Unakumbuka MAJAMBO kiboko ya Vikojozi mtaani?

Unakumbuka MAJAMBO kiboko ya Vikojozi mtaani?

Chemwali

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2011
Posts
397
Reaction score
178
hivi mnamkumbuka muuza karanga maarufu kiboko ya vikojozi wengi mitaani Majambo?yaani nakumbuka mdogo wangu mkimwambia majambo huyooo atajifungia kabisa chumbani kwa kilio na kutetemeka
 
we uliishi mitaa ipi?
unazungumza as if watu wote humu waliishi mitaa ya kwenu
mi namjua mzee majambo but wengi humu hawamjui
 
we uliishi mitaa ipi?
unazungumza as if watu wote humu waliishi mitaa ya kwenu
mi namjua mzee majambo but wengi humu hawamjui
Boss ,yule mzee alikuwa anatembea bwana na karanga zake nasisitiza yule mzee alikuwa anatembea na alikuwa entertainer mzuri tu pamoja na mpiga zeze mmoja bosco kanyau!
Wakazi wooote wa uswazi watakuwa wanamfahamu ila kweli maeneo yenu ya masaki ,mikocheni o-bay alikuwa atimbi!
 
Majambo alikua anakatiza mitaa yooote na manyoya yake nakumbuka nlikua namuogopa lakini nlikua nataka nimuone anavyocheza kwa hiyo sikai mbali na baba maana nlikua nina imani hawezi kunidhuru kama niko benet na baba , basi ukinunua karanga anachezaaa na kuimba lol!
 
hivi mnamkumbuka muuza karanga maarufu kiboko ya vikojozi wengi mitaani Majambo?yaani nakumbuka mdogo wangu mkimwambia majambo huyooo atajifungia kabisa chumbani kwa kilio na kutetemeka
Dah!! Umenikumbusha mbali sana
mkuu. Miaka ile nipo mitaa ya Kino, ilikuwa akitokea Mwananyamala lazima apite Kino then anashuka zake Migomigo. Unanunuwa karanga halafu anacheza ngoma. Mara baadae nikaanza kusikia, ooh! huyu mzee usalama wa taifa. Si unajua kipindi kile. Kipindi hicho Dar tuko pekeyetu, kabla mamluki hawajafika. Ilikuwa safi sana.
 
hivi mnamkumbuka muuza karanga maarufu kiboko ya vikojozi wengi mitaani Majambo?yaani nakumbuka mdogo wangu mkimwambia majambo huyooo atajifungia kabisa chumbani kwa kilio na kutetemeka

We ni short sighted, mambo ya mtaani kwenu ndio unaleta hapa? Majambo ni kitu ghani?
 
Kino ni wapi? Kabanga nawe kwani tanzania yote ni Dar?

Mkuu acha wakumbushane yaliyopita, namkumbuka vyema yule bwana alikuwa akifika mtaani kwetu watoto wanakusogelea kwa ajili ya kutafuta kinga na ili uwanunulie karanga wapate kuona pia akicheza ila palikuwa hapatoshi pale anapoonyeshwa kikojozi inakuwa balaa kwa mtoto.
 
Majambo..kapita sana mikocheni nilikuwa naenda kwa babu kushinda kila wkend nilikuwa sili chakula basi nikiambiwa majambo anakuja lazima nikimalize..nilikuwa nalia sana lakini mitaa ya home sinza alikuwa anapita kwa nadra sana..
 
hivi mnamkumbuka muuza karanga maarufu kiboko ya vikojozi wengi mitaani Majambo?yaani nakumbuka mdogo wangu mkimwambia majambo huyooo atajifungia kabisa chumbani kwa kilio na kutetemeka
Haa kwa jinsi unavyokumbuka mambo ya zamani..mbona hatari.
 
we uliishi mitaa ipi?
unazungumza as if watu wote humu waliishi mitaa ya kwenu
mi namjua mzee majambo but wengi humu hawamjui

Hahahaha nilikaa magomeni mikumi,then kuna aunt yangu alikuwa anakaa knyama tukienda likizo anapita pia..family friend wetu alikuwa anakaa kinondni sijui mwananyamala pia alikuwa anapiata
 
Dah!! Umenikumbusha mbali sana
mkuu. Miaka ile nipo mitaa ya Kino, ilikuwa akitokea Mwananyamala lazima apite Kino then anashuka zake Migomigo. Unanunuwa karanga halafu anacheza ngoma. Mara baadae nikaanza kusikia, ooh! huyu mzee usalama wa taifa. Si unajua kipindi kile. Kipindi hicho Dar tuko pekeyetu, kabla mamluki hawajafika. Ilikuwa safi sana.
hahaha nakumbuka nami kuambiwa kwamba jamaa alikuwa usalama wa Taifa..wengine wakawa wanadai ni tajiri kinoma sijui ana nyumba ngapi mjini
 
nakumbuka nilikuwa mdogo kitambo hicho,nilikuwa naogopa minyoya yake kichwani na manyanga miguuni,karanga zake zilikuwa tamu,basi huyu babu alikuwa anazunguka daslam nzima sababu mwembechai almost kila siku alikuwa anapita,..nimemkumbuka na tekelo ghafla.
 
hahaha nakumbuka nami kuambiwa kwamba jamaa alikuwa usalama wa Taifa..wengine wakawa wanadai ni tajiri kinoma sijui ana nyumba ngapi mjini
Yaah! Nakumbuka hilo swala la utajiri. Wa makamu walikuwa wanatuambia "msimdharau huyu mzee, ana nyumba kibao". Si unajuwa mentality aliyotupa Mchonga!!!! Nyumba ndiyo mpango mzima. Basi mtu unapata inspiration flani hivi mixer flag kwa Majambo, unatamani na wewe uuze karanga upate nyumba. Those days bwana!!!! Those days watoto wengi walikuwa na matovu makubwa. Lakini sikuhizi siwaoni watoto wenye vitovu vikubwa. Halafu Majambo alikuwa story ya jiji, coz kipindi kile uko kwenye Ikarus (mtu ataulizi ndiyo nini hiyo) kitu nyomi, kuchungulia dirishani unamuona Majambo yuleee anakula Morogoro road kwa ngondi. Probably coverage yake ilikuwa si ya kitoto. Lakini nashangaa watu kibao humu kama vile kitu cha mkunga....halafu reli ya kati niniii......hahahahaaa!!!!
 
Back
Top Bottom