Unabii huu tayari umetimia!

Unabii huu tayari umetimia!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Yesu alipokuwa akiwaeleza wanafunzi wake dalili za kuja kwake, na za mwisho wa dunia, alitamka maneno haya ya kinabii: “Na kwa sababu ya kuongezeka kwa maasi, upendo wa wengi utapoa.” (Mathayo 24:12). Huu ni unabii unaoeleza hali ya kijamii na ya kiroho itakavyokuwa duniani kabla ya kuja kwa Bwana Yesu Kristo.

Unabii huo tayari umetimia. Hebu tuuchambue kwa kifupi unabii huo.
1. Maasi kuongezeka – Kuna ushahidi gani kuwa maasi au maovu yameongezeka nyakati hizi? Leo tunaishi katika kizazi ambacho uasi au maovu dhidi ya Mungu na maadili mema, umepindukia. Labda utasema, "Ah, hata zamani watu walitenda maovu." Lakini ukweli ni kwamba maasi yameongezeka kwa sababu nyakati hizi kuna nchi zimehalalisha maovu na kuyapa kinga kisheria. Zamani, uzinzi, ushoga, na mimba za utotoni vilikuwa aibu na vilipigwa vita. Leo, uovu huo unatungiwa sheria za kuulinda?! Duh!

Haya, angalia tena jinsi maovu yanavyosambaa kwa kasi kwa njia ya mitandao. Sasa hivi, mtoto wa miaka 3 anaweza kupata maudhui machafu kwa simu bila hata mzazi kujua. Hali hii haikuwepo zamani.

Leo hii watu wanajivunia dhambi badala ya kutubu. Siku hizi watu wanajitangaza mitandaoni kwa kufanya mambo yasiyo ya haki—wanajiona mashujaa wa uovu.

Ukatili na uhalifu umeongezeka kwa kiwango cha kutisha. Miaka ya zamani, milango ya nyumba iliachwa wazi bila hofu. Leo, hata watu wakiwa ndani, wanafunga milango kwa makufuli matatu! Ripoti za uhalifu wa kikatili, mauaji ya kifamilia, ubakaji wa watoto wachanga, na hata ibada za kishetani—vimejaa kila kona ya dunia.

2. Upendo wa wengi kupoa
Siku hizi, upendo wa kweli wa kibinadamu na ule wa kumcha Mungu umepoa mno: Sio jambo la ajabu leo hii kuona wanandoa wanapeana talaka wiki moja baada ya kuoana kwa sherehe kubwa!

Zamani, majirani walikuwa kama familia. Leo, mtu anaweza kuugua hadi kufa chumbani kwake bila jirani kujua.

Watu hawasaidiani tena kwa moyo wa upendo.
"Kila mtu apambane na hali yake" ni usemi ulioanza hivi majuzi tu. Zamani, mtu alipokuwa na njaa, kijiji kilimhudumia. Leo, mtu akilia barabarani, wengi hupita bila kujali. Na wengine wanampiga picha za video badala ya kumsaidia. Gari likipata ajali, watu wanadiriki kusechi mifuko ya majeruhi ili wapate pesa badala ya kuokoa maisha ya majeruhi!

Tazama manabii wa uongo wanavyohubiri ili kupata pesa za kujaza matumbo yaotu. Mtu ana shida, anaumwa, lakini bado anakamuliwa hata kile kidogo alicho nacho kwa kuambiwa anunue eti chumvi na mafuta ya upako. Ni nini hiyo kama sio upendo kupoa?
 
Ndugu zangu, huu ni wakati wa kuamka. Kupoa kwa upendo na kuongezeka kwa maasi ni ishara ya nyakati za mwisho. Tusidanganywe na uongo wa shetani kwamba hali hii ya sasa ni ya kawaida tu. Unabii wa Yesu umetimia kwa kiwango kikubwa, na kila aliye na macho ya kiroho anaona wazi wazi. Ni dhahiri kama Maandiko yanenavyo, Yesu yuaja upesi.

