Unajua nini kuhusu Mamajusi?

Unajua nini kuhusu Mamajusi?

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2017
Posts
1,605
Reaction score
1,957
Wadau wa JF
Mamajusi ni neno la Kiswahili ambalo limetokana na Kiarabu 'majus' lililopokelewa kutoka Kiajemi cha kale kupitia Kigiriki.Kwa asili neno hili lilimaanisha makuhani wa dini ya Uajemi ya Kale, hasa wafuasi wa Zoroaster.
Wagiriki hao waliamini ya kwamba makuhani hao walikuwa na elimu ya siri hasa kuhusu nyota na utabiri wa nyota.Kwa hiyo katika lugha kadhaa neno limeendelea kumaanisha ama wanajimu au watu waliojua fani za ushirikina.

*Matumizi yake ya kawaida leo*
Leo kwa kawaida jina hilo linatumika kuwataja watu wa namna hiyo ambao kadiri ya Injili ya Mathayo (2:1-12) walitokea mashariki kwa Israeli wakifuata nyota ya pekee ili kumfikia Mfalme wa Wayahudi aliyezaliwa, yaani Yesu. Walipofika Yerusalemu kwenye ikulu ya Herode Mkuu walimfanya afadhaike kwa habari hiyo, lakini walielekezwa Bethlehemu kadiri ya utabiri wa nabii Mika. Walifika na kumkuta mtoto Yesu akiwa na mama yake, Bikira Maria, wakamtolea zawadi: dhahabu, ubani na manemane.Halafu wakaonywa wasimrudie Herode, bali warudi kwao kwa njia nyingine.
Kumbe Herode, alipoona hawarudi, akikusudia kumuua mtoto, aliagiza wauawe watoto wote wa kiume wenye umri chini ya miaka 2 katika eneo la Bethlehemu.

Liturujia ya madhehebu mbalimbali ya Ukristo inakumbuka ujio wa mamajusi kwa Yesu kama mwanzo wa maandamano ya watu wa mataifa wanaokuja kumuabudu.Sikukuu husika inaitwa Epifania, yaani Tokeo.
Kwa kuwa mara nyingi jina hilo linatumika katika wingi, linatokea ma-majusi; baadhi ya watu wakisikia au kusoma mwanzoni mwa neno silabi dabo ma-ma wanakuja kudhani walikuwa wanawake, kumbe sivyo.
 
Aksante kwa kutukumbusha habari njema inahuisha nafsi zetu na kesho tena usiache kutukumbusha
 
Dini ya Uajemi ya kale iliyoanzishwa na Zoroaster ni mojawapo ya dini za zamani zilizoamini katika Monotheism.

Story za dini Yao zinafanana na za ukiristo na kiislamu.
 
Mmajusi mmojawapo alikuwa mweusi na alitokea Ethiopia!..Jina kama sijasahau aliitwa Simeone!.
 
Dini ya Uajemi ya kale iliyoanzishwa na Zoroaster ni mojawapo ya dini za zamani zilizoamini katika Monotheism.

Story za dini Yao zinafanana na za ukiristo na kiislamu.
Tupe kidogo habari za hao watu mkuu na sisi tujifunze hapa jamvini (unaweza kuleta uzi)
 
Dini ya Uajemi ya kale iliyoanzishwa na Zoroaster ni mojawapo ya dini za zamani zilizoamini katika Monotheism.

Story za dini Yao zinafanana na za ukiristo na kiislamu.
Zinapatikana wapi hizi story??? huenda tukapata mbivu na mbichi
 
Chuo enzi zile kuna jamaa walikua manotorious, room hawana mafuta wala sabuni, ni walevi na hawahudhurii masomo. Hela ya kujikimu yote walikua wanamalizia kwenye tungi tu.

Sasa hawa jamaa walikua wakitaka kubadili nguo anakuja room kwako anasema "mtaalam niazime shati nimeitwa kwa Dean of Students"...ukimoa shati ndo jumla utakua unapidhana nae kavaa shati lako hata wiki 2. Na akitaka suruali anaenda kwa mwingine hvo hivo

Kama anataka kula na hela hana, mida ya kula anamdandia mdada yyte anamkomalia wanaenda wote cafeteria, anamnunulia msosi au 'wanakula nae'

Hao walikuaga wanaitwa MAMAJUSI na jinsi walivokua wanapata mahitaji yao kupitia watu wengine wenyewe wakawa wanaita "kusafuria".

