Unafiki wa baadhi ya watanzania

Unafiki wa baadhi ya watanzania

mdachi mdachi

Senior Member
Joined
Mar 9, 2017
Posts
118
Reaction score
138
Watanzania tumekuwa na kaunafiki fulani na km tusipojirekebisha itatugharimu sana

Kipindi cha kikwete kwa sisi ambao tulishakuwa na ufaham wa kufuatilia mambo ya siasa, Watz walikuwa wanalalamika na kusema kuwa nibora utawala(awamu) iliyopita wakimaanisha awamu ya rais mkapa, lakin hali hiyo ilikuwepo hata kipind cha rais mkapa kuwa afadhali ya awamu iliyopita yaan ya rais mwinyi, na kipind cha mwinyi hali ilikuwa n hivyo hivyo,

Kipind cha rais kikwete hali ilikuw hivyo hivyo kwamba afadhali awamu ya mkapa maana wakaanza kusema kuwa awamu hiyo imekuwa na ufisadi mwingi yaana utawala wa kikwete umekuwa na ufisad mwingi Watanzania hatukuridhika na mema yaliyokuwa yanapatikana kipindi/awamu hiyo, tukamtukana kila tusi na mzee wa watu akawa anavumilia yote,

Tukasema ni rais anayechekacheka mpole n.k

Akatuletea chuma mzee Magu tukapelekwa mputa mputa hakuna kumsema ovyo rais ukimsema unapotezwa, hakuna mikutano ya kisiasa na wengine wakakimbilia njee za nchi km wakimbizi wa kisiasa

Hapakuwa ajira za kutosha watoto wetu wakamaliza vyuo na kuendelea kukaa nyumban tukinyang'anyana dagaa huku tukiishi angalau tuzuie kufa tu maana hali ikawa mbaya hakuna kufanya maendeleo yoyote maana watoto wamejaa nyumban baada ya kumaliza vyuo maana kamshahara kakawa hakatoshi,

Bas watz tukaleta unafiki wetu tena kwa kuanza kusema kuwa afadhali utawala uliyepita maana pamoja na ufisad uliyekuwepo ilazee kikwete aliajiri ajira za kutosha kila mwaka na karibu kila mwaka alikuwa akiongeza mishajara

Tukamkumbuka sana na mpaka siku ile ameenda bungeni kwenye uapisho wa mke wake mama salma wabunge walishangiliana sio waccm wala wapinzani huku wakiimba tumekumissssssss mzee akaona isiwe tabu akatoka njee ili wabunge wasikilizane

Sasa likatokea la kutokea mzee magu akafariki akachukua nchi mama samia,

Watanzania tunaendeleza unafiki wetu kuwa afadhali ya Magu

Sasa hali hii inaweza kuwafanya viongozi wakawa wanatupuuza kwa kujua ni kawaida yetu kulalamika na kusifia utawala uliyepita

Na wakafikiri hata wao wakitoka madarakani ndio watasifiwa ila ukiwa madarakan huwez kusifiwa

Aminini mawaambia hata huyu mama akitoka madarakani watatokea watu watasema afahadli utawala wa mama

Watanzania tuache unafiki
 
Back
Top Bottom