Umuhimu wa "Lock down" na faida zake!!

Umuhimu wa "Lock down" na faida zake!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,169
Reaction score
48,451
Kwanza nianze na tafsiri ya neno "Lock down" ambalo limekuwa ni shina la mijadala hapa JF na Tanzania kwa ujumla hasa kwenye medani ya siasa.

"Lock down" ni amri maalum kwa wakati maalum inayotolewa na wenye mamlaka kwa eneo husika kuzuia watu kufanya jambo fulani kwa kuwatenga ama kuwazuia kabisa watu hao kushirikiana kwa lengo la kufanya tathimini ya ukubwa wa tatizo,kuzuia kuenea kwa tatizo, kukusanya rasirimali za kupambana na tatizo, na kupata muda wa kufanya tafakuri jinsi ya kuendenda kwa ajili ya siku zijazo baada ya tatizo kupita.

Kwa ivo "lock down" si tendo la kiwendawazimu bali ni mfumo maalum wa kitaalamu wa kupambana na majanga mbali mbali kwa njia za kisayansi. "Lock down" kwa kuwa ni jambo la kisayansi haifanywi kwa kukurupuka.

Tangu kuingia kwa Janga la Korona hapa Tanzania, kama jamii tumegawanyika kwenye makundi mawili. Kuna kundi la wale waliotaka itangazwe "Lock down" kuinusuru nchi na kuenea kwa COVID-19 na kuna kundi linalopinga kuanzishwa kwa "lock down". Makundi yote mawili yana hoja zao!!

Kundi linalopinga kuwepo kwa "Lock down" linadhani kwamba "lock down" maana yake ni kufunga ama kuzuia kufanyika kwa kila kitu kwenye nchi yetu kwa kukurupuka. Hoja yao kubwa ni kwamba Uchumi wa nchi yetu utaporomoka kwa kasi ya ajabu sana.

Lakini hata kwenye zile nchi za Ulaya na Marekani ambako "Lock down" imefanyika, siyo kwamba kila kitu kilizuiliwa kwa muda wote kwa watu wote, mambo muhimu yaliendelea kwa mpangilio na utaratibu maalum uliosimamiwa na serikali.

Ni kweli kwamba kazi za Uzalishaji zilisimamishwa kwa kiwango kikubwa, lakini kazi nyingi za kiofisi zilifanyika tokea nyumbani. Kwa ivo hata hapa Tanzania hakuna mtu anayesema kwamba watu waache kufanya kazi, bali tunasema kazi zile muhimu tu ndizo zifanyike tena kwa utaratibu maalum.

Hapa kwetu ambako miji sehemu yake kubwa sana haijapangwa (hili siyo kosa la COVID-19) watu wanaishi shaghalabaghala sana kiasi kwamba kuitunza ile kanuni ya kukaa mbali mbali (social distancing) inashindikana, ni lazima kuwe na sheria ya "Lock down" ili kulazimisha watu wasio na kazi za muhimu sana kuonekana mitaani.

Wakati tunaambiwa kwamba maisha ya watanzania yameboreka kwa kipindi cha miaka 4 iliyopita, bado tena tunaambiwa watanzania wote wasipotoka kwenda kazini hawawezi kulisha familia zao kwa siku husika. Hivi ni kweli kwamba kila mtanzania anatakiwa atoke kwenda kutafuta ndiyo alishe familia yake? KWA NINI?

"Lock down" itasidia kuzuia kuenea kwa kasi kwa maambukizi ya COVID-19, kutupa muda wa kujipanga, kufanya tathimini ya hasara inayotokea kwenye uchumi wetu kutokana na COVID-19, na kubwa kuliko yote ni kujipanga na kupambana na athari za uchumi wa dunia unaoporomoshwa na janga la ugonjwa huu.
 
Niongezee

1. Hakuna vifaa vya kutosha kwa sasa Dunia hivyo itasaidia kuvuta muda vifaa vipatikane. Oxygen tanks na ventilators hatuna za kutosha

2. Dawa zipo kwenye uchunguzi hivyo tukipinguza maambukizi yakiongezeka kutakuwa tayari kuna dawa na chanjo

3 Ugojwa unaweza kuisha wenyewe baada ya muda hivyo kipindi cha mfungo wale wanaoumwa wataponea nyumbani bila kueneza kwa watu wengine

4 Dunia sasa imefugwa hivyo hata mapato ni madogo huu ndiyo muda mzuri wa kufanya hivi maana hata shughuli za kipato hazipo kwa sasa. Kodi na shughuli za kipato zitapungua tu hata kama hatutaki maana nchi nyingi ambazo tunafanya nazo biashara zimefugwa
 
Natamani kuona suluhu dhidi ya huu ugonjwa ikipatikana mapema iwezekanavyo! Kinyume na hapo, kwa namna tunavyo yaendesha maisha yetu! Ukichanganya na siasa, hakika tutaangamia.
 
Naendelea
IMG_20200501_072642.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo shughuli/kazi muhimu zitakazofanyika kwa utaratibu maalum kukiwa na lockdown ni zipi? Tuanzie hapo.
Kwenye mazingira kama haya ni lazima watu watakuwa na uhitaji wa LAZIMA wa mambo fulani fulani hivi. Kwa mfano chakula na madawa pamoja na huduma fulani za usafi.

Masoko yanaweza kuwa wazi lakini kwa mpangilio maalum. Si lazima makuli kujazana sokoni kama hakuna mzigo wa kushusha na inawezekana kabisa mizigo ikawa inashushwa usiku hapo sokoni baada ya wahusika wote kupimwa halijoto zao.

Serikali kwa kutumia wasimamizi wa masoko kusimamia ufanyaji biashara ndani ya masoko. Kwa mfano kwenye masoko yetu kuna watu wengi sana wako mle wanapiga soga tu, si wanunuzi wala wauzaji.

Kwenye vituo vya mabasi kuna watu wanaitwa "wapiga debe" ambao wapo tu lakini sidhani kama kuna ulazima wa wao kuwepo na kuweka msongamano usiohitajika. Tembea kwenye miji mingi sana ya Tanzania utaona ni kwa kiasi gani tuna lundo la watu wapo mahali ambapo hawahitajiki kuwepo.

Nini kitaharibika kama serikali ikuchukua jukumu la kuweka utaratibu maalum wa jinsi ya kuishi wakati huu wa janga hili? Mbona imefunga vyuo, shule za msingi na sekondari na michezo yote na maisha yanaendelea?

Au unadhani hizo shughuli zilizofungwa hazina watu wanaozitegemea kuendeshea maisha yao?
 
Kama unaihitaji jifungie na familia yako nobody will question
Kuihoji serikali ni haki na wajibu wa kila Mtanzania. Inawezekanaje mtumishi wa serikali kujifungia nyumbani kwake kama serikali haijafunga shughuli anayoifanya?
 
Kuihoji serikali ni haki na wajibu wa kila Mtanzania. Inawezekanaje mtumishi wa serikali kujifungia nyumbani kwake kama serikali haijafunga shughuli anayoifanya?
Mwalimu shule ikifungwa nenda kafanye biashara nyingine mtaani, hakuna vya bure, asiyefanya kazi na asile.
 
Back
Top Bottom