Umasikini Ngara wamtisha Pinda

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Umasikini Ngara wamtisha Pinda Wednesday, 09 March 2011 20:31 0diggsdigg

pindakilimokwanza.jpg

Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Phinias Bashaya,Ngara

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amezitaka halmashauri za wilaya nchini, kuharakisha 
mipango ya upimaji wa vijiji na kuwasaidia wananchi, kuendesha kilimo chenye tija 
kama njia ya kuwakomboa dhidi ya umasikini wa kipato.


Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya Wilaya ya Ngara juzi, Waziri mkuu alielezea kusikitishwa kwake juu ya kukithiri kwa kiwango cha umasikini, huku viongozi wakishindwa 
kuwasidia wananchi kutumia fursa zilizopo, kujiendeleza.

Kwa mujibu wa Pinda, fursa hizo ni pamoja na matumizi bora ya ardhi kwa shughuli za kilimo.


Alisema halmashauri za wilaya nchini, lazima zitoe kipaumbele katika upimaji wa vijiji 
na kwamba kufanya hivyo, mipango ya halmashauri, itakuwa imetafsiriwa kwa vitendo, vitakavyosaidia kubadili maisha ya 
wananchi.


Baada ya kupokea taarifa hiyo kutoka kwa Mkuu wa wilaya hiyo, Salumu Nyakonji, Pinda 
alisema mazingira aliyoyaona kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Kumubuga, katika Kata ya 
Mulusagamba, yalitoa tafsiri halisi ya kiwango cha umasikini kwa wananchi.


"Wanafunzi niliowaona hali zao ni kielelezo cha umasikini katika familia 
wanazotoka, halmashauri zina mawazo mazuri ambayo hayajatafsiriwa kwa vitendo ili 
kubadili maisha ya wananchi, kuna fursa za ardhi, maji na mifugo wakisaidiwa 
wanaweza kujilisha na kuwa na kipato cha kutosha,"alisema Pinda.


Waziri mkuu pia alionyesha kutoridhishwa kwake kuhusu halmashauri za 
wilaya, kujivunia ukusanyaji mkubwa wa mapato huku makusanyo ya mapato hayo yakishindwa kuonekana katika kubadili maisha ya wananchi.

Alisema wastani wa pato la wananchi katika wilaya hiyo yenye kaya 
50,000 uko chini mno ikilinganishwa na fursa zilizopo.


Akiwa wilayani Ngara, Pinda pia alifungua Zahanati ya Kumubuga, Shule ya Sekondari Kibogora na kuhutubia mkutano wa 
hadhara, katika eneo la Mulusagamba.
 
Hivi huyu Pinda anaishi Tanzania ipi mpaka aende Ngara ndiyo atishike na umaskini wa kutisha wa Watanzania? Mbona umaskini wa kutisha umewakumba Watanzania walio wengi katika kila kona ya nchi yetu? Analaumu Halmashauri za Wilaya je Serikali imefanya yepi katika kupunguza kero mbali mbali za Wananchi ikiwemo umaskini wa kutisha? Kwa maoni yangu huyu naye ni msanii wa hali ya juu anataka kulaumu Halmashauri za Wilaya wakati Serikali yake inafanya madudu makubwa zaidi lakini hayaoni!!!!!
 
Inakatisha tamaa, Inatia uchungu, Inatia aibu, kiongozi mwingine aishiye masaki anapokataa maandamano ya CDM wanaotoa hoja mbali mbali za kumsaidia mwananchi. Lakini mwisho wa siku, inatupa moyo zaidi wa kuendeleza mapambano dhidi ya viongozi wetu wanaojiona wao ndo wenye haki ya kuendelea kuongoza hata kama fikra zao hazileti wala kusaidia kuleta uhalisia wa maisha ya mtanzania kutokana na rasilimali tulizonazo.

Its time to work up and keep fighting and protect our nation against the New blalk colonial masters, who don't care about their neighbours, about the lives of the people! they care about Ndiyo Mzee and so on.
 
Anashangaa nini wakati CCM ndio imewafikisha watanzania hapo, huyu mung'amba nae amezidisha :blah::blah:
 
Ni katika kuzima moto ule wa CDM nyanda za juu kaskazini, sasa serikali ndio imeamka na kuanza utendaji kwa lugha safi tunaita 'zimamoto'. Pinda alikuwa wapi kutembelea wilaya hii awamu ya kwanza na kujua kama wananchi wake ni maskini. Watafute ufumbuzi wa haraka, ni dhahiri kuwa CDM sasa inaongoza nchi
 
Hivi huyu Pinda anaishi Tanzania ipi mpaka aende Ngara ndiyo atishike na umaskini wa kutisha wa Watanzania? Mbona umaskini wa kutisha umewakumba Watanzania walio wengi katika kila kona ya nchi yetu? Analaumu Halmashauri za Wilaya je Serikali imefanya yepi katika kupunguza kero mbali mbali za Wananchi ikiwemo umaskini wa kutisha? Kwa maoni yangu huyu naye ni msanii wa hali ya juu anataka kulaumu Halmashauri za Wilaya wakati Serikali yake inafanya madudu makubwa zaidi lakini hayaoni!!!!!

