Nchi Kavu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 4,271
- 2,401
karibuni nilikutana na mdogo wangu wa kike kwenye daladala. Alikuwa na rafiki yake wa kike wakitokea chuo (sikitaji). Baada ya muda yule shost alishuka nikabaki na mdogo wangu. Tuliposhuka nikamuuliza vipi kuhusu rafiki yako? Nikutanishe nae. Nimevutiwa nae. Akaniambia tayari ana mchumba wake. Nakasema basi.
Baada ya muda akaniambia kuwa lakini shost yake huyo hana raha katika mahusiano yake. Jamaa anambana sana hadi kumnyima uhuru. Inafika wakati anatamani kuachana nae. Moyoni nikasema YES! Nikamwambia mshawishi waachane. Akasema atalifanyia kazi.
Baada ya siku chache nikampigia mdogo wangu kumuulizia ishu imefikia wapi. Akasema alijaribu kumshawishi lakini binti alikataa kushawishika. Akasema anaogopa akiachana na jamaa, atamuua. Nikashangaa sana moyoni.
Hizi ndizo fikra za wanawake na wanaume? Haya ndo mapenzi? Hapo ni uchumba. Wakioana itakuwaje? Moyoni nikasikitika binti mzuri anakosa amani kiasi hicho. Yani hadi leo wanawake hawajitambui? Anaogopa atauawa...!
Baada ya muda akaniambia kuwa lakini shost yake huyo hana raha katika mahusiano yake. Jamaa anambana sana hadi kumnyima uhuru. Inafika wakati anatamani kuachana nae. Moyoni nikasema YES! Nikamwambia mshawishi waachane. Akasema atalifanyia kazi.
Baada ya siku chache nikampigia mdogo wangu kumuulizia ishu imefikia wapi. Akasema alijaribu kumshawishi lakini binti alikataa kushawishika. Akasema anaogopa akiachana na jamaa, atamuua. Nikashangaa sana moyoni.
Hizi ndizo fikra za wanawake na wanaume? Haya ndo mapenzi? Hapo ni uchumba. Wakioana itakuwaje? Moyoni nikasikitika binti mzuri anakosa amani kiasi hicho. Yani hadi leo wanawake hawajitambui? Anaogopa atauawa...!