Umeishia wapi mchakato wa vitambulisho vya taifa?

Umeishia wapi mchakato wa vitambulisho vya taifa?

Mulangila Mukuru

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2010
Posts
1,945
Reaction score
729
Wadau hivi huu mchakato wa viatmbulisho vya taifa ambao ulizinduliwa kwa mbwembwe na tukashudia viongozi waandamizi wa serkali wakigawiana umeishia wapi? Mara ya mwisho ulikuwa Dar na Zanzibar baada ya hapo ikawa kimya kulikoni?
Tusaidieni kufahamu kwa mnaojua kinachoendelea.
 
Haah!! kipindi kagasheki akiwa naibu waziri mambo ya ndani, mbele ya JK akisisifia eti ''mheshimiwa rais naakuahidi kutekeleza ilani ya CCM kwamba kabla ya mwisho wa mwaka 2012 kila mtanzania atakuwa na kitambulisho cha taifa..., hadi sasa yaleyale ya serikali dhaifu..........!
 
Wadau hivi huu mchakato wa viatmbulisho vya taifa ambao ulizinduliwa kwa mbwembwe na tukashudia viongozi waandamizi wa serkali wakigawiana umeishia wapi? Mara ya mwisho ulikuwa Dar na Zanzibar baada ya hapo ikawa kimya kulikoni?
Tusaidieni kufahamu kwa mnaojua kinachoendelea.
Soma magazeti ya Habari Leo ukurasa wa pili na Daily News ukurasa wa nne wanagawa Vitambulisho huko.
 
Deal lishaisha hilo... mchezo ulikuwa uchezwe na Masha sasa mlivyomuondoa kwa kumnyima kura kila kitu kikawa vyalu vyalu tukaona bora tu tuchomoe halina manufaa kwa Chama...
 
Kwa walio makazini kuna baadhi ya ofisi wameshapewa vitambulisho. Binafsi nikitazama ni zoezi ni gumu sana. Na inaonekana NIDA hawakujiandaa hasa suala la vitendea kazi na watendaji kazi.
 
hicho kitambulisho chenye jina na jinsia kama vile jinsia zetu hazionekani
Mbona kina taarifa zote za mwombaji kwenye chip ya kitambulisho ambayo ni contact less kama NIDA walivyoonyesha wabunge bungeni wakati bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ikiwasilisha bajeti yake!
 
Zoezi linaendelea hasa kwa wilaya za dar, sina hakina na mikoani. ila kwa dar wengi wamekwishavipata.

nafikiri wana vifaa vichache na pia wana wafanyakazi wachache ndiyo maana wanafanya taratibu.
 
Mbona kina taarifa zote za mwombaji kwenye chip ya kitambulisho ambayo ni contact less kama NIDA walivyoonyesha wabunge bungeni wakati bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ikiwasilisha bajeti yake!

ndo itakuwa sababu nyingine ya usumbufu mana kila sehemu itabidi iwe na machine ya kusoma hyo data
 
Mkuu mbona zoezi la ugawaji linaendelea, kama uliandikishw na bado hujapata kuwa mvumilivu tu zamu yako itafika. Kwa sasa wameanza na watumishi wa umma hasa wa DAR ES SALAAM.
 
Viongozi wa NIDA mpaka sasa wanamiliki fungu kubwa ktk account zao, subiri waishie program itazuka upya ili watunishe tena
 
hicho kitambulisho chenye jina na jinsia kama vile jinsia zetu hazionekani
Sio lazima kila taarifa iwe visible kwako,ukitaka kila kitu kisomeke hapo juu, itakuwa kijarida badala ya ID. taarifa nyingine ulizojiandikisha wewe mwenyewe kwenyee fomu zipo kwenye Chip. Wakitaka kuisoma wenyewe ni suala la kuingiza kwenye machine tu.
 
Sio lazima kila taarifa iwe visible kwako,ukitaka kila kitu kisomeke hapo juu, itakuwa kijarida badala ya ID. taarifa nyingine ulizojiandikisha wewe mwenyewe kwenyee fomu zipo kwenye Chip. Wakitaka kuisoma wenyewe ni suala la kuingiza kwenye machine tu.

naelewa lakini sio kihvyo hata tarehe ya kuzaliwa ndo wasiweke wamekurupuka kusema ukweli
 
naelewa lakini sio kihvyo hata tarehe ya kuzaliwa ndo wasiweke wamekurupuka kusema ukweli
Ndiyo maana nikakwambia sio kila taarifa lazima wewe uione kwa urahisi. Taarifa nyingine zimekuwa coded, labda kukusaidia tu kama una kitambulisho hicho sasa hivi geuza upande wa nyuma.

Utaona maandishi: THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA CITIZEN IDENTINTY CARD, chini ya hapo kuna tarakimu 20. Tarakimu 8 za kwanza zinaonesha mwaka wako wa kuzaliwa.

Kuhusu kutokuwa na jinsi, sio kweli usipotoshe umma kwa kuwa mara baada ya "jina la mwisho" pale chini, jinsi ya mmiliki wa ID ipo. Baada ya hapo inafuatia tarehe ya mwisho wa matumizi yake.

Naomba kutoa taarifa.
 
naelewa lakini sio kihvyo hata tarehe ya kuzaliwa ndo wasiweke wamekurupuka kusema ukweli
Kalagabao hayo ni mambo ya teknolojia tarehe ya kuzaliwa unakoishi kazi vote vipo lakini huwezi kuving'amua kwa sababu inaonekana si mtaalamu wa mambo hayo. Pia taarifa za mtu ni Siri kwa nini zianikwe juu ya kitambulisho? Waacheni NIDA wachape kazi.
 
kila kinachofanyika tz kina malengo yake sasa katika hili huenda walichohitaji ($$$$$) kupata wameshakipata na vile vilivyotolewa Karimjee ni justification ya mabilioni ya dolali, endelea kusubiri!
 
Mkuu mbona zoezi la ugawaji linaendelea, kama uliandikishw na bado hujapata kuwa mvumilivu tu zamu yako itafika. Kwa sasa wameanza na watumishi wa umma hasa wa DAR ES SALAAM.

Huu nao nimkanganyiko usio wa lazima kwani watumishi wa umma ndo watanzania wa kweli kuliko wengine? kitu ambacho wangefanya ni kuhkikisha wanawamaliza wakazi wote wa dar bila kubagua ni mtumishi ,mfanyabiashara,au asiye na kazi baada ya hapo ndo wahamie mikoa mingine.
 
Back
Top Bottom