Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Nimezamishwa kinani, kwenye lindi la huzuni,
pakushika sipaoni, mwenzenu ni simanzini,
Nina uchungu moyoni,limenikuta jamani,
Umenipata msiba.
Mwana kukuza nyumbani, na vyuoni masomoni,
Nikamfunza kanuni, za kuishi maishani,
Za kuheshimu jirani, na wakubwa majiani,
Ametoweka.
Kama mvuke wa chai, mwanangu amenihini,
umemtoka uhai, sijui nifanye nini,
Leo mfu siyo hai, amelala kitandani,
Kifo kimemzingira.
Nyumba yote ni vilio, waja hawasikizani,
Alikuwa kimbilio, la kwangu na majirani,
Kweli mola atakalo, hutokea dunia,
Mwanangu nakulilia.
Najipangusa machozi, ni mkiwa wa wakiwa,
Lilikuwa pandikizi, mwenye tabia muruwa,
Leo hii hajiwezi, hakuna analotambuwa
Umenipata msiba!!
pakushika sipaoni, mwenzenu ni simanzini,
Nina uchungu moyoni,limenikuta jamani,
Umenipata msiba.
Mwana kukuza nyumbani, na vyuoni masomoni,
Nikamfunza kanuni, za kuishi maishani,
Za kuheshimu jirani, na wakubwa majiani,
Ametoweka.
Kama mvuke wa chai, mwanangu amenihini,
umemtoka uhai, sijui nifanye nini,
Leo mfu siyo hai, amelala kitandani,
Kifo kimemzingira.
Nyumba yote ni vilio, waja hawasikizani,
Alikuwa kimbilio, la kwangu na majirani,
Kweli mola atakalo, hutokea dunia,
Mwanangu nakulilia.
Najipangusa machozi, ni mkiwa wa wakiwa,
Lilikuwa pandikizi, mwenye tabia muruwa,
Leo hii hajiwezi, hakuna analotambuwa
Umenipata msiba!!