Unaanzaje kubariki Uzinzi?

Unaanzaje kubariki Uzinzi?

Ryan The King

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
2,789
Reaction score
2,701
Habari za jumapili.

Bikra ni alama ya usafi na uaminifu kwa mwanamke. Ni dalili ya kujitunza na kujizuia na tamaa za mwili. Hapo zamani mwanamke asiye na bikra alikuwa hawezi kuolewa.

Na Mara nyingi ndio waliokuwa wanafanya biashara ya umalaya kwa kulipwa kiasi kidogo kulingana na thamani yake.

Mwanamke alijivunia bikra yake hata asipokuwa na mvuto wa kuastaajabisha. Bikra ilionekana yathamani zaidi kuliko uzuri wa mwanamke mwenyewe.

Ilikuwa kama huna bikra basi aibu ingeikumba familia yako na wewe binafsi.

Wanawake wenye bikra ndio walipaswa kuvaa shela jeupe pee kama ishara ya usafi wa mavazi, mwili na roho.

Lakini siku hizi utakuta mwanamke bila aibu anavaa shela na ndani bikra ilitoka miaka kumi iliyopita.

Ni kosa la kimaadili kwa Mchungaji kufungisha ndoa ya watu wasiowasafi. Mwanamke asiye na bikra unawezaje kufungisha ndoa yake tena kwa kutumia maneno ya Mungu.

Hapo ndipo watu wanapomchokoza Mungu. Ndipo wachungaji na mapadri wanapoongeza Akaunti zao za makosa kwa kujua au kutokujua.

Mchungaji anapaswa kujua na kutangazia umma kuwa watu hawa ni wasafi na mwanamke huyu ni bikra baada ya kupewa ushahidi.

Vinginevyo kinachoendelea ni uhuni tuu uliohalalishwa.

Kubariki Uzinzi kanisani ni ushetani uliovuka mipaka. Ndio maana kizazi cha sasa hakina nidhamu.

Serikali inapaswa iweke sheria Kali kuhusiana na suala la uasherati kwa vijana wadogo.

Wanafunzi wapimwe mimba na bikra zao. Watoto wakike wafundishwe uoga kwa wanaume. Hii itasaidia lakini bila kuwapa hofu hawa watoto wa kike basi ndipo mambo haya huwa machafuko.

Wachungaji wajitizama upya.

Na wanaume ambao hatujaoa, tuepuke kuoa mwanamke asiye na bikra.

Ni vigumu kumuamini mwanamke asiye na bikra yakuwa ni muaminifu. Atajieleza kwa namna gani uelewe.

Na wanawake wenye bikra, usitoe bikra yako isipokuwa usiku ule wa kufunga ndoa.

Kwa hisani ya kiumeni.

Nawasilisha!
 
Serikali na uzinzi wapi na wapi?

Bikra zinatoka kwa njia moja tu?

Baadaye mtataka serikali isimamie ratiba za kuoga
Hujui serikali ndio inayoweka sheria au hilo hulijui.

Unafikiri serikali ikisema mwanafunzi asiye na bikra hapaswi kufanya mtihani Wa kidato cha nne unafikiri wanafunzi hawatajitunza?

Hujui serikali inauwezo wa kukuamulia uzae watoto wangapi? Pengine hujui.

Serikali unajua maana yake?
Hujui serikali ndiyo inapaswa kuframe mitazamo, mitindo ya maisha, tabia na matendo ya wananchi wake?

Hujui mengi kuhusu serikali?
 
Inavyosemekana mwanamke mwalimu wake ni kipofu...

Uchu na ufisi tunauanza sisi wanaume kwa kumlaghai mwanamke...

Ukishamtoa bikra yake, unamuacha, siku ukiwa tayari kuoa bila aibu unatafuta mwenye bikra, hukumbuki wangapi uliyowatoa bikra zao na ukawaacha solombe...

Sisi wanaume tukiwa na misimamo ya kumlala mwanamke mpaka ukimuoa nadhani wote watakutwa na bikra zao siku ndoa...

Cc: mahondaw
 
Hao ambao hawana bikra waende wapi? Unaweza kuoa bikra ila kwenye ndoa yakawa majanga.

Kwenye kuoa kuna mambo mengi ya kuangalia tofauti na hiyo bikra!!
Usidanganywe kabisa. Bikra ni Bikra siku zote.

Awali ni awali hakuna awali mbovu.

Unadhani wazee zamani walikosea kama sisi tunaojifanya wajuaji na matokeo yake ndio haya.

Mwanamke anashindwa kulinda bikra yake ataweza kulinda mapenzi yako
 
Bikra inatolewa kwa njia moja tuu. Hizo zingine ni simulizi za kubuni.

Labda mtoto afanyiwe upasuaji.
 
Inavyosemekana mwanamke mwalimu wake ni kipofu...

Uchu na ufisi tunauanza sisi wanaume kwa kumlaghai mwanamke...

Ukishamtoa bikra yake, unamuacha, siku ukiwa tayari kuoa bila aibu unatafuta mwenye bikra, hukumbuki wangapi uliyowatoa bikra zao na ukawaacha solombe...

Sisi wanaume tukiwa na misimamo ya kumlala mwanamke mpaka ukimuoa nadhani wote watakutwa na bikra zao siku ndoa...

Cc: mahondaw
Mwanamke lazima akutane na vishawishi vya wanaume ili aonyeshe kujizuia, kuepukana na tamaa na kuonyesha msimamo wake.

Ndio maana unaoa mwanamke alafu anakuja kukusaliti kutokana na yeye hana uwezo wa kujizua na vishawishi vya wanaume.

Usidanganywe. Tumefika hapa tulipo kutokana na mitizamo ya kijinga kama hii.