Mungu akusaidie ndugu, siku Yesu atakapokuja akukute katika utakatifu ili akunyakue pamoja na watakatifu wengine na kukupeleka mbinguni. Vinginevyo itakuwa kilio na kusaga meno ukiachwa duniani. Duniani kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijakuwepo tangu ulimwengu ulipoumbwa.
 
Ndugu zangu, huu ni wakati wa kuamka. Kupoa kwa upendo na kuongezeka kwa maasi ni ishara ya nyakati za mwisho. Tusidanganywe na uongo wa shetani kwamba hali hii ya sasa ni ya kawaida tu. Unabii wa Yesu umetimia kwa kiwango kikubwa, na kila aliye na macho ya kiroho anaona wazi wazi. Ni dhahiri kama Maandiko yanenavyo, Yesu yuaja upesi.

Mungu akusaidie ndugu, siku Yesu atakapokuja akukute katika utakatifu ili akunyakue pamoja na watakatifu wengine na kukupeleka mbinguni. Vinginevyo itakuwa kilio na kusaga meno ukiachwa duniani. Duniani kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijakuwepo tangu ulimwengu ulipoumbwa.
Ndugu, umeyasikia hayo. Je, uko tayari kumpokea Yesu na kuanza maisha mapya? Au utaendelea kusema "Bado muda upo," mpaka mlango wa neema ufungwe?

Biblia inasema wazi:
Waebrania 9:27
"Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu..."

Hakuna nafasi ya pili baada ya kufa. Hakuna rehema kaburini. Wokovu ni sasa – kabla hujachelewa.

Yesu anakuita leo. Anasema:
"Tazama, nasimama mlangoni nabisha; mtu akiisikia sauti yangu na kuufungua mlango, nitaingia kwake..."(Ufunuo 3:20)

Usikawie. Tubu dhambi zako. Mwamini Yesu Kristo. Mkaribishe katika moyo wako kwa kuomba sala hii ya toba kwa unyenyekevu.

Omba kwa kufuatisha sala hii:
“Ee Mungu Baba, nimetambua mimi ni mwenye dhambi. Na kwamba hizi ni nyakati za mwisho. Leo nakuja mbele zako nikiomba msamaha wako. Natubu dhambi zangu zote na kuziacha. Nakiri kuwa Yesu Kristo ni Bwana, na Yeye ndiye Mwokozi wa ulimwengu. Yesu karibu moyoni mwangu utawale maisha yangu kuanzia leo. Naomba unipe nguvu ya kushinda dhambi na kuishi maisha matakatifu. Namkataa shetani na kazi zake zote. Asante Yesu kwa kuniokoa. Katika Jina la Yesu Kristo, ninaomba na kushukuru. Amen.”

Kama umeomba sala hiyo kwa moyo wako wa dhati, tayari umeokoka. Yesu akija, utakuwa miongoni mwao watakaonyakuliwa. Anza kusoma Biblia kila siku na kumuomba Mungu akusaidie kuendelea vizuri kiroho. Tafuta pia Kanisa lolote linalohubiri wokovu na kufundisha utakatifu, watakupa msaada zaidi wa jinsi ya kukua kiroho. Ubarikiwe!
 
Kukataa wokovu ni kuchagua hukumu.
Yohana 3:18
"Amwaminiye Yesu hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa."
 
Mwombee kwanza lissu atoke salama salmin halafu tuendelee
Rafiki, maisha ya mwanadamu ni mafupi sana, na wokovu ni jambo la haraka, sio la kusubiri.
Ya kesho huyajui. Sikutishi, lakini jiulize: ukiondoka duniani usiku huu, ukaishia motoni, utamlaumu nani?

