Umoja wa Ulaya(EU) waipatia Oksijeni Ukraine kwa kitita cha Euro billion 50 wakiisubira Marekani

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,634
46,278
Umoja wa Ulaya kwa kauli moja ya wanachama wote 27 wamepitisha kitita cha msaada wa Euro billion 50 kwa ajili ya Ukraine.

Orban wa Hungary aliyekuwa ameweka mkwamo wa pesa hizo kutoka kwa muda mrefu hatimaye amekubali kuondoa kura yake ya veto na kupelekea msaada huo kupitishwa .

Ukraine imekuwa katika ukata mkubwa baada ya Republicans kuchukua uongozi wa bunge la wawakilishi mwaka 2023 na kukata msaada wa serikali ya Marekani ambao ndio ulikuwa mkubwa zaidi. Hata hivyo Biden wa anajaribu kukiepuka kikwazo cha bunge la Marekani kwa kutumia sheria inayompa Rais mamlaka kuamua ni silaha zipi zimeisha muda wake na hivyo zinaweza kugaiwa bure au kuuzwa kwa bei rahisi bila ridhaa ya bunge.

Kwa hali hii vita ya Urusi na Ukraine bado ipo sana ikiendelea kwa muda mrefu sana kuliko ilivotarajiwa.
 
Kwa hali hii vita ya Urusi na Ukraine bado ipo sana ikiendelea kwa muda mrefu sana kuliko ilivotarajiwa.
Shida ya waUikrane wapiganaji wake mpaka itumike nguvu Ndo waende vitani ,athari zake hawezi kupigana Kwa ufanisi.
Screenshot_20230722-154745.png
 
Ukraine inazidi kuangamizwa sababu misaada ya aina yeyote haitaleta mabadiliko chanya yeyote dhidi ya SMO ya Russia
Labda western wawe wanataka kumchosha Russia jambo ambalo silioni tena kwasasa
Taifa la Russia limeisha adopt mazingira ya vita yalioambatana na vikwazo nk...
Acha tuone
 
Wanafurahia vita huku wanapiga bizinesi......ukiona faida ya uuzaji silaha waliyopata Marekani kwa Ukraine, inasikitisha sana
Ukraine ana hela gani ya kununulia silaha Marekani, kumbe watu wengine mko humu kama mazombi tu hata hamuelewi dunia inakoenda ila ni kukalia mambo ya vijiweni tu. Bure kabisa.
 
NATO -wanaongoza kwa ugaidi ,wanapata faida kubwa sana kwenye vita,hawataki amani wao ni vita tu inasikitisha sana!
 
Ukraine inazidi kuangamizwa sababu misaada ya aina yeyote haitaleta mabadiliko chanya yeyote dhidi ya SMO ya Russia
Labda western wawe wanataka kumchosha Russia jambo ambalo silioni tena kwasasa
Taifa la Russia limeisha adopt mazingira ya vita yalioambatana na vikwazo nk...
Acha tuone
2024 hii mwaka wa pili huu , bado hamjaangamiza Ukraine tu?
 
Hayo ni maandalizi ya kumchapa Iran.

Hii mipango na gharama zote ni kwa ajili ya kumchapa Iran tu.

Hapa ni kumchosha Russia ili watu wakafunge hesabu zao kule middle East.
Russia alishaambiwa kuwa muda wa kumchapa Irani umefika na akiambiwa atulie ila yeye alikataa, sasa kwa kuwa wazungu hawataki kujimaliza wao kwa wao ndio maana wameamua kumchosha kabisa Russia
 
Back
Top Bottom