Umebaki mwaka mmoja serikali ya CCM imalize muda wake

Umebaki mwaka mmoja serikali ya CCM imalize muda wake

Roga Roga

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2013
Posts
655
Reaction score
500
Kwa wale wapenda mabadiliko hapa Tanzania sasa ni wakati wa kuanza kufurahi na kusherekea kwani muda uliobaki kwa serikali hii ya kijeshi imalize muda wake wa miaka 10 ambayo iliingia madarakani 2005 na ita-expiry mwaka 2015.
Ninaiita serikali ya mpito au ya kijeshi kutokana na mambo kadhaa yaliyotokea katika kipindi hichi na kuzimwa kwa nguvu kubwa ya jeshi la polisi au la wananchi na kuacha sintofahamu kubwa katika jamii, mfano wa matukio hayo ni

1. Sakata la gesi mtwara ambalo lilishuhudia nguvu kubwa ya kijeshi ikitumika na kugharimu maisha ya watu kadhaa, huku wengine wakiachwa na ulemavu wa kudumu, yatima na kukosa nyumba za kuishi.

2. Mgomo wa madaktari, ambao ilishuhudia wagonjwa wakipoteza maisha sehemu mbalimbali nchini na mgomo huo ulizimwa kwa Dkt Ulimboka kutekwa na kufanyiwa ukatili wa kutisha na watu wa usalama wa Taifa (kwa mjibu wa M.w.a.n.a.h.a.l.i.si)

3. Kuingiliwa uhuru wa vyombo vya habari pale tu vilipoandika ubaya au kuikosoa serikali iliyomadarakani. Mfano ni kufungiwa kwa magazeti kama Mwananchi na Mtanzania.

4. Kuuwawa na kuwadhuru waandishi wa habari, mfano Said Kubenea kumwagiwa tindi kali na Daudi Mwangosi kuuawa huku RPC husika akipandishwa cheo.

5. Jeshi la polisi kugeuka na kufanya kazi za siasa kama moja ya vitengo muhimu pale Lumumba. Mfano ni unyanyasaji wa viongozi wa Upinzani kama Halima Mdee, Wilfred Lwakatale kufunguliwa kesi ya Ugaidi

6. Kumwagiwa tindikali kwa viongozi wa dini sehemu mbalimbali huku wahusika wakiwa hawajatiwa mbaloni mpaka leo

7. Kuuwawa watu mbalimbali katika mikutano ya siasa mfano viwanja vya Soweto, muuza magazeti Morogoro na maandamano ya chadema 2011

8. Kuuwawa, kuumizwa, kubakwa, kupewa vilema vya kudumu raia mbalimbali katika kile kilichoitwa oparasheni tokomeza ujangili 2013

9. Kuvurugwa kwa mchakato wa katiba huku nguvu kubwa ikitumika katika hafra ya Sita kumkabidhi Rais Kikwete katiba iliyopendekezwa.

10. Vifo mbalimbali katika chaguzi ndogo na uchaguzi mkuu wa 2010 huku wahusika wakifumbia macho tatizo hilo mfano Arumeru Mashariki na Igunga

11. Baraza la mawaziri kuvunjika kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa hili huku historia ikiandikwa zaidi kwa idadi kubwa ya mawaziri kujiuzuru katika utawala wa awamu hii.

12. Elimu kuporomoka kwa kiasi kikubwa sana.



Ningeeleza mengi lakini nawaachia mengine mjazie
 
MAZURI ya Kikwete ambayo hayajawahi kufanywa na marais waliomtangulia HAYA HAPA
Katika kipindi cha Kikwete masuala yafuatayo lazima tumpe Credit kwani baadhi yamefanywa na JK wa mwanzo tu na hayakufanywa na Mwinyi wala Mkapa.


1. Ujenzi wa Sekondari za Kata ni maamuzi sahihi ingawa yana changamoto zake zinazoweza kutatuliwa na watakaomfuatia, lakini hapa JK ametumia madaraka yake vizuri


2. Ameendelea na uendelezaji wa Miradi ya Barabara, suala lililoanza kujitokea wakati wa awamu ya 3, JK ameendelea nalo suala hilo kwa kasi kubwa na kwa kipindi chote


3. Daraja Kigamboni, Malagarasi na Kilombero ni miongoni mwa mambo yatakayokumbukwa forever


4. Ongezeko la Taasisi za Elimu ya Juu limefanyika vizuri sana katika awamu ya Kikwete, mbali na UDOM lakini taasisi na vyuo vingi vimeimarishwa, kupandishwa hadhi na vyuo vingi binafsi vimeanziswa. Kwa sasa Taifa haliko tena na dhana ya UDII, Mzumbe na SUA. Aidha ari na moyo wa watanzania kulipia huduma za elimu umeongezeka.


5. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ajira ukilinganisha na awamu mbili zilizomtangulia. Mkapa aliendesha Serikali nyembamba, suala ambalo ni zuri lakini lina changamoto zake kwa wale waliokuwepo wameliona hata akapewa sifa ya mzee wa "ukapa"


6. Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara kwa lengo la kutatua kero ya Umeme ni hatua nzuri ambayo haijawahi kufanywa katika awamu ya 2 na ya Tatu (Vyanzo vya Nishati)


7. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Chuma (Kule Liganga?) ambao maandalizi ya ujenzi wake yamekamilika ni hatua nzuri ili kuvutia au kuanzisha uwekezaji wa zana za Chuma pamoja na Viwanda vikubwa.


8. Hatua ya Kujenga Bandari mpya eneo la Bagamoyo yenye hadhi ya 4th Generation ni tukio litakalokumbukwa na vizazi Dahri vijavyo.


9. Hatua ya Utekelezaji wa mradi wa DRT ambao ulikuwepo miaka mingi pia ni miongoni mwa mazuri yaliyotendeka katika awamu ya JK


10. Zoezi la kutambua na kuwarudisha kwao wahamiaji haramu pia ni zoezi zuri ambalo bila shaka halijawahi kufanywa katika uongozi wa awamu nyinginezo kwa kiwango na utashi wa namna hiyo


11. Kitendo cha utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya Taifa ni credit kubwa kwa JK ambao hakuna sababu za wazi kwanini nchi imekaa miaka 50 pasipo na vitambulisho vya uraia kwa wakazi wake na raia wake


12. Ameendelea kuiweka Tanzania kwenye mahusiano mazuri kimataifa hususan SADC, UN na nyanja nyingine za Kitaifa. Ukiacha EAC ambayo sababu za kuzorota kwake ziko wazi, lakini maeneo mengine ame-play well.
picha; maendeleo ya ujenzi wa daraja la kigamboni eneo la kurasini jijini dsm. ujenzi ulikuwa asilimia 47 mwezi july
 
Mbona nao ni muda mrefu? Ningetamani waondoke hata leo!
 
13.Amechangia kuleta utulivu mashariki mwa DRC
14.Ametoa uraia kwa wakimbizi wa Burundi waliostahili
15. Ameanzsha juhudi za kufufua reli ya kati na kuimasha ile ya Tazara
16.Ameridhia mchakato wa kutugwa katiba mpya achilia mbali uhalibifu wa akina 6
17 Msisitizo wa BR

Endelezeni mema na mtoa mada na wale wa type yako ongezeni yenu
 
13.Amechangia kuleta utulivu mashariki mwa DRC
14.Ametoa uraia kwa wakimbizi wa Burundi waliostahili
15. Ameanzsha juhudi za kufufua reli ya kati na kuimasha ile ya Tazara
16.Ameridhia mchakato wa kutugwa katiba mpya achilia mbali uhalibifu wa akina 6
17 Msisitizo wa BR

Endelezeni mema na mtoa mada na wale wa type yako ongezeni yenu
Pamoja sana Mkuu.
 
13.Amechangia kuleta utulivu mashariki mwa DRC
14.Ametoa uraia kwa wakimbizi wa Burundi waliostahili
15. Ameanzsha juhudi za kufufua reli ya kati na kuimasha ile ya Tazara
16.Ameridhia mchakato wa kutugwa katiba mpya achilia mbali uhalibifu wa akina 6
17 Msisitizo wa BR

Endelezeni mema na mtoa mada na wale wa type yako ongezeni yenu

Ameonyesha "ubinadamu" kwa kuwasamehe wauza madawa ya kulevya ili waendelee na biashara licha ya kusema anawajua maana ndio wafadhili wa chama "chetu"
Kwa huruma kabisa na utu uliotukuka aliwaambia wale walioiba fedha za EPA warudishe tuu maana ni ndugu zetu na Tanzania ni moja.
Majangili kawaonya kuwa hata kama wanaua Tembo basi sio vizuri wakawaua sana maana lazima wabaki wengine ili wazaliane na biashara isife kwa kuwa anawafahamu wahusika.
Kaamua hayo ya IPTL ayaache tuu maana hao waliokwapua ni watendaji wake wakuu ya nini kuumbuana kwa Bil 400 wakati katika tembeatembea yake akiomba wafadhili wamejitolea matrilioni?
Mazuri ni mengi sana kwa kweli.
 
