Umeshawahi kuachana na mpenzi wako kwa sababu umeona mahusiano yenu "hayatofika mbali" (hamjagombana kabisa)

anaweza akakuhudumia na mchepuko akawa anauhudumia pia,kwani mchepuko unataka sh.ngap!!??

Bora nipate huduma hata nikijua kuna mchepu ntapata pa kujifariji Ila unajihudumia mwenyewe na kumhudumia halafu uje ujue ni msaliti utapata maumivu dabo dabo....
 
Mimi nulikimbia baada ya kukuta madawa dawa,kucha na nywele za sehemu za siri,zimechanganywa na madawa dawa ya kienyeji,nilipomuuliza akasema alienda kwa mganga ili anikamate sawa nisifurukute,nilimwacha nikaenda zangu...
Moyo wangu uliteseka sana kumuacha lakini akili yangu iliniambia kumrudia Tena Ni upumbumbavu mkubwa,SIKURUDI MPAKA LEO SIJAANZISHA MAHUSIANO TENA...
 
Sisi(mimi) hiyo tunaipata hapa hapa bongo sio hadi uende kwa vladimir p.
Yeah it’s the biggest challenge that most of us African Men facing, lucky you if you can understand

Na hata hayuko polite wala kutumia lugha yenye ushawishi as if she earned it,

nilikuwa na jamaa yangu kutoka Benin alikuwa na mwanamke wake from Russia ananisimulia

Anadai Binti wa kirussia alikuwa so independent inafika kipindi anafanya zake job anatafuta nauli lengo Tu akakutane na Mpenzi wake, and she was doing for love na jamaa akawa ananiambia yeye alikuwa anajihisi Fahari hata kumpa zawadi na kumfanyia mambo mengine out of love

Lakini mifumo yetu ya kiafrika baadhi ya wanawake ndiyo inawalemaza na kuwadidimiza shimoni kabisa.
 
Kuna manzee nilimpenda balaaa alafu nilimuamini kweli alikua mzuri hatari alafu Mimi wa kawaida tu ila daah alikua ananipenda nadhani ule ulikua upendo wa kweli aisee basi tulidumu kwenye mapenzi miaka karibia 6 na muda mwingi nilikua nae ingawa hatukuwa tunakaa pamoja ila kila nikimuhitaji au hata nisipomuhitaji alikua anakuja

Kuna kipindi niliyumba vibaya kiuchumi daah alinisave sana yule dada alikua anakuja na misosi home kidume navunga ila ananikazia acha kujifanya kidume wewe basi nakula msosi namla na yeye fresh yani mambo yalikua bambam kwao nilikua napajua Kwa mama yake ila yeye alifikia muda akasema anaenda kupanga nikaona poa ingawa napo nilikua naenda ila sijawahi kulala kwake

Basi bwana siku Kaja na bonge la gauni la kama la harusi vile akataka nimyosheee mana anaenda kusimamia harusi ya rafiki yake kweli baada ya siku tatu akarudi gheto ila amechorwa balaa ila sikujiuliza nikapiga gemu week nzima ndio akasepa

Maisha yakaendlea baada ya miaka miwili kuna siku simu ikaingia eti unamjua S duuuh sauti ya kike ikasema Mimi ni mama yake naomba achana na mwanangu ameshaolea miaka miwili


Duuuh kidume sijui kitu kumbe manzee kaolewa miaka miwili nyuma

Basi nilitafuta ushahidi tu nikahakikisha kweli demu aliolewa na sababu ya kuolewa ni pesa mi sikua nazo ila yule jamaa yake alikua vizuri


Basi nikaona sio issue nika hama getho kimywa kimywa alafu akalamba broke kila sehemu so nikawa nimeachana nae

Sababu ya kufanya hivo kuna siku nilimuuliza alikataa kabisa ila alisema hey nakupenda sana nafanya mambo ya ajaabu sababu yako naomba ukijua chochote usinichukie nafanya sababu nakupenda basi nilimumiza kichwa nikajua pesa nyingi anatoa Kwa jamaa lakini jamaa hapendwi

Kwakweli yule manzee nilimuacha ingawa tulikua tunapendana sana Ila ndio hivo tena saizi ni mwaka sasa nasikia ananitafuta ingawa nimeapa siwezi kuonana nae nikiwa masikini bado
 
Hehehe duh me kuna mwana nlimwacha yaan alikua vzuri tu lkn alikua akisema kitu hatekelezi swala dogo tu LA kunyoa Nywele na ndevu na kubet vlikua shida kuoga ndo kabisaaa...nkaona isiwe shida nkamwacha for good....

Kuna mwamba mwingine yeye haoni shida kutoa hewa ya ukaa (kujamba) na shuzi Lina nuka kwelikweli mwamba mchafu kinoma kuoga ishu mswaki ishu geto hapafai...vuzi LA ela yote ukimwambia ndo kwanzaaa anakuona kama katuni nkaona isiwe tabu nkamwacha for good.....
Hizo ndo type zako.
 
"I still see your shadows in my room
Can't take back the love that I gave you
It's to the point where I love and I hate you
And I cannot change you so I must replace you"
 
(Nilinyala)unatokea Mk sio
Umenikumbusha mbali pia my dear, iliwahi nikuta mkaka anachamba kama muimba taarabu na ana wivu sio mchezo siku moja alipiga bahati mbaya nikawa mbali na simu aliongeaaa, alitukanaaa alichonikera ni kunitukania mama angu nilijibu jibu moja tu nikamwambia hapa hujanioa ukinioa si utanitukania ukoo mzima?? Nilinyala kimya kimya mpaka leo
 
Note:
hakuna mahusiano ambayo yanadumu kama yale ya kusema sina mpango tufike mbali tunajiweka weka tu.. miaka inakatika mara mnafika na huko mbali.

Aloo hii kama umenigusa hivi tulianza tuu kama Friends with Benefits
Daaah Muda kweli huzungumza, tuna Familia sasa.
‍♂️‍♂️‍♂️‍♂️
 
Aloo hii kama umenigusa hivi tulianza tuu kama Friends with Benefits
Daaah Muda kweli huzungumza, tuna Familia sasa.
‍♂‍♂‍♂‍♂
wengi tu sio wewe.
ni ile hali ya kuwa humfatilii na yeye hakufatilii hakuna wivu mnakua kama marafiki, na mapenzi ni urafiki urafiki ukikosekana hakuna mapenzi .
Ndio mana wasiotaka kufika mbali wanaoana, huku kujifanya kwetu tunataka kufika mbali tunakua selective mwisho wa siku tunaishia kujaza nyuzi jf tunazeeka tunakufa
 
Back
Top Bottom