Serikali lazima iweke sheria za namna hii.
 
Usidanganywe kabisa. Bikra ni Bikra siku zote.

Awali ni awali hakuna awali mbovu.

Unadhani wazee zamani walikosea kama sisi tunaojifanya wajuaji na matokeo yake ndio haya.

Mwanamke anashindwa kulinda bikra yake ataweza kulinda mapenzi yako

Kama ulivyosema awali ni awali, kila zama na kitabu chake. Wazee hao walikua wanaangalia bikra, ila zama hizi bikra ni kitu kidogo sana kwenye kigezo cha ndoa.

Wangapi hawajaoa bikra ila maisha yao ya ndoa yana furaha? Usikariri.
 
Ukitaka bikra labda uende mashariki ya mbali au kati wao walau wana maadili ya kimila yanayowakinga sana na mambo ya zinaa...


Ila barani kwetu Afrika huo utamaduni ulishapigwa kumbo kiasi kwamba hakuna tena mambo ya unyago n.k
 
Umeongea mengi mazuri mkuu. Naomba kukuuliza kiimani, hili neno 'toba' lina maana gani na umuhimu gani?
Toba ipo lakini haiondoi adhabu. Ndio maana mpaka Leo watu wanakufa japokuwa Adamu alitubu.

Mwanamke asiye na bikra aolewe na wazee. Ili ajute vizuri
 
1: umeegemea upande mmoja wa wakristo hapohapo unaitaka serikali isimammie kwa kuweka sheria huoni kama itakua discriminative kwa upande wa pili

2: zama zimebadilika sio kila homa ni malaria

3: unatuhakikishia vipi kama wewe umeoa bikra(kama ni me)/umeolewa ukiwa na bikra(kama ni ke)

4: kama ni me ,unataka kutuambia hujawahi kuonja/kutathimini tunda
 
Kama ulivyosema awali ni awali, kila zama na kitabu chake. Wazee hao walikua wanaangalia bikra, ila zama hizi bikra ni kitu kidogo sana kwenye kigezo cha ndoa.

Wangapi hawajaoa bikra ila maisha yao ya ndoa yana furaha? Usikariri.
Unauhakika kuwa wanafuraha?

Unafikiri kwanini watu wanasema ndoa ngumu?

Acha kubisha Mkuu.

Uzinzi haufai. Na ili kuupinga lazima tuwazuie wanawake na bikra zao
 
Habari za jumapili.

Bikra ni alama ya usafi na uaminifu kwa mwanamke. Ni dalili ya kujitunza na kujizuia na tamaa za mwili. Hapo zamani mwanamke asiye na bikra alikuwa hawezi kuolewa.

Na Mara nyingi ndio waliokuwa wanafanya biashara ya umalaya kwa kulipwa kiasi kidogo kulingana na thamani yake.

Mwanamke alijivunia bikra yake hata asipokuwa na mvuto wa kuastaajabisha. Bikra ilionekana yathamani zaidi kuliko uzuri wa mwanamke mwenyewe.

Ilikuwa kama huna bikra basi aibu ingeikumba familia yako na wewe binafsi.

Wanawake wenye bikra ndio walipaswa kuvaa shela jeupe pee kama ishara ya usafi wa mavazi, mwili na roho.

Lakini siku hizi utakuta mwanamke bila aibu anavaa shela na ndani bikra ilitoka miaka kumi iliyopita.

Ni kosa la kimaadili kwa Mchungaji kufungisha ndoa ya watu wasiowasafi. Mwanamke asiye na bikra unawezaje kufungisha ndoa yake tena kwa kutumia maneno ya Mungu.

Hapo ndipo watu wanapomchokoza Mungu. Ndipo wachungaji na mapadri wanapoongeza Akaunti zao za makosa kwa kujua au kutokujua.

Mchungaji anapaswa kujua na kutangazia umma kuwa watu hawa ni wasafi na mwanamke huyu ni bikra baada ya kupewa ushahidi.

Vinginevyo kinachoendelea ni uhuni tuu uliohalalishwa.

Kubariki Uzinzi kanisani ni ushetani uliovuka mipaka. Ndio maana kizazi cha sasa hakina nidhamu.

Serikali inapaswa iweke sheria Kali kuhusiana na suala la uasherati kwa vijana wadogo.

Wanafunzi wapimwe mimba na bikra zao. Watoto wakike wafundishwe uoga kwa wanaume. Hii itasaidia lakini bila kuwapa hofu hawa watoto wa kike basi ndipo mambo haya huwa machafuko.

Wachungaji wajitizama upya.

Na wanaume ambao hatujaoa, tuepuke kuoa mwanamke asiye na bikra.

Ni vigumu kumuamini mwanamke asiye na bikra yakuwa ni muaminifu. Atajieleza kwa namna gani uelewe.

Na wanawake wenye bikra, usitoe bikra yako isipokuwa usiku ule wa kufunga ndoa.

Kwa hisani ya kiumeni.

Nawasilisha!
Nimeipenda hii.........Na mwenye kusikia na Asikie..................
 
Ukitaka bikra labda uende mashariki ya mbali au kati wao walau wana maadili ya kimila yanayowakinga sana na mambo ya zinaa...


Ila barani kwetu Afrika huo utamaduni ulishapigwa kumbo kiasi kwamba hakuna tena mambo ya unyago n.k
Kweli kabisa. Na hii ni kutokana na Wababa tumepoteza Sifa muhimu
 
KULE TANGA KWA WADIGO WANATENGENEZA BIKRA FEKI, MCHINA NAE ANATENGENEZA DONT BE STUPID THINK TWICE MY FRIEND.
 
Back
Top Bottom