Kama yeye pia analia na kusikitika basi hatuna kiongozi! Kwani huko ngara ndo amegundua umasikini wa watanzania? Their inaction in fighting poverty while condoning embezlement just increases umasikini!
 
huyu mzee manafiki sana..sipendi haa kumsikia akiongea mie ..kila kitu anajifanya kushangaa wakati yeye ndo waziri mkuu..watu wengine bana wanataka tutukane humu tupigwe BAN
 
Kwani anayosema yana tofauti gani na yanayosemwa na cdm, au anataka kusababisha uvunjifu wa amani?
 
Huyu si nmtoto wa mkulima, familia yao wanamiliki ekali si zaidi ya 20 na wanazolima si zaidi ya ekali 6 leo anajiita mtoto wa mkulima ? hayumo kwenye orodha ya wakulima, kwao wasukuma wanalima zaidi ya ekali 300 kwa familia moja na ndiyo maana anawachukia wasukuma.Anashangaa nini wakati pale mpanda watu wanaomiliki nyumba za bati ni wageni wa kuja na si wenyeji .Kwao wamepigika kinoma.Hiloooooooooo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Eti anashangaa mapato makubwa lakini hakuna chochote,hivi serikali kuu nayo si ndio vivyo hivyo..mdogo anaiga kwa mkubwa..
 
Umasikini Ngara wamtisha Pinda Wednesday, 09 March 2011 20:31 0diggsdigg

pindakilimokwanza.jpg

Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Phinias Bashaya,Ngara

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amezitaka halmashauri za wilaya nchini, kuharakisha 
mipango ya upimaji wa vijiji na kuwasaidia wananchi, kuendesha kilimo chenye tija 
kama njia ya kuwakomboa dhidi ya umasikini wa kipato.


Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya Wilaya ya Ngara juzi, Waziri mkuu alielezea kusikitishwa kwake juu ya kukithiri kwa kiwango cha umasikini, huku viongozi wakishindwa 
kuwasidia wananchi kutumia fursa zilizopo, kujiendeleza.

Kwa mujibu wa Pinda, fursa hizo ni pamoja na matumizi bora ya ardhi kwa shughuli za kilimo.


Alisema halmashauri za wilaya nchini, lazima zitoe kipaumbele katika upimaji wa vijiji 
na kwamba kufanya hivyo, mipango ya halmashauri, itakuwa imetafsiriwa kwa vitendo, vitakavyosaidia kubadili maisha ya 
wananchi.


Baada ya kupokea taarifa hiyo kutoka kwa Mkuu wa wilaya hiyo, Salumu Nyakonji, Pinda 
alisema mazingira aliyoyaona kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Kumubuga, katika Kata ya 
Mulusagamba, yalitoa tafsiri halisi ya kiwango cha umasikini kwa wananchi.


"Wanafunzi niliowaona hali zao ni kielelezo cha umasikini katika familia 
wanazotoka, halmashauri zina mawazo mazuri ambayo hayajatafsiriwa kwa vitendo ili 
kubadili maisha ya wananchi, kuna fursa za ardhi, maji na mifugo wakisaidiwa 
wanaweza kujilisha na kuwa na kipato cha kutosha,"alisema Pinda.


Waziri mkuu pia alionyesha kutoridhishwa kwake kuhusu halmashauri za 
wilaya, kujivunia ukusanyaji mkubwa wa mapato huku makusanyo ya mapato hayo yakishindwa kuonekana katika kubadili maisha ya wananchi.

Alisema wastani wa pato la wananchi katika wilaya hiyo yenye kaya 
50,000 uko chini mno ikilinganishwa na fursa zilizopo.


Akiwa wilayani Ngara, Pinda pia alifungua Zahanati ya Kumubuga, Shule ya Sekondari Kibogora na kuhutubia mkutano wa 
hadhara, katika eneo la Mulusagamba.
ni bora hata hao wa Ngara wa kule kwake Rukwa hajawaona? eti amesikitishwa na umaskini? statement ya kinafiki inanikumbusha lile shairi la "BUILDING THE NATION"
 
Back
Top Bottom