Unaanzaje kubariki Uzinzi?

Unaanzaje kubariki Uzinzi?

Japo sijasoma comments za wachangiaje wengine zote na huenda ntakachouliza kilishaulizwa ila wacha niulize tu. Ni mwanamke pekee ambaye akifunga ndoa asipokuwa bikra hiyo ndoa inakuwa batili!? Uzinzi wa mwanaume kabla ya ndoa hauifanyi ndoa kuwa batili!?
 
Usidanganywe kabisa. Bikra ni Bikra siku zote.

Awali ni awali hakuna awali mbovu.

Unadhani wazee zamani walikosea kama sisi tunaojifanya wajuaji na matokeo yake ndio haya.

Mwanamke anashindwa kulinda bikra yake ataweza kulinda mapenzi yako
Kweli mkuu.
 
Japo sijasoma comments za wachangiaje wengine zote na huenda ntakachouliza kilishaulizwa ila wacha niulize tu. Ni mwanamke pekee ambaye akifunga ndoa asipokuwa bikra hiyo ndoa inakuwa batili!? Uzinzi wa mwanaume kabla ya ndoa hauifanyi ndoa kuwa batili!?
Mwanamke akijizuia mwanaume atazinije?
 
10 kwa mujibu wa dhehebu langu.
Watu ndio wamesema zipo kumi lakini Mungu hajasema anaamri 10. Soma Biblia Mkuu.

Kuna Amri za mahusiano ambazo zimegawanyika katika makundi mawili;
1. Mahusiano ya mtu na Mungu
2. Mahusiano ya Mtu na mtu/watu.

Kuna Amri za Vyakula.
Kuna Amri za mavazi
Kuna Amri za Mali kama mambo ya Ardhi, urithi n.k.

Hujui mambo mengi mkuu. Sema ufundishwe
 
Watu ndio wamesema zipo kumi lakini Mungu hajasema anaamri 10. Soma Biblia Mkuu.

Kuna Amri za mahusiano ambazo zimegawanyika katika makundi mawili;
1. Mahusiano ya mtu na Mungu
2. Mahusiano ya Mtu na mtu/watu.

Kuna Amri za Vyakula.
Kuna Amri za mavazi
Kuna Amri za Mali kama mambo ya Ardhi, urithi n.k.

Hujui mambo mengi mkuu. Sema ufundishwe
Nimesoma mkuu. Labda unipe hiyo mistari husika.
 
Mwanamke akijizuia mwanaume atazinije?
Kama mwanaume angalitaka thamani na umuhimu wa bikra ya mwanamke wakati wa ndoa basi asingekuwa na haja ya kuhangaika kumshawishi mwanamke ili akubali kisha wakazini maana ingekuwa kichwani kwake kuwa huyo atakayezini ama atakuja kuwa mkewe ambapo atamuo akiwa hana bikra au atakuwa mke wa mwanaume mwingine na hivyo isingempendeza yeye wala mwanaume mwingine. Mimi si msomaji mzuri sana wa maandiko matakatifu na kwa mantiki hiyo naomba kuuliza,kunayo maandiko ambayo waliandika wakisema bikra ya mwanamke ilikuwa kigezo cha ndoa katika zama zao!?
Pamoja na kujadili hapa ambako huenda kukawa kunaonyesha ukinzano wa fikra ni ukweli kwamba uzinzi haupaswi kuendekezwa.
 
Kama mwanaume angalitaka thamani na umuhimu wa bikra ya mwanamke wakati wa ndoa basi asingekuwa na haja ya kuhangaika kumshawishi mwanamke ili akubali kisha wakazini maana ingekuwa kichwani kwake kuwa huyo atakayezini ama atakuja kuwa mkewe ambapo atamuo akiwa hana bikra au atakuwa mke wa mwanaume mwingine na hivyo isingempendeza yeye wala mwanaume mwingine. Mimi si msomaji mzuri sana wa maandiko matakatifu na kwa mantiki hiyo naomba kuuliza,kunayo maandiko ambayo waliandika wakisema bikra ya mwanamke ilikuwa kigezo cha ndoa katika zama zao!?
Pamoja na kujadili hapa ambako huenda kukawa kunaonyesha ukinzano wa fikra ni ukweli kwamba uzinzi haupaswi kuendekezwa.
Muulize Babu yako naona huwezi elewa
 
Back
Top Bottom