Unajua satellite ni nini?

Unajua satellite ni nini?

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
1,221
Reaction score
2,425
Umeshawahi kujiuliza kuhusu satellite kwenye huu ulimwengu wa dunia ni Nini ?

Najua watu wengi mlikua hamjui angani Kuna zaidi ya satellite 6542 zilizo active ni 3372 wakati 3170 haziko active ila je iyo satellite ni kitu gani?

Satellite tunaweza sema ni mwezi , sayari, mashine inayozunguka sayari au tunaweza sema ni nyota.mfano dunia ni satellite kwa sababu inazunguka Jua, pia mwezi ni satellite kwa sababu inazunguka Dunia.

Kwa kawaida Neno satellite ni mashine inayorushwa angani na kuizunguka Dunia au kitu chengine Chochote angani. Mfano Dunia na mwezi ni satellite za asili. Pia Kuna maelfu ya Satellite bandia zinazotengenezwa na binadamu ambazo huzunguka Dunia.

Kupitia Satellite watu huweza kupata picha za sayari ambazo zinawasaidia sana watu kutabiri mfumo wa Hali ya hewa na masuala ya vimbunga. Wengine wakipata picha mbalimbali za sayari nyingine, Jua , mashimo meusi , vitu vyenye Giza nk picha hizi huwasaidia sana wana sayansi kuelewa vyema mfumo wa jua na ulimwengu.

Pia satellite zinatumika kwa ajili ya mawasiliano ,kama vile mtu kupata mawimbi kwenye Tv (signal) pamoja na kupiga simu ulimwenguni kote. Nje ya Dunia Kuna zaidi ya satellite 20 kazi zake ni kuunda mfumo wa kuweka Gps Kupitia hizo Satellite tunajua mtu Yuko wapi gani kwa sasa kupitia kifaa chako.

Unajua Satellite husaidia watu kuweza kukusanya data za eneo Fulani kwa haraka zaidi kuliko vifaa vilivyopo kwenye ardhi kwani kwenye satellite huwezesha watu kuona maeneo makubwa ya Dunia kama vile angani , ardhini kwa wakati mmoja.

Kabla ya Satellite , mawimbi yanayotoka kwenye Tv yalikuwa hayaendi mbali sana kwa sababu mawimbi ya Runinga usafiri kwenye mstari uliyonyooka pekee. Kwaiyo kwenye majengo , marefu , milima na Kupiga simu maeneo mbalimbali kulikua changamoto.

Kupitia Satellite sasa mawimbi huweza kusafirishwa mpaka juu kwa haraka zaidi papo hapo, Kisha satellite huweza kusafirisha kwenye maeneo mengine uyatawanya sehemu tofauti tofauti duniani.

Satellite ziko za aina mbalimbali kuanzia maumbo na size, watu wengi wanamiliki za aina mbili ambazo zinafanana antenna na power source. Antenna hutuma na kupokea taarifa, mara nyingi kwenda na kutoka duniani.

Wakati power source inaweza kuwa solar paneli ya jua au betri. Solar Paneli za jua hutengeneza nguvu kwa kugeuza mwanga wa jua kuwa umeme. Ila satellite nyingi zilizopo nje ya Dunia hubeba kamera na sensor za kisayansi

hivyo huelekezwa kwenye hii Dunia ili kuchukua taarifa mbalimbali kuhusu ardhi , hewa na maji. Wakati mwingine huelekeza angani ili kukusanya data kutoka kwenye Jua na mifumo mingine.

Source nasa
 
Mkuu kwa unachokijua juu ya satelite ni sawa na mtoto wa chekechea kuwaelezea kaka zake wa darasa la saba jinsi ya kukokotoa hesabu rudi tena darasani tunataka maarifa umetoa kidogo mnooo
 
Picha tafadhali, Kule Tanga kuna gari inaitwa Satelait
 
Fact, yaani maelezo ya jamaa yanafurahisha sana. Kagoogle haraka haraka tu, na kutranslate, Kisha kuleta huku.
Mkuu kwa unachokijua juu ya satelite ni sawa na mtoto wa chekechea kuwaelezea kaka zake wa darasa la saba jinsi ya kukokotoa hesabu rudi tena darasani tunataka maarifa umetoa kidogo mnoo
 
Back
Top Bottom