Uchaguzi 2020 Uliza, Ujibiwe kuhusu Uchaguzi 2020. Karibuni

nyumbamungu

JF-Expert Member
Mar 3, 2017
997
828
Wadau, Viongozi na Wachambuzi wa Sayansi ya Siasa nawapa salamu bila kuwasahau wana JF, katika jukwaa hili tupo mchanganyiko kwa taaluma zetu, ninawaomba wale wenye majibu mahsusi yanayohusu Uchaguzi Mkuu 2020 wawe wanapitia kwenye Uzi huu na kudongosha majibu ili kutuondolea sintofahamu vichwani mwetu.

Hoja: Tume ya Uchaguzi ya Taifa, imetoa angalizo kwa vyama vya siasa visitumie zaidi ya Bilioni 17 katika kampeni.

Swali: (1) Kwani mgombea huwa anapewa pesa na chama kilicho mdhamini, na baada ya matokeo mgombea awe ameshinda au ameshindwa anawasilisha risiti zenye mchanganuo wa matumizi yake?

Swali: (2) Naomba mchanganuo wa kila mgombea anatakiwa apewe au atumie kiasi gani kuanzia kiti cha Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani?

Swali: (3) Katika orodha ya wagombea wa CCM nimeona jina la Deo Mwanyika ( Njombe - M ) Je ni yule Rais wa Acacia?

Swali: (4) Majina ya wagombea hawa yanauhusiano? Jennister Mhagama ( Peramiho ) na Joseph Mhagama ( Madaba ). Deo Sanga ( Makambako ) na Festo Sanga ( Makete ).
 
1.Aliondoa FAO la kujitoa, Sasa watu wanateseka
2.Alipora Bureau De Change
3.Akawanyima wana kagera Hela ya tetemeko iliyochangwa na wazalendo
4.Akawanyima wafanyakazi haki zao walizofanya kazi kwa kisingizio cha Watumishi hewa
5.Akaongeza makato ya Loans Board.
 
Back
Top Bottom