Mfano akimfuata "Miss Natafuta" mida ya kula mpaka amnunulie chakula akikutana na wenzie anasema "mchana NIMEMSAFIRIA miss natafuta" (yaan kama vile mamajusi walivokua wanafuata nyota mpaka wanafika kwenye kitu walichokua wanahitaji/wanasafiria nyota)
 
Tupe kidogo habari za hao watu mkuu na sisi tujifunze hapa jamvini (unaweza kuleta uzi)
Maada kama hizi hapa JF hazina wasomaji watu hawapo interested na haya mambo ndo maana kuanzisha thread inakuwaga ngumu.

Kwa ufupi tu dini hii ilianzishwa na mwanafalsafa wa kiajemi Zoroaster miaka ya 600 B.C..Zoroaster alipinga miungu ya sanamu ya kiajemi.

Akadai kulikuwa na Mungu mmoja mwenye nguvu anayetawala dunia aliyeitwa Ahura-Mazda.

Akasema Ahura-Mazda alikuwa kwenye vita ya mda mrefu na Ahriman ambaye ni baba wa uongo na maovu.Na kila binadamu anachagua upande wa kuufuata either kwa Ahura-Mazda au Ahriman.

Dini hii ilifundisha kwamba kuna siku ya hukumu.Ambapo kila mtu atahukumiwa kwa matendo yake.

Waliotenda mema wataenda mbinguni na waliotenda maovu watachomwa moto.

Kwa kujifunza zaidi tafuta kitu kinaitwa Zend-avesta.
 
Maada kama hizi hapa JF hazina wasomaji watu hawapo interested na haya mambo ndo maana kuanzisha thread inakuwaga ngumu.

Kwa ufupi tu dini hii ilianzishwa na mwanafalsafa wa kiajemi Zoroaster miaka ya 600 B.C..Zoroaster alipinga miungu ya sanamu ya kiajemi.

Akadai kulikuwa na Mungu mmoja mwenye nguvu anayetawala dunia aliyeitwa Ahura-Mazda.

Akasema Ahura-Mazda alikuwa kwenye vita ya mda mrefu na Ahriman ambaye ni baba wa uongo na maovu.Na kila binadamu anachagua upande wa kuufuata either kwa Ahura-Mazda au Ahriman.

Dini hii ilifundisha kwamba kuna siku ya hukumu.Ambapo kila mtu atahukumiwa kwa matendo yake.

Waliotenda mema wataenda mbinguni na waliotenda maovu watachomwa moto.

Kwa kujifunza zaidi tafuta kitu kinaitwa Zend-avesta.
Duh....mambo matam sana haya. Asnate mkuu, inatosha
 
Wale walikuwa wazee was busara.
Uko sahihi wise men wale walikuwa ni spiritual men.Spiritual men walikuwa wakiitwa wise men.Walikuwa na uwezo wa kuangalia climate mfano na kujua kuna tatizo gani.Mfano ukipata shamba ambalo limejaa miba mwanzo mwisho hiyo ardhi imelaaniwa na kuna roho ya umaskini usinunue eneo kama hilo.Mfano mawise men ikinyesha mvua kubwa au disaster kubwa inawezekana kuna tatizo kubwa kwenye jamii husika mfano kuna uhusiano mkubwa wa dhambi nyingi na climate change. kumbuka gharika hali ya hewa ilibadilika kukawa na climate change kutokana na dhambi za watu.Pia sodoma na gomora kulikuwa na climate change kutokana na dhambi za sodoma na gomora.Wisemen mamajusi walipotizama angani wakaona nyota isiyo ya kawaida angani inatembea walipata interpretation kuwa inaenda mahali MTU.mkubwa kazaliwa na kwa kuwa ilikuwa inatembea wakaamua kuifuata hadi kufika.Mambo ya climate change sio tu physical sehemu kubwa kuna spiritual problems. mfano kagera kumekuwa na majanga mengi mno tatizo kubwa ni spiritual sio physical au bahati mbaya.Wenyewe wanajua tatizo ni kama sodoma na gomorah au LA.kuna MTU alisema katika kila watu kumi wa watu wazima wa kagera ukimkuta MTU ambaye haumwi maradhi yatokanayo na zinaa basi atakuwa mmoja
 
Haya mambo siku hadi siku yanaibika mengine, ila sijui tutajua lakweli ni lipi kati ya haya yanayoibuka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom