"Ulikuja kazini hujui kuvaa"

Weltmeisterschaftung

JF-Expert Member
Aug 27, 2014
364
247
Mimi ni mwenyeji wa mkoa wa Kigoma.

Siku ya kwanza nilipokwenda kwenda ku-report kazini mwaka 2011 kampuni moja ya Dar kabla ya kuletwa huku Tanga,nilichomekea suruali yangu nzuri tu nimeipiga pasi upanga unangaa mtoto wa kiume na shati safi pamoja na tai moja matata sana kama nilivyozoeshwa taratibu za uvaaji nikiwa primary, o level na hata high school.

Nilipofika kwenye ofisi na meneja rasilimali watu alinipokea vizuri sana na kuanza kunipitisha kwenye partition ya kila department nikitambulishwa kuwa mimi ni mfanyakazi wao mpya hivyo wanipe ushirikiano wa kutosha katika shughuli zangu.

Kilichonishangaza ni kwamba watu walikuwa wakinong'ona chini kwa chini kwa kila idara niliyokuwa nikitambulishwa na nilipokuja kuuliza baadaye baada ya kuzoeana nao nikaambiwa kuwa nilikuja ofisini nimevaa kama babu mzee wakati wao wanatupia vimodo vya kijanja. Kuna wakati watu wanatupia mpaka vimodo vinaishia chini ya magoti utafikiri anaenda disko kusakata rumba.

Nilishangaa sana na kujiuliza zile tabia njema za uvaaji tunazofundishwa mashuleni huwa zinapoteleaga wapi? Lakini kwa kuwa nilijua kwa maisha ya mjini kila mtu huwa ana ustaarabu wake nilipotezea.

Sasa unajua ni nini kilitokea,baada kupiga mzigo wa kufa mtu kama miezi sita nikapewa transfer kuletwa Tanga kuwa assistant branch manager na kuwaacha "wajanja wa mjini" wakiwa mdomo wazi hawana la kusema. Nilichojifunza tangu siku hiyo ni kuwa usafi unalipa sana pahala pa kazi na utaonekana ni mtu tofauti sana kama utajipenda na kujijali.
 
Ila huu unao itwa usafi kwa vijana wengi wa kuime unapita mipaka, Kijana ili aonekane msafi anapaka powder, sijui anatinda nyusi eti unakuta baba zima eti amepanga foleni asuguliwe miguu na kukutwa kucha tena saloon za kina dada zetu..
 
Ila huu unao itwa usafi kwa vijana wengi wa kuime unapita mipaka, Kijana ili aonekane msafi anapaka powder, sijui anatinda nyusi eti unakuta baba zima eti amepanga foleni asuguliwe miguu na kukutwa kucha tena saloon za kina dada zetu..
watu walikuwa wananishangaa utasema nimenyijea mkuu. mpaka nikawa ninajishtukia shtukia. kwa kweli si kuwa na raha siku za mwanzoni.
 
Mimi jamani mpaka kesho sipendi mwanaume wa kunyoosha trouser akaweka upanga halafu tena iwe na size pana... Ila hongera lkn sidhani kama umepata cheo kwasababu ya usafi wako, siamini pia kua wenzako hawakua smart.....
hanuna kigine zaidi ya kuwa smart ndio kulikonipa cheo dada yangu. kama suala ni uwezo kuna ambao wananizidi kidogo alafu ni wakongwe sana hapo kwa ofisi.
 
Point iko hivi yaani ww ulikuwa unapiga pamba za shamba na wenzio walikuwa wanapiga pamba za mjini sasa ww utapigaje pasi upanga unasimama acha ushamba
ila nilikuwa natoka bomba sana rafiki yangu...................naona ni wivu tu ulikuwa unawasumbua watoto wadogo wale.
 
Mimi ni mwenyeji wa mkoa wa Kigoma.

Siku ya kwanza nilipokwenda kwenda ku-report kazini mwaka 2011 kampuni moja ya Dar kabla ya kuletwa huku Tanga,nilichomekea suruali yangu nzuri tu nimeipiga pasi upanga unangaa mtoto wa kiume na shati safi pamoja na tai moja matata sana kama nilivyozoeshwa taratibu za uvaaji nikiwa primary, o level na hata high school.

Nilipofika kwenye ofisi na meneja rasilimali watu alinipokea vizuri sana na kuanza kunipitisha kwenye partition ya kila department nikitambulishwa kuwa mimi ni mfanyakazi wao mpya hivyo wanipe ushirikiano wa kutosha katika shughuli zangu.

Kilichonishangaza ni kwamba watu walikuwa wakinong'ona chini kwa chini kwa kila idara niliyokuwa nikitambulishwa na nilipokuja kuuliza baadaye baada ya kuzoeana nao nikaambiwa kuwa nilikuja ofisini nimevaa kama babu mzee wakati wao wanatupia vimodo vya kijanja. Kuna wakati watu wanatupia mpaka vimodo vinaishia chini ya magoti utafikiri anaenda disko kusakata rumba.

Nilishangaa sana na kujiuliza zile tabia njema za uvaaji tunazofundishwa mashuleni huwa zinapoteleaga wapi? Lakini kwa kuwa nilijua kwa maisha ya mjini kila mtu huwa ana ustaarabu wake nilipotezea.

Sasa unajua ni nini kilitokea,baada kupiga mzigo wa kufa mtu kama miezi sita nikapewa transfer kuletwa Tanga kuwa assistant branch manager na kuwaacha "wajanja wa mjini" wakiwa mdomo wazi hawana la kusema. Nilichojifunza tangu siku hiyo ni kuwa usafi unalipa sana pahala pa kazi na utaonekana ni mtu tofauti sana kama utajipenda na kujijali.
Ni Uvaaji wa kisabato ndio umekupa promo amaa?
 
Ukija kwenye auditing, tax,etc huku usafi wako kaa nao huko huko, huku ni kichwa chako tu ndo kinakubeba. Au ulikua ni secretary wa ofisi nini?
 
Back
Top Bottom