kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,253
- 16,171
Taifa linajazwa hofu ya kuvunjika kwa amani kwa maslahi ya watu wachache.
Badala ya kuwachukulia hatua watu wanaohusika na kauli na vitendo ambavyo vinaweza kuwa chanzo cha kuvunjika amani tunalijaza hofu taifa zima kwa matamasha, makongamano, mihadhara, na mikutano ya kuliombea taifa amani. Tunafanya mambo ya jumlajumla kwanini wakati wahusika wanafahamika? Huu ni unafiki mkubwa.
Watu wanaofanya kampeni za kikabila majukwaani kwa kusalimia na kuongea kikabila wanafahamika, watu wanaotukana wenzao majukwaani wanafahamika, watu wanaotoa kauli za kichochezi wanafahamika, watu wanaogombea wakiwa bado ni mawazi wanafahamika, watu wanaofanya kampeni za kidini wanafahamika, na watu wanaopanga kuiba kura wanafahamika, badala ya kuwafuata wahusika moja kwa moja na kuwaonya waache mara moja vitendo hivyo nyiye unaandaa matamasha ya kwenda kuimba nyimbo za kuliombea taifa amani. Tunamdhihaki Mungu? kwani huko ambako amani zao zimevunjika hakuna Mungu? tena kule Libya, Misri, Somalia, Syria na Iraq ndo wanakosali sana kuliko sisi, na hata mitume yetu mingi imeshawahi kukanyaga kwenye ardhi za baadhi ya nchi hizo. Mnatafuta pesa au mnamaanisha kuombea nchi amani, hebu acheni unafiki wenu, tungeni nyimbo (kama mnaweza) za kuwataja woote kwa majina wale watakaohatarisha amani yetu kwa kauli na vitendo vyao.
Hata wajumbe wa NEC, msajili wa vyama, polisi, masheikh, na maaskofu wanaongelea amani ya nchi kwa ujumlajumla tu kana kwamba nao hawawasikii wala kuwaona wanaohatarisha amani yetu. Amani ikivunjika tutalia na ninyi kwa ama unafiki wenu pia, au kutochukua hatua, bora mimi nimeandika kama sehemu ya mchango wangu wa kuelekea kudumisha amani.
Badala ya kuwachukulia hatua watu wanaohusika na kauli na vitendo ambavyo vinaweza kuwa chanzo cha kuvunjika amani tunalijaza hofu taifa zima kwa matamasha, makongamano, mihadhara, na mikutano ya kuliombea taifa amani. Tunafanya mambo ya jumlajumla kwanini wakati wahusika wanafahamika? Huu ni unafiki mkubwa.
Watu wanaofanya kampeni za kikabila majukwaani kwa kusalimia na kuongea kikabila wanafahamika, watu wanaotukana wenzao majukwaani wanafahamika, watu wanaotoa kauli za kichochezi wanafahamika, watu wanaogombea wakiwa bado ni mawazi wanafahamika, watu wanaofanya kampeni za kidini wanafahamika, na watu wanaopanga kuiba kura wanafahamika, badala ya kuwafuata wahusika moja kwa moja na kuwaonya waache mara moja vitendo hivyo nyiye unaandaa matamasha ya kwenda kuimba nyimbo za kuliombea taifa amani. Tunamdhihaki Mungu? kwani huko ambako amani zao zimevunjika hakuna Mungu? tena kule Libya, Misri, Somalia, Syria na Iraq ndo wanakosali sana kuliko sisi, na hata mitume yetu mingi imeshawahi kukanyaga kwenye ardhi za baadhi ya nchi hizo. Mnatafuta pesa au mnamaanisha kuombea nchi amani, hebu acheni unafiki wenu, tungeni nyimbo (kama mnaweza) za kuwataja woote kwa majina wale watakaohatarisha amani yetu kwa kauli na vitendo vyao.
Hata wajumbe wa NEC, msajili wa vyama, polisi, masheikh, na maaskofu wanaongelea amani ya nchi kwa ujumlajumla tu kana kwamba nao hawawasikii wala kuwaona wanaohatarisha amani yetu. Amani ikivunjika tutalia na ninyi kwa ama unafiki wenu pia, au kutochukua hatua, bora mimi nimeandika kama sehemu ya mchango wangu wa kuelekea kudumisha amani.