Uchaguzi 2020 Umuhimu wa mdahalo kwa wagombea wetu wa urais, Wananchi tunataka kujua mbivu na mbichi

niggarz upbaganika

Senior Member
Apr 22, 2016
109
90
Baada ya kuwasikiliza wagombea wetu wa uraisi napendekeza/tunapendekeza tume ya uchaguzi iandae mdahalo kwa wagombea wetu wa uraisi(wote) na tunaomba patafutwe ukumbi ambao utakuwa neutral ground. Napendekeza Kila mgombea anadi Sera zake kwa maeneo yafuatayo:

1. Muungano
2. Muundo wa utawala/uongozi
3. Maliasili na nishati
4. Elimu
5 .Kilimo
6. Ulinzi na usalama
7. Biashara
8. Miundombinu
9. Sheria na Katina
10. Mahusiano na Katina

Tunapendekeza mdahalo huu uwepo mwezi mmoja kabla ya uchaguzi. Muda mzuri ni kuanzia saa moja mpaka saa nne usiku.

Tunaomba vyombo vyote vya habari nchi mzima viombwe kurusha live mdahalo huu. Baada ya mdahalo kesho yake wagombea waendelee na ratiba ya kuzunguka nchi mzima kutafuta kura zao,wabunge na madiwani wao.
 
Hahahahhaha mtamuua mwenzenu jaman. Hamuoni mpaka hapa kashatema ndoano?
IMG_20200922_131314.jpg


Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
Ni vizuri mdahalo lakini jiwe kamwe hatokubali kuumbuka mchana kweupe kwenye mdahalo huo.
 
Mdahalo siyo jukumu la tume ya uchaguzi- wewe andaa tu kazi yako kubwa itakuwa kuwashawishi wagombea kuja kushiriki huo mdahalo wako ambao utauandaa
 
Mdahalo siyo jukumu la tume ya uchaguzi- wewe andaa tu kazi yako kubwa itakuwa kuwashawishi wagombea kuja kushiriki huo mdahalo wako ambao utauandaa
Kwa vile inaandaa ratiba ya mikutano ndio maana tunapendekeza kwenye hiyo ratiba ipatikane siku moja ambayo tume ya uchaguzi ishirikiane na taasisi yoyote makini nchini ili kufanikisha mdahalo huo.
 
Dr (PhD) JPM hana mpinzani kwenye kujenga hoja...atajiongezea points nyingi. Kichwa cha Mh Rais JPM imehifadhi kumbukumbu nyingi,uwezo wa kufikiri haraka,mafanikio aliyopata kipindi chake cha kwanza,,,aliyopanga 5 kijacho.... CCM hawawezi kukimbia mdahalo...wengine sijui
 
Makatibu wakuu wa vyama wanaweza kushindanisha/kunadi ilani zao,,kama wagombea watakuwa na ratiba ngumu
 
Kwa vile inaandaa ratiba ya mikutano ndio maana tunapendekeza kwenye hiyo ratiba ipatikane siku moja ambayo tume ya uchaguzi ishirikiane na taasisi yoyote makini nchini ili kufanikisha mdahalo huo.
US Presidential Debates are not constitutionally mandated but have become an integral part of presidential elections. The first Presidential Debate was held in 1960, between Democratic Presidential nominee John F. Kennedy and Republican Nominee and Vice-president Richard M. Nixon. However, there are several others debates which are considered to have set the precedent to this debate.
soma:Explainer: The US Presidential Debates – History & Format
 
US Presidential Debates are not constitutionally mandated but have become an integral part of presidential elections. The first Presidential Debate was held in 1960, between Democratic Presidential nominee John F. Kennedy and Republican Nominee and Vice-president Richard M. Nixon. However, there are several others debates which are considered to have set the precedent to this debate.
soma:Explainer: The US Presidential Debates – History & Format
Now, please educate me. Who should organize a debate for our presidential candidates??!
 
Back
Top Bottom