Utapataje kupona, ukipuuza wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliomsikia(Waebrania 2:3)
 
Ndugu, umeyasikia hayo. Je, uko tayari kumpokea Yesu na kuanza maisha mapya? Au utaendelea kusema "Bado muda upo," mpaka mlango wa neema ufungwe?
Ufunuo 3:20
“Tazama, nasimama mlangoni nabisha; mtu akiisikia sauti yangu na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nitakula pamoja naye, naye pamoja nami.”
 
Yesu alipokuwa akiwaeleza wanafunzi wake dalili za kuja kwake, na za mwisho wa dunia, alitamka maneno haya ya kinabii: “Na kwa sababu ya kuongezeka kwa maasi, upendo wa wengi utapoa.” (Mathayo 24:12). Huu ni unabii unaoeleza hali ya kijamii na ya kiroho itakavyokuwa duniani kabla ya kuja kwa Bwana Yesu Kristo.

Unabii huo tayari umetimia. Hebu tuuchambue kwa kifupi unabii huo.
1. Maasi kuongezeka – Kuna ushahidi gani kuwa maasi au maovu yameongezeka nyakati hizi? Leo tunaishi katika kizazi ambacho uasi au maovu dhidi ya Mungu na maadili mema, umepindukia. Labda utasema, "Ah, hata zamani watu walitenda maovu." Lakini ukweli ni kwamba maasi yameongezeka kwa sababu nyakati hizi kuna nchi zimehalalisha maovu na kuyapa kinga kisheria. Zamani, uzinzi, ushoga, na mimba za utotoni vilikuwa aibu na vilipigwa vita. Leo, uovu huo unatungiwa sheria za kuulinda?! Duh!

Haya, angalia tena jinsi maovu yanavyosambaa kwa kasi kwa njia ya mitandao. Sasa hivi, mtoto wa miaka 3 anaweza kupata maudhui machafu kwa simu bila hata mzazi kujua. Hali hii haikuwepo zamani.

Leo hii watu wanajivunia dhambi badala ya kutubu. Siku hizi watu wanajitangaza mitandaoni kwa kufanya mambo yasiyo ya haki—wanajiona mashujaa wa uovu.

Ukatili na uhalifu umeongezeka kwa kiwango cha kutisha. Miaka ya zamani, milango ya nyumba iliachwa wazi bila hofu. Leo, hata watu wakiwa ndani, wanafunga milango kwa makufuli matatu! Ripoti za uhalifu wa kikatili, mauaji ya kifamilia, ubakaji wa watoto wachanga, na hata ibada za kishetani—vimejaa kila kona ya dunia.

2. Upendo wa wengi kupoa
Siku hizi, upendo wa kweli wa kibinadamu na ule wa kumcha Mungu umepoa mno: Sio jambo la ajabu leo hii kuona wanandoa wanapeana talaka wiki moja baada ya kuoana kwa sherehe kubwa!

Zamani, majirani walikuwa kama familia. Leo, mtu anaweza kuugua hadi kufa chumbani kwake bila jirani kujua.

Watu hawasaidiani tena kwa moyo wa upendo.
"Kila mtu apambane na hali yake" ni usemi ulioanza hivi majuzi tu. Zamani, mtu alipokuwa na njaa, kijiji kilimhudumia. Leo, mtu akilia barabarani, wengi hupita bila kujali. Na wengine wanampiga picha za video badala ya kumsaidia. Gari likipata ajali, watu wanadiriki kusechi mifuko ya majeruhi ili wapate pesa badala ya kuokoa maisha ya majeruhi!

Tazama manabii wa uongo wanavyohubiri ili kupata pesa za kujaza matumbo yaotu. Mtu ana shida, anaumwa, lakini bado anakamuliwa hata kile kidogo alicho nacho kwa kuambiwa anunue eti chumvi na mafuta ya upako. Ni nini hiyo kama sio upendo kupoa?
Anayepinga kwamba maasi hayajaongezeka, anyoshe mkono
 
Back
Top Bottom