Apollo
JF-Expert Member
- May 26, 2011
- 4,920
- 3,244
Habari wakuu. Naamini wote ni wazima katika safari yetu ya Maisha ya sasa hapa duniani.
Nimependa kuanzisha mada hii kutokana na kuwa ni watu wachache sana walioweza kujifunza hili. Katika maisha yangu ya utafutaji na kujaribu kujifunza vitu mbalimbali nilijikuta katika hatua ambayo ilinifungua macho kwa undani sana.
Kupitia meditation, vitabu, mafundisho ya walimu wa imani na sayansi pamoja na kujichunguza nilikuja kuona kuwa Wazo/Mawazo yoyote (au thoughts kwa kingereza) yana nguvu kubwa sana katika maisha yetu. Kupitia meditation nilijifunza kuweza kukaa bila mawazo na nikajua kuwa mawazo/akili inaweza kukaa bila kufikiria chochote na ikiweza kukaa hivyo ndipo furaha inapokuja na kujitambua kunaongezeka. Pia nilijifunza kuwa wazo sio mimi. Mimi na wazo ni vitu viwili tofauti. Mwanadamu anaweza kulikubali wazo au kulikataa pale linapokuja akilini. Na mwanadamu anaweza kukaa bila wazo akilini, kitu ambacho ni kigumu kwa wengi. Hata hapo unaposoma hii post kuna wazo kichwani linacheza na linataka wewe ulikubali au ulikatae.
Ukikaa ukajiangalia au kutazama vitu vinavyokuzunguka utaona kabla ya hivyo vitu kuwa vitu vilikuwa ni viwazo/mawazo katika akili ya mtu fulani. Mfano madirisha, kifaa unachotumia kusoma hii mada, malazi, n.k vyote vilikuwa ni mawazo hapo mwanzo na vikaanza kutokea kweli na hivi sasa unaviona katika dunia ya kifizikia.
Kuna dunia ambayo ni limitedless, haina mwanzo wala mwisho, hakuna anayejua ipoje bali tunaona matokeo yake tu, na dunia hiyo ni MIND au Visualization halafu kuna dunia ya kifizikia. Ili kitu kitokee lazima kianzie katika dunia ya Wazo. Mfano helikopta hapo mwanzo ilianza kama wazo, mtu alijisemea au alihisi kitu kama helikopta (au kitu kinachoweza kupaa), halafu akatendea kazi wazo hilo (akajaribu kuunda na kutengeneza), halafu akafanikiwa na wewe leo unaiona helikopta. Pia unaweza kuchukua mfano wa kitu chochote ambacho mwanadamu amekiumba utaona kilianza kama wazo ndipo kikatokea baada ya kutendewa action.
Unaweza ukafanya zoezi la kuchunguza kila kinachokuzunguka hapo ulipo halafu hesabu ni vingapi vinavyokuzunguka ambavyo uliwahi kuvifikiria/kuvihisi/ au kuvizungumzia. Mimi naamini kuna siri kubwa katika mind ya mwanadamu.
Ni somo ambalo sio kila mmoja atalielewa lakini tambua kwa ufupi kuwa UNAUMBA KUPITIA MAWAZO, HISIA, IMANI NA MATENDO YAKO. Unapoamini jambo fulani unalifanya litokee na kila kitu kitajipangilia kama unavyoamini. Hata kama unaamini baya utalipata na hata kama unaamini zuri utalipata.
Hata sayansi inasema THOUGHTS ARE ENERGY LIKE WAVES. Chukulia mfano wa redio. Mawazo ni mawimbi ya redio na Universe ni channel. Kama una mawazo mazuri unapelekea mawimbi mazuri kukuzunguka na kuona vitu vizuri kiuhalisia.