MAZURI ya Kikwete ambayo hayajawahi kufanywa na marais waliomtangulia HAYA HAPA
Katika kipindi cha Kikwete masuala yafuatayo lazima tumpe Credit kwani baadhi yamefanywa na JK wa mwanzo tu na hayakufanywa na Mwinyi wala Mkapa.


1. Ujenzi wa Sekondari za Kata ni maamuzi sahihi ingawa yana changamoto zake zinazoweza kutatuliwa na watakaomfuatia, lakini hapa JK ametumia madaraka yake vizuri


2. Ameendelea na uendelezaji wa Miradi ya Barabara, suala lililoanza kujitokea wakati wa awamu ya 3, JK ameendelea nalo suala hilo kwa kasi kubwa na kwa kipindi chote


3. Daraja Kigamboni, Malagarasi na Kilombero ni miongoni mwa mambo yatakayokumbukwa forever


4. Ongezeko la Taasisi za Elimu ya Juu limefanyika vizuri sana katika awamu ya Kikwete, mbali na UDOM lakini taasisi na vyuo vingi vimeimarishwa, kupandishwa hadhi na vyuo vingi binafsi vimeanziswa. Kwa sasa Taifa haliko tena na dhana ya UDII, Mzumbe na SUA. Aidha ari na moyo wa watanzania kulipia huduma za elimu umeongezeka.


5. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ajira ukilinganisha na awamu mbili zilizomtangulia. Mkapa aliendesha Serikali nyembamba, suala ambalo ni zuri lakini lina changamoto zake kwa wale waliokuwepo wameliona hata akapewa sifa ya mzee wa "ukapa"


6. Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara kwa lengo la kutatua kero ya Umeme ni hatua nzuri ambayo haijawahi kufanywa katika awamu ya 2 na ya Tatu (Vyanzo vya Nishati)


7. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Chuma (Kule Liganga?) ambao maandalizi ya ujenzi wake yamekamilika ni hatua nzuri ili kuvutia au kuanzisha uwekezaji wa zana za Chuma pamoja na Viwanda vikubwa.


8. Hatua ya Kujenga Bandari mpya eneo la Bagamoyo yenye hadhi ya 4th Generation ni tukio litakalokumbukwa na vizazi Dahri vijavyo.


9. Hatua ya Utekelezaji wa mradi wa DRT ambao ulikuwepo miaka mingi pia ni miongoni mwa mazuri yaliyotendeka katika awamu ya JK


10. Zoezi la kutambua na kuwarudisha kwao wahamiaji haramu pia ni zoezi zuri ambalo bila shaka halijawahi kufanywa katika uongozi wa awamu nyinginezo kwa kiwango na utashi wa namna hiyo


11. Kitendo cha utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya Taifa ni credit kubwa kwa JK ambao hakuna sababu za wazi kwanini nchi imekaa miaka 50 pasipo na vitambulisho vya uraia kwa wakazi wake na raia wake


12. Ameendelea kuiweka Tanzania kwenye mahusiano mazuri kimataifa hususan SADC, UN na nyanja nyingine za Kitaifa. Ukiacha EAC ambayo sababu za kuzorota kwake ziko wazi, lakini maeneo mengine ame-play well.
picha; maendeleo ya ujenzi wa daraja la kigamboni eneo la kurasini jijini dsm. ujenzi ulikuwa asilimia 47 mwezi july

Asilimia 86.8% ya hizo kazi alifanya na Edward Lowassa, safi sana Jakaya Kikwete, safi sana Edward Lowassa Mungu awabariki
 
Panapo majaliwa Watanzania muda na majira kama haya mwakani 2015 tutatua mzigo. Ewe Mwenyezi Mungu tunaomba hekima na busara zako tusirudie tena kosa kama tulilolifanya.
 
mimi mwenyewe nasubiri kwa hamu kubwa aise.....I cant wait for that moment to come...nmesisitiza na kidhungu kidogo
 
Back
Top Bottom