Umebaki mwaka mmoja serikali ya CCM imalize muda wake

Umebaki mwaka mmoja serikali ya CCM imalize muda wake

Imefanya mema na ya kijinga...japo amezdi sana kucheka cheka...wadanganyika tuweni makini labda tukiona inafaa tukipe chama chochote pinzani madaraka labda mabadiliko yanaweza kutokea
 
MAZURI ya Kikwete ambayo hayajawahi kufanywa na marais waliomtangulia HAYA HAPA
Katika kipindi cha Kikwete masuala yafuatayo lazima tumpe Credit kwani baadhi yamefanywa na JK wa mwanzo tu na hayakufanywa na Mwinyi wala Mkapa.


1. Ujenzi wa Sekondari za Kata ni maamuzi sahihi ingawa yana changamoto zake zinazoweza kutatuliwa na watakaomfuatia, lakini hapa JK ametumia madaraka yake vizuri


2. Ameendelea na uendelezaji wa Miradi ya Barabara, suala lililoanza kujitokea wakati wa awamu ya 3, JK ameendelea nalo suala hilo kwa kasi kubwa na kwa kipindi chote


3. Daraja Kigamboni, Malagarasi na Kilombero ni miongoni mwa mambo yatakayokumbukwa forever


4. Ongezeko la Taasisi za Elimu ya Juu limefanyika vizuri sana katika awamu ya Kikwete, mbali na UDOM lakini taasisi na vyuo vingi vimeimarishwa, kupandishwa hadhi na vyuo vingi binafsi vimeanziswa. Kwa sasa Taifa haliko tena na dhana ya UDII, Mzumbe na SUA. Aidha ari na moyo wa watanzania kulipia huduma za elimu umeongezeka.


5. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ajira ukilinganisha na awamu mbili zilizomtangulia. Mkapa aliendesha Serikali nyembamba, suala ambalo ni zuri lakini lina changamoto zake kwa wale waliokuwepo wameliona hata akapewa sifa ya mzee wa "ukapa"


6. Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara kwa lengo la kutatua kero ya Umeme ni hatua nzuri ambayo haijawahi kufanywa katika awamu ya 2 na ya Tatu (Vyanzo vya Nishati)


7. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Chuma (Kule Liganga?) ambao maandalizi ya ujenzi wake yamekamilika ni hatua nzuri ili kuvutia au kuanzisha uwekezaji wa zana za Chuma pamoja na Viwanda vikubwa.


8. Hatua ya Kujenga Bandari mpya eneo la Bagamoyo yenye hadhi ya 4th Generation ni tukio litakalokumbukwa na vizazi Dahri vijavyo.


9. Hatua ya Utekelezaji wa mradi wa DRT ambao ulikuwepo miaka mingi pia ni miongoni mwa mazuri yaliyotendeka katika awamu ya JK


10. Zoezi la kutambua na kuwarudisha kwao wahamiaji haramu pia ni zoezi zuri ambalo bila shaka halijawahi kufanywa katika uongozi wa awamu nyinginezo kwa kiwango na utashi wa namna hiyo


11. Kitendo cha utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya Taifa ni credit kubwa kwa JK ambao hakuna sababu za wazi kwanini nchi imekaa miaka 50 pasipo na vitambulisho vya uraia kwa wakazi wake na raia wake


12. Ameendelea kuiweka Tanzania kwenye mahusiano mazuri kimataifa hususan SADC, UN na nyanja nyingine za Kitaifa. Ukiacha EAC ambayo sababu za kuzorota kwake ziko wazi, lakini maeneo mengine ame-play well.
picha; maendeleo ya ujenzi wa daraja la kigamboni eneo la kurasini jijini dsm. ujenzi ulikuwa asilimia 47 mwezi july

Nakunukuu"ONGEZEKO KUBWA LA AJIRA"
Hivi unaishi TANZANIA KWELI AU UNAOTA?
 
Ndani ya huu mwaka 1 ulobakia,atasafiri sana ili kumalizia ungwe,safiri baba
 
MAZURI ya Kikwete ambayo hayajawahi kufanywa na marais waliomtangulia HAYA HAPA
Katika kipindi cha Kikwete masuala yafuatayo lazima tumpe Credit kwani baadhi yamefanywa na JK wa mwanzo tu na hayakufanywa na Mwinyi wala Mkapa.


1. Ujenzi wa Sekondari za Kata ni maamuzi sahihi ingawa yana changamoto zake zinazoweza kutatuliwa na watakaomfuatia, lakini hapa JK ametumia madaraka yake vizuri


2. Ameendelea na uendelezaji wa Miradi ya Barabara, suala lililoanza kujitokea wakati wa awamu ya 3, JK ameendelea nalo suala hilo kwa kasi kubwa na kwa kipindi chote


3. Daraja Kigamboni, Malagarasi na Kilombero ni miongoni mwa mambo yatakayokumbukwa forever


4. Ongezeko la Taasisi za Elimu ya Juu limefanyika vizuri sana katika awamu ya Kikwete, mbali na UDOM lakini taasisi na vyuo vingi vimeimarishwa, kupandishwa hadhi na vyuo vingi binafsi vimeanziswa. Kwa sasa Taifa haliko tena na dhana ya UDII, Mzumbe na SUA. Aidha ari na moyo wa watanzania kulipia huduma za elimu umeongezeka.


5. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ajira ukilinganisha na awamu mbili zilizomtangulia. Mkapa aliendesha Serikali nyembamba, suala ambalo ni zuri lakini lina changamoto zake kwa wale waliokuwepo wameliona hata akapewa sifa ya mzee wa "ukapa"


6. Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara kwa lengo la kutatua kero ya Umeme ni hatua nzuri ambayo haijawahi kufanywa katika awamu ya 2 na ya Tatu (Vyanzo vya Nishati)


7. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Chuma (Kule Liganga?) ambao maandalizi ya ujenzi wake yamekamilika ni hatua nzuri ili kuvutia au kuanzisha uwekezaji wa zana za Chuma pamoja na Viwanda vikubwa.


8. Hatua ya Kujenga Bandari mpya eneo la Bagamoyo yenye hadhi ya 4th Generation ni tukio litakalokumbukwa na vizazi Dahri vijavyo.


9. Hatua ya Utekelezaji wa mradi wa DRT ambao ulikuwepo miaka mingi pia ni miongoni mwa mazuri yaliyotendeka katika awamu ya JK


10. Zoezi la kutambua na kuwarudisha kwao wahamiaji haramu pia ni zoezi zuri ambalo bila shaka halijawahi kufanywa katika uongozi wa awamu nyinginezo kwa kiwango na utashi wa namna hiyo


11. Kitendo cha utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya Taifa ni credit kubwa kwa JK ambao hakuna sababu za wazi kwanini nchi imekaa miaka 50 pasipo na vitambulisho vya uraia kwa wakazi wake na raia wake


12. Ameendelea kuiweka Tanzania kwenye mahusiano mazuri kimataifa hususan SADC, UN na nyanja nyingine za Kitaifa. Ukiacha EAC ambayo sababu za kuzorota kwake ziko wazi, lakini maeneo mengine ame-play well.
picha; maendeleo ya ujenzi wa daraja la kigamboni eneo la kurasini jijini dsm. ujenzi ulikuwa asilimia 47 mwezi july

1. Katika uongozi wake viongozi wa serikali na chama CCM wauwawa mikononi mwa wananchi. Mfano aliyekuwa R.P.C mkoa wa mwanza Liberatus Ballo na aliyekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza.

2. Katika uongozi wake tunashuhududia akiziidi kuweka rekodi za ajabu mfano kuwa kiongozi pekee duniani kusafiri mara nyingi zaidi duniani zaidi ya mara 370 yaani ni sawa na kusema katika miaka 9 tangu aingie madarakani ametumia miaka miwili kuwa nje ya Nchi sababu safari moja inatumia siku tatu mpaka tano, ungekuwa mpira angekuwa Messi mzee wa rekodi.

3. Kipindi chake pia tumeshuhudia na tutaendelea kushuhudia mawaziri wengi wakijiuzuru ndani ya bunge kuliko awamu yoyote ile. Mfano ni Karamagi, Msabaha, Kagasheki, Lowasa, ................... n.k

4. Katika utawala wake pia kwa mara ya kwanza tumeshuhudia waziri mkuu akishtakiwa mahakamani huku akiwa madarakani kwa kutoa kauli za kichochezi katika historia ya taifa hili.

5. Katika uongozi wake tumeshuhudia serikali ikikubwa na kashifa nzito nzito za ufisadi na rushwa, mfano IPTL, Richmond, Scrow, na baadhi ya kashifa kupelekea waziri mkuu kujiudhuru, kujiudhuru huku kwa waziri mkuu ni mara ya kwanza katika historia ya taifa hili tena kwa kashifa nzito.

6. Akiwa kama kiongozi pia tumeshuhudia akitoa kauli za ajabu ajabu kama
> "Mnapata mimba kwa viele ele vyenu"
> "Foleni Dar ni ishara ya maisha bora"
> "Mwenge umepunguza maambukizo ya ukimwi"
> "Ukijua kula, ukubali Kuliwa"
> "Kama hutaki kazi acha"
> "Tundu Lissu ni mnafiki, mzindaki, mnafiki, ...........mzindaki, n.k"

7. Ni utawala pekee uliominya demokrasia ya habari na siasa kwa hari ya juu, mfano katika utawala huu tunashuhudia viongozi wengi wa vyama vya upinzani wakifunguliwa mashitaka na kukamatwa ovyo kuliko hata kipindi cha mkoloni mweupe enzi za kudai uhuru wa kwanza. Wengine wamefunguliwa mpaka kesi za ugaidi, hatari sana

8. Migogoro ya kidini imekuwa mikubwa kufikia hatua mabomu kulipuka makanisani, makanisa kuchomwa moto, mapadri kupigwa risasi, mapadri na mashehe kumwagiwa tindikali, n.k
 
11073249_10153247802899216_737545996092304506_n.jpg
 
Ila watanzania wasirudie kosa tena kuchagua ccm..itakula kwao mno
 
Tz ni shida yaani uchaguzi niboctober lkn mpk leo kimyaaaaaaaaa marekani ni mwakani lkn thic year mgombea tayari na bado
 
Ameonyesha "ubinadamu" kwa kuwasamehe wauza madawa ya kulevya ili waendelee na biashara licha ya kusema anawajua maana ndio wafadhili wa chama "chetu"
Kwa huruma kabisa na utu uliotukuka aliwaambia wale walioiba fedha za EPA warudishe tuu maana ni ndugu zetu na Tanzania ni moja.
Majangili kawaonya kuwa hata kama wanaua Tembo basi sio vizuri wakawaua sana maana lazima wabaki wengine ili wazaliane na biashara isife kwa kuwa anawafahamu wahusika.
Kaamua hayo ya IPTL ayaache tuu maana hao waliokwapua ni watendaji wake wakuu ya nini kuumbuana kwa Bil 400 wakati katika tembeatembea yake akiomba wafadhili wamejitolea matrilioni?
Mazuri ni mengi sana kwa kweli.
katika hii Lizaboni hawezi kukujibu.
 
Back
Top Bottom