kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,255
- 16,185
Hakuna asiyependa kusifiwa, lakini kusifia sana kitu ni sawa na kukijaladia ili rangi yake halisi isionekane na kujulikana. Sifa nyingi ni sawa na ganzi inayomfanya mtu asijisikie maumivu akikwaruzwa.
Sifa muhimu yenye maana kwa aliyekuteua ni kufanya vizuri sana kwenye kazi alizokutaka uzifanye, baaasi. Watu wezi, wavivu na wazembe wa kazi wanamziba mdomo, macho na masikio aliyewateua kwa kumpamba na sifa zilizopitiliza uhalisia.
Ukiwa kwenye mamlaka ya uteuzi penda kukutana na kazi zenye takwimu za wateuliwa sio maneno na hotuba ndefu kama za kwenye kampeni za uchaguzi majimboni.
Ukikuta mteule anakupamba sana kwenye mikutano usivimbe kichwa bali mchunguze sana na sana na sana lazima utamkuta na madudu mengi sana.
Nikupe mfano wa mteule mmoja ambae alipewa idara nyeti sana na kubwa, mteule huyu alikuwa anajua kuyapanga maneno, alikuwa kwenye hotuba zake alikuwa akilitaja jina lote la mteule wake karibu hotuba yote, na maneno ya mh. fulani oyeeee! Kila wakati na mpigieni makofi Mh. Fulani kila wakati. Lakiñi kila akikaguliwa anakutwa na ugoigoi kwenye kazi zake hadi akaambiwa na mamlaka kuwa ajirekebishe ama sivyo asaidiwe, na hatimae akasaidiwa kweli kwa kuwekwa pembeni kwenye idara hiyo.
Ukiona mteule anamsifu kupita kiasi aliyemteua tuma jopo kubwa kukagua kazi zake na mwenendo wake, lazima utamkuta na kasoro.
Viongozi msilevywe na sifa za wateule wenu.
Sifa muhimu yenye maana kwa aliyekuteua ni kufanya vizuri sana kwenye kazi alizokutaka uzifanye, baaasi. Watu wezi, wavivu na wazembe wa kazi wanamziba mdomo, macho na masikio aliyewateua kwa kumpamba na sifa zilizopitiliza uhalisia.
Ukiwa kwenye mamlaka ya uteuzi penda kukutana na kazi zenye takwimu za wateuliwa sio maneno na hotuba ndefu kama za kwenye kampeni za uchaguzi majimboni.
Ukikuta mteule anakupamba sana kwenye mikutano usivimbe kichwa bali mchunguze sana na sana na sana lazima utamkuta na madudu mengi sana.
Nikupe mfano wa mteule mmoja ambae alipewa idara nyeti sana na kubwa, mteule huyu alikuwa anajua kuyapanga maneno, alikuwa kwenye hotuba zake alikuwa akilitaja jina lote la mteule wake karibu hotuba yote, na maneno ya mh. fulani oyeeee! Kila wakati na mpigieni makofi Mh. Fulani kila wakati. Lakiñi kila akikaguliwa anakutwa na ugoigoi kwenye kazi zake hadi akaambiwa na mamlaka kuwa ajirekebishe ama sivyo asaidiwe, na hatimae akasaidiwa kweli kwa kuwekwa pembeni kwenye idara hiyo.
Ukiona mteule anamsifu kupita kiasi aliyemteua tuma jopo kubwa kukagua kazi zake na mwenendo wake, lazima utamkuta na kasoro.
Viongozi msilevywe na sifa za wateule wenu.