NDIO MAANA INASEMEKANA HUWEZI KUBADILI MAISHA YAKO KAMA HUJABADILI MITAZAMO YAKO NA AKILI YAKO. TTUANGALIE MAWAZO TUNAYOWEKA KICHWANI AU VITU TUNAVYOVIAMINI KWANI VINAWEZA KUTUTAWALA NAKUKUA KATIKA DUNIA YA KIFIZIKIA.
Asanteni.
Kupitia meditation, vitabu, mafundisho ya walimu wa imani na sayansi pamoja na kujichunguza nilikuja kuona kuwa Wazo/Mawazo yoyote (au thoughts kwa kingereza) yana nguvu kubwa sana katika maisha yetu. Kupitia meditation nilijifunza kuweza kukaa bila mawazo na nikajua kuwa mawazo/akili inaweza kukaa bila kufikiria chochote na ikiweza kukaa hivyo ndipo furaha inapokuja na kujitambua kunaongezeka. Pia nilijifunza kuwa wazo sio mimi. Mimi na wazo ni vitu viwili tofauti. Mwanadamu anaweza kulikubali wazo au kulikataa pale linapokuja akilini. Na mwanadamu anaweza kukaa bila wazo akilini, kitu ambacho ni kigumu kwa wengi. Hata hapo unaposoma hii post kuna wazo kichwani linacheza na linataka wewe ulikubali au ulikatae.
Ukikaa ukajiangalia au kutazama vitu vinavyokuzunguka utaona kabla ya hivyo vitu kuwa vitu vilikuwa ni viwazo/mawazo katika akili ya mtu fulani. Mfano madirisha, kifaa unachotumia kusoma hii mada, malazi, n.k vyote vilikuwa ni mawazo hapo mwanzo na vikaanza kutokea kweli na hivi sasa unaviona katika dunia ya kifizikia.
Kuna dunia ambayo ni limitedless, haina mwanzo wala mwisho, hakuna anayejua ipoje bali tunaona matokeo yake tu, na dunia hiyo ni MIND au Visualization halafu kuna dunia ya kifizikia. Ili kitu kitokee lazima kianzie katika dunia ya Wazo. Mfano helikopta hapo mwanzo ilianza kama wazo, mtu alijisemea au alihisi kitu kama helikopta (au kitu kinachoweza kupaa), halafu akatendea kazi wazo hilo (akajaribu kuunda na kutengeneza), halafu akafanikiwa na wewe leo unaiona helikopta. Pia unaweza kuchukua mfano wa kitu chochote ambacho mwanadamu amekiumba utaona kilianza kama wazo ndipo kikatokea baada ya kutendewa action.
Unaweza ukafanya zoezi la kuchunguza kila kinachokuzunguka hapo ulipo halafu hesabu ni vingapi vinavyokuzunguka ambavyo uliwahi kuvifikiria/kuvihisi/ au kuvizungumzia. Mimi naamini kuna siri kubwa katika mind ya mwanadamu.
Ni somo ambalo sio kila mmoja atalielewa lakini tambua kwa ufupi kuwa UNAUMBA KUPITIA MAWAZO, HISIA, IMANI NA MATENDO YAKO. Unapoamini jambo fulani unalifanya litokee na kila kitu kitajipangilia kama unavyoamini. Hata kama unaamini baya utalipata na hata kama unaamini zuri utalipata.
Hata sayansi inasema THOUGHTS ARE ENERGY LIKE WAVES. Chukulia mfano wa redio. Mawazo ni mawimbi ya redio na Universe ni channel. Kama una mawazo mazuri unapelekea mawimbi mazuri kukuzunguka na kuona vitu vizuri kiuhalisia.
NDIO MAANA INASEMEKANA HUWEZI KUBADILI MAISHA YAKO KAMA HUJABADILI MITAZAMO YAKO NA AKILI YAKO. TTUANGALIE MAWAZO TUNAYOWEKA KICHWANI AU VITU TUNAVYOVIAMINI KWANI VINAWEZA KUTUTAWALA NAKUKUA KATIKA DUNIA YA KIFIZIKIA.
Asanteni.