuata akanirudishia wiki moja baadae nikashangaa sijapigiwa simu wala text siku mbili kumbe kila mtu alitukanwa kwenye simu kwanzia masela mpaka mademu wote alikuwa anapiga msela anamuuliza huyu mwenzenu anamademu wangapi msela asipojibu anaogeshwa matusi mpaka basi yaaaaan balaaah ......
Nikirudi nimelewa pombe zangu akija ghetto ananiambia sogea hapa ananinusa mdomoni anaanza kulia aise kuna matukio nikikumbuka najua tu yule ndio alikuwa mke wangu sema nilizingua .

Narudi nimelewa mwanamke analia ananiambia kwanini unakuywa pombe nimekukataza sana husikii nk , akishamaliza hapo ety ananikagua kama nime kwich kwich kwanzia chupi mzee inakaguliwa kama daktari , akimaliza napewa mpka basi mpaka nasema ntakufa Mama .

Huyo narudi zake kwao akishajua nimechoka mpaka nataka kufa ndio ananiacha aise huyu mwanamke acheni tu .
 
Back
Top Bottom