Unamiliki silaha ili iweje?

Mshana wewe uwe unalala. Naona umepost saa 10: 48 usiku! I salute you!
 
mshana jr, je kipi bora kumiliki kati ya kinga za kishirikina na mabunduki ?
 
Nyika-one umeongea vizuri sana, nakubaliana na hoja yako 100%.Kumiliki silaha haimaanishi kuwa haumwamini Mungu. Barikiwa ndugu
 
Hivi ule uhakiki wa silaha kwa wakazi wa Dar uliishia wapi maana nilimuona mkuu wa Kaya peke yake akiwa anahakikiwa au movie ilikuwa inaendelea. [emoji41] [emoji41] [emoji41]
Hahaahaha kwani hujazoea maigizo yetu mkuu bado???
 
Nyika-one umeongea vizuri sana, nakubaliana na hoja yako 100%.Kumiliki silaha haimaanishi kuwa haumwamini Mungu. Barikiwa ndugu
Dhima ya kumiliki silaha ninini?
 
upo vizuri sana
 
Haya ndio madhara ya kukaa na silaha ndani
1.Jamaa mmoja hapa Dar aliwakurupusha majambazi waliotaka kuiba kwa jirani yake kwa kupiga risasi tatu juu
Siku iliyofuata usiku wa saa mbili jamaa walimvamia jamaa akiwa kakaa sebuleni na kumtoboa macho mbele ya familia yake

2. Jamaa mwingine yeye alipishana lugha na mkewe usiku wakiwa wamelala jamaa akatishia kumpiga mkewe risasi, ni katika purukushani za kupokonyana silaha jamaa alimpiga ya tumboni mkewe na kufa muda mfupi baadae, mpaka leo yupo segerea

3. Hii niliishuhudia live tulienda kumtembelea jamaa yetu siku moja jumapili mchana , tukiwa tumekaa sebuleni akatoka chumbani mwanae wa kiume wa umri wa miaka 5 hivi kaelekeza bastola kwa baba yake
Mwanzoni tulidhani ni toy lakini kumwangalia jamaa alivyotoa macho ya woga tukajua kuna hatari
Mtoto akawa anamwambia babaake Dad hands up wote tulikuwa kimya
Aliyeokoa jahazi ni mdada wa kazi aliyekuja kwa nyuma na kuikamata silaha na kuelekezea juu ambapo ili fire[emoji134] [emoji134] [emoji134] [emoji134]
Kumbe jamaa analala na ile silaha na kuiweka tayari kwa kupiga ila asubuhi huirudisha kabatini lakini siku hiyo akapitiwa, siku iliyofuata jumatatu jamaa aliipeleka police ikauzwe

Tunapaswa kujihami tunapaswa kujilinda lakini ulinzi wetu Usiwe chanzo cha maafa na matatizo
Tunajenga nyumba na kuziwekea ulinzi mkali mpaka zinageuka gereza la kifo badala ya nyumba
Tunakuwa na silaha za hatari ndani ya nyumba kwa ajili ya kujilinda lakini ni silaha hizo hizo hutuletea maafa wenyewe
Tunakuwa na mazindiko mbalimbali na mahirizi makubwa yanayotufanya tuingie kwenye maagano yenye madhara makubwa halafu Tunakufa na malaria
Bado ulinzi wa Kimungu ndio ulinzi bora kuliko mwingine wowote ule..vyovyote iwavyo usisahau Mungu ndo mweza wa yote na vyote
 
Mungu yupo na ndiye anayetulinda dhidi ya hatari zote, lakini lazima na sisi tujitume ktk ulinzi wetu. kila kitu kina sababu ya kukianzisha. ikiwa huna hatari(risk) ya kuvamiwa huhitaji silaha hizo za moto. ila watu kama wafanyabiashara wakubwa na viongozi wakubwa wanapaswa kuwa nazo ili kujilinda. uhai wa binadamu ni wa thamani kubwa ulindwe kwa nguvu yoyote inayowezekana. kumiliki silaha kwa ajili ya ulinzi wa uhai si kupingana na hoja ya kumtegemea Mungu bali ni udhihirisho wa kutenda atakayo Mungu yaani kuulinda uhai
 
hizo ni ajali tu kama zilivyo ajali nyingine. watu wasipomiliki silaha madhara ni makubwa zaidi! tafakari vizuri kama hoja yako umeitoa moyoni.
 
hizo ni ajali tu kama zilivyo ajali nyingine. watu wasipomiliki silaha madhara ni makubwa zaidi! tafakari vizuri kama hoja yako umeitoa moyoni.
Ni kweli mkuu. Tena ajali alizotolea mfano Mshana Jr ni zile ambazo kwa kiasi kikubwa zimetokana na aidha uzembe au matumizi mabaya ya silaha. Hiyo ya jamaa kumtishia mke wake kwa bastola ni matumizi mabaya ya silaha kama ilivyo matumizi mabaya ya barabara kwa madereva. Na kwa upande wa mfano wa mtoto aliyetoka chumbani na bastola hadi sebuleni huo ni uzembe wa mmiliki ambao hautakiwi.
 
Mkuu kuna mazingira mengine silaha inakuaga muhimu sana...mi shambani kwangu usalama si mkubwa sana hasa nyakati za usiku kwa hiyo nafikiria ipo siku ntanunua kwa ajili hiyo maana sometimes nakua kule mpaka usiku... najua nikipiga moja tu hewani I'll shy them burglars away
 
Dunia ya leo mkuu wote tukiwa na mawazo kama yako mshana jr. Magaidi watatawala dunia na mauaji ya watu wasio na hatia yataongezeka
 
asante sana mshana maana kuna jamaa alitaka kunipeleka mahali nikatengenezewe kitu mahalumu cha kunilinda sasa sitaenda tena itanibidi nibaki na ulinzi wa mungu tu
 
Uwepo wa Mungu na kumiliki silaha hakufungamani wala kuleta conflict kama unayotaka kuelezea. Nitamuomba Mungu sawa, lakini wezi na wanyama wakali wanapokuvamia, utawakabili au utaanza maombi?

Huku tuendako, utasema tusijishughulishe kujifunza namna ya kuvuka barabara kwa kuwa Mungu atatulinda tusigongwe. Badala yake, ulipaswa kuwaasa watu wamuombe Mungu awape hekima ya matumizi ya silaha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