Unadhani itakuwa lini?

Unadhani itakuwa lini?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,091
Reaction score
136,650
...ambapo Magufuli atasafiri kwenda nje ya nchi.

...itakuwa nchi gani?

...ataongea na waandishi wa habari wa kimataifa?
 
Mi naweza kutabiri ataenda nchi za Africa na Asia sana
hasa China
 
kwa mie mtanzania wa kawaida hata asipoenda nje au kufanya hayo makitu poa tu
Ilimradi nipate maji, madawa, umeme, elimu bora na huduma nyingine za kijamii
 
....Magufuli si diplomat....hivyo sitegemei kumwona akisafiri sana nje ya nchi....haswa huko ulaya na marekani wanakotupatia misaada...ila ikibidi awepo huko namwona akiwatumia zaidi ma diplomats atakaowachagua...haswa waziri wa mambo ya nje....Katika kujenga mahusiano na nchi za nje...naona hili Magufuli halitamsumbua sana .....maana tayari JK hii ndio ilikua agenda yake iliyomfanya mtembezi wa dunia...

....katika kukuza viwanda...namwona JPM atashughulika sana na asia...haswa china...katika kuvuta uwekezaji wa wachina TZ...

...labda akiwa makini JPM anaweza kuchukua model ya ethiopia...pale ambapo wao wamevutia wachina kuwajengea special economic zones kule ethiopia....jambo ambalo ni bora sana na halihitaji utembezi wa rais nje....maana wao wawekezaji ndio wanavutika kuja africa kuwekeza..na si viongozi wetu kushinda kwao wakitembeza bakuli....
 
Vasco da Gama ni shidaaa
 
...ambapo Magufuli atasafiri kwenda nje ya nchi.

...itakuwa nchi gani?

...ataongea na waandishi wa habari wa kimataifa?
Kumbuka kazi ya Makufuri ni kuiosha nchi, kusafiri safiri NJE ndio kumetufikisha hapa.
 
Mimi kwa mtazamo wangu kama hizo safari zingekuwa zaleta maendeo basi tungeyaona kwa safari alizofanya Rais alomaliza muda wake Kikwete
 
Ataanza Kenya au nchi nyingine ya jumuiya ya EA.

Lini atasafiri hiyo sijui na hainihusu.

Kwanini asiongee na wanahabari? Sasa tutajua nini kuhusu kiongozi wa nchi?
 
Cha msingi ni kutimiza ahadi zake alizowaahidi watanzania ili awe kiongozi bora kuliko wengine waliomtangulia. Safari sio issue sana as long as aliyepita alitembea sana kuimarisha uhusiano wa nchi yetu na mataifa ya nje.
 
Khaa!! Safari za nje za nini mapema hivi bana?? Kwanza tunyooshwe huku ndani ili hata mambo yakija kutoka nje tuwe tumenyooka tayari 😎
 
mmmhhh ngosha hatajaga. Labda berlin ugerman kidogo
 
mmmhhh ngosha hatajaga. Labda berlin ugerman kidogo. Maana ujeruman ni watu wa kazi kama mwana chato
 
Nataka atulie japo mwaka ajenge displine.....
 
Miafikira ndivyo tulivyo..wakati mmoja tunafikiri kwa kutumia kichwa/ubongo wakati mwingine tunatumia tumbo
 
Back
Top Bottom