BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Umasikini Ngara wamtisha Pinda Wednesday, 09 March 2011 20:31 0diggsdigg
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
Phinias Bashaya,Ngara

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amezitaka halmashauri za wilaya nchini, kuharakisha 
mipango ya upimaji wa vijiji na kuwasaidia wananchi, kuendesha kilimo chenye tija 
kama njia ya kuwakomboa dhidi ya umasikini wa kipato.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya Wilaya ya Ngara juzi, Waziri mkuu alielezea kusikitishwa kwake juu ya kukithiri kwa kiwango cha umasikini, huku viongozi wakishindwa 
kuwasidia wananchi kutumia fursa zilizopo, kujiendeleza.
Kwa mujibu wa Pinda, fursa hizo ni pamoja na matumizi bora ya ardhi kwa shughuli za kilimo.

Alisema halmashauri za wilaya nchini, lazima zitoe kipaumbele katika upimaji wa vijiji 
na kwamba kufanya hivyo, mipango ya halmashauri, itakuwa imetafsiriwa kwa vitendo, vitakavyosaidia kubadili maisha ya 
wananchi.

Baada ya kupokea taarifa hiyo kutoka kwa Mkuu wa wilaya hiyo, Salumu Nyakonji, Pinda 
alisema mazingira aliyoyaona kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Kumubuga, katika Kata ya 
Mulusagamba, yalitoa tafsiri halisi ya kiwango cha umasikini kwa wananchi.

"Wanafunzi niliowaona hali zao ni kielelezo cha umasikini katika familia 
wanazotoka, halmashauri zina mawazo mazuri ambayo hayajatafsiriwa kwa vitendo ili 
kubadili maisha ya wananchi, kuna fursa za ardhi, maji na mifugo wakisaidiwa 
wanaweza kujilisha na kuwa na kipato cha kutosha,"alisema Pinda.

Waziri mkuu pia alionyesha kutoridhishwa kwake kuhusu halmashauri za 
wilaya, kujivunia ukusanyaji mkubwa wa mapato huku makusanyo ya mapato hayo yakishindwa kuonekana katika kubadili maisha ya wananchi.

Alisema wastani wa pato la wananchi katika wilaya hiyo yenye kaya 
50,000 uko chini mno ikilinganishwa na fursa zilizopo.

Akiwa wilayani Ngara, Pinda pia alifungua Zahanati ya Kumubuga, Shule ya Sekondari Kibogora na kuhutubia mkutano wa 
hadhara, katika eneo la Mulusagamba.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
Phinias Bashaya,Ngara

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amezitaka halmashauri za wilaya nchini, kuharakisha 
mipango ya upimaji wa vijiji na kuwasaidia wananchi, kuendesha kilimo chenye tija 
kama njia ya kuwakomboa dhidi ya umasikini wa kipato.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya Wilaya ya Ngara juzi, Waziri mkuu alielezea kusikitishwa kwake juu ya kukithiri kwa kiwango cha umasikini, huku viongozi wakishindwa 
kuwasidia wananchi kutumia fursa zilizopo, kujiendeleza.
Kwa mujibu wa Pinda, fursa hizo ni pamoja na matumizi bora ya ardhi kwa shughuli za kilimo.

Alisema halmashauri za wilaya nchini, lazima zitoe kipaumbele katika upimaji wa vijiji 
na kwamba kufanya hivyo, mipango ya halmashauri, itakuwa imetafsiriwa kwa vitendo, vitakavyosaidia kubadili maisha ya 
wananchi.

Baada ya kupokea taarifa hiyo kutoka kwa Mkuu wa wilaya hiyo, Salumu Nyakonji, Pinda 
alisema mazingira aliyoyaona kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Kumubuga, katika Kata ya 
Mulusagamba, yalitoa tafsiri halisi ya kiwango cha umasikini kwa wananchi.

"Wanafunzi niliowaona hali zao ni kielelezo cha umasikini katika familia 
wanazotoka, halmashauri zina mawazo mazuri ambayo hayajatafsiriwa kwa vitendo ili 
kubadili maisha ya wananchi, kuna fursa za ardhi, maji na mifugo wakisaidiwa 
wanaweza kujilisha na kuwa na kipato cha kutosha,"alisema Pinda.

Waziri mkuu pia alionyesha kutoridhishwa kwake kuhusu halmashauri za 
wilaya, kujivunia ukusanyaji mkubwa wa mapato huku makusanyo ya mapato hayo yakishindwa kuonekana katika kubadili maisha ya wananchi.

Alisema wastani wa pato la wananchi katika wilaya hiyo yenye kaya 
50,000 uko chini mno ikilinganishwa na fursa zilizopo.

Akiwa wilayani Ngara, Pinda pia alifungua Zahanati ya Kumubuga, Shule ya Sekondari Kibogora na kuhutubia mkutano wa 
hadhara, katika eneo la Mulusagamba.