UNAFIKI MSIBANI. Hadi MUNGU Anasingiziwa..!

UNAFIKI MSIBANI. Hadi MUNGU Anasingiziwa..!

BEHOLD

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
5,057
Reaction score
10,731
Hii huwa inanipa shida kidogo;

Unakuta marehemu kafa kwa ugonjwa wa kujitakia au kauwawa kwa uhalifu wake, lakini utasikia BWANA alitoa na BWANA ametwaa Jina la BWANA libarikiwe;

Unakuta marehemu alikua tatizo katika jamii au hata mchango wake kama ulikuwepo ulikua hauthaminiwi, lakini utasikia Ooo Pengo aliloliacha marehemu halizibika.

Unakuta marehemu kafa kwa ugonjwa unaofahamika japo ni aibu (kwa mujibu wa jamii husika), Lakini utasikia kafa baada ya kuugua kwa muda mrefu.

NADHANI TUNAHITAJI KUBADIKIKA.
 
ni kweli.

lakini marehem akifa anakuwa mwema na maovu yote inabidi asamehewe...
 
Kama ni komba mungu amlipe anachostahiki.
 
Hii huwa inanipa shida kidogo;

Unakuta marehemu kafa kwa ugonjwa wa kujitakia au kauwawa kwa uhalifu wake, lakini utasikia BWANA alitoa na BWANA ametwaa Jina la BWANA libarikiwe;

Unakuta marehemu alikua tatizo katika jamii au hata mchango wake kama ulikuwepo ulikua hauthaminiwi, lakini utasikia Ooo Pengo aliloliacha marehemu halizibika.

Unakuta marehemu kafa kwa ugonjwa unaofahamika japo ni aibu (kwa mujibu wa jamii husika), Lakini utasikia kafa baada ya kuugua kwa muda mrefu.

NADHANI TUNAHITAJI KUBADIKIKA.

Asante kwa hii topic kuileta na huku. Maana alishaitoa siku nyingi sana wambura mtani mtangazaji wa redio free africa kwenye kipindi chake cha je, huu ni uungwana? Na kweli wanaboa sana watu wa namna hiyo acheni hizo. Unakuta mtu kibaka sugu anasumbua watu mchana na usiku hawalali leo akifa tu. Bwana ametoa bwana ametwaa bwana gani huyo? Acheni hizo
 
Nadhani humzungumzii Komba. Ila kama umemlenga Komba, hapana ndugu yangu. Huyu kijogoo ngoja akawike kwa Mola. Kala sana mademu.
 
BEHOLD
Kwa wakristo... Nabii Issa alimwokoa "Malaya" kupigwa mawe hadi kufa
 
Last edited by a moderator:
Jamani...sasa hata mkimsimamanga marehemu mtapata faida gani?? Kama alofariki hakuwa baba, mama, rafiki wala nduguyo huwez elewa maana ya kumuaga kwa staha hata kama alikuwa na mapungufu makubwa au tabia chafu.Ivi baba yako mzazi akifariki kwa ngoma lets say, kuna haja ya kuutangazia umma ikiwa yeye mwenyewe aliona iwe siri ya familia? Nadhani huu aliouleta mleta mada ni unafiki pia.Bwana ametoa na ametwaa ndio kwani uongo?
 
Back
Top Bottom