MTZ 255Dar
JF-Expert Member
- Sep 25, 2018
- 1,114
- 3,768
Mapigano ya Bakhmut nimeyafuatilia kwa kina bila Upendeleo wowote ule. Ukweli uko hivi:
1.Wapiganaji wa WAGNER kazi yao ni kuuteka mji wa Bakhmut(City centre) wakitokea Mashariki mwa Dotnesk.
2.Wanajeshi wa Urusi (Russia Regular Army) walipewa kazi mbili:
(i) Kuteka vijiji vote vinavyouzunguka mji wa Bakhmut wakitokea Kusini na Kaskazini.
(ii) Kutoa Air Support na Arterraly kwa Vikosi vya Wagner. Wagner wanatumia Drones kupata Coordinates mahali wanajeshi wa Ukraine walipo then wanazituma kwa Wanajeshi wa Urusi ambao wanapiga Maroketi kuelekea huko.
Matokeo yake
1. Vikosi vya Wagner vimewazidi nguvu wanajeshi wa Ukraine ambao wanadhibiti sehemu ndogo tu (12%) ya Mji wa Bakhmut. Baada ya kuona hivyo, Wanajeshi wa Ukraine wameanza kuukimbia Mji wa Bakhmut kimkakati kama ifuatavyo:
(i) Brigade 3 za Wanajeshi wa Ukraine zimeelekea North ambapo baada ya Mapambano makali, wanajeshi wa Urusi wameanza kuyakimbia maeneo yao na kutekwa na wanajeshi wa Ukraine wanaokimbia mji wa Bakhmut ulioharibiwa.
(ii) Brigade 4 za Wanajeshi wa Ukraine zimeelekea South na kukumbana na wanajeshi wa Urusi. Mapigano makali yameripotiwa jana na Wanajeshi wa Urusi wamerudi nyuma umbali wa Mita 570 kuelekea Mashariki.
Malalamiko ya Kiongozi wa Wagner
Kuna Video kadhaa zimesambaa zikimuonesha Kiongozi wa Wagner akilalamika kwamba Wanajeshi wa Urusi wanayakimbia maeneo yao huko Kusini na Kasikazini mwa Bakhmut. Kitendo hicho kitasababisha Wapiganaji wa Wagner Kuzungukwa (Encircled) kama watasonga mbele kuuteka mji wa Bakhmut.
Kwahiyo tutalajie mambo 3:
1. Wanajeshi wa Wagner kuuteka mji wa Bakhmut na baadae kuzungukwa na vikosi vya Ukraine endapo wanajeshi wa Urusi wakiendelea kutimua Mbio.
2. Wapiganaji wa Wagner Kusitisha kusonga mbele kuelekea mji wa Bakhmut mpaka pale watakapoona Wanajeshi wa Ukraine wanarudishwa nyuma na Wanajeshi wa Urusi ili kuepuka kuzungukwa.
3. Wapiganaji wa Wagner kuuteka mji wa Bakhmut baada ya wanajeshi wa Urusi kuwarudisha nyuma wanajeshi wa Ukraine upande wa South na North. Mpaka sasa Urusi imepeleka Reinforcement ya wanajeshi 50,000 kuelekea Bakhmut ili kuzuia majeshi ya Ukraine yanayosonga mbele South na North.
1.Wapiganaji wa WAGNER kazi yao ni kuuteka mji wa Bakhmut(City centre) wakitokea Mashariki mwa Dotnesk.
2.Wanajeshi wa Urusi (Russia Regular Army) walipewa kazi mbili:
(i) Kuteka vijiji vote vinavyouzunguka mji wa Bakhmut wakitokea Kusini na Kaskazini.
(ii) Kutoa Air Support na Arterraly kwa Vikosi vya Wagner. Wagner wanatumia Drones kupata Coordinates mahali wanajeshi wa Ukraine walipo then wanazituma kwa Wanajeshi wa Urusi ambao wanapiga Maroketi kuelekea huko.
Matokeo yake
1. Vikosi vya Wagner vimewazidi nguvu wanajeshi wa Ukraine ambao wanadhibiti sehemu ndogo tu (12%) ya Mji wa Bakhmut. Baada ya kuona hivyo, Wanajeshi wa Ukraine wameanza kuukimbia Mji wa Bakhmut kimkakati kama ifuatavyo:
(i) Brigade 3 za Wanajeshi wa Ukraine zimeelekea North ambapo baada ya Mapambano makali, wanajeshi wa Urusi wameanza kuyakimbia maeneo yao na kutekwa na wanajeshi wa Ukraine wanaokimbia mji wa Bakhmut ulioharibiwa.
(ii) Brigade 4 za Wanajeshi wa Ukraine zimeelekea South na kukumbana na wanajeshi wa Urusi. Mapigano makali yameripotiwa jana na Wanajeshi wa Urusi wamerudi nyuma umbali wa Mita 570 kuelekea Mashariki.
Malalamiko ya Kiongozi wa Wagner
Kuna Video kadhaa zimesambaa zikimuonesha Kiongozi wa Wagner akilalamika kwamba Wanajeshi wa Urusi wanayakimbia maeneo yao huko Kusini na Kasikazini mwa Bakhmut. Kitendo hicho kitasababisha Wapiganaji wa Wagner Kuzungukwa (Encircled) kama watasonga mbele kuuteka mji wa Bakhmut.
Kwahiyo tutalajie mambo 3:
1. Wanajeshi wa Wagner kuuteka mji wa Bakhmut na baadae kuzungukwa na vikosi vya Ukraine endapo wanajeshi wa Urusi wakiendelea kutimua Mbio.
2. Wapiganaji wa Wagner Kusitisha kusonga mbele kuelekea mji wa Bakhmut mpaka pale watakapoona Wanajeshi wa Ukraine wanarudishwa nyuma na Wanajeshi wa Urusi ili kuepuka kuzungukwa.
3. Wapiganaji wa Wagner kuuteka mji wa Bakhmut baada ya wanajeshi wa Urusi kuwarudisha nyuma wanajeshi wa Ukraine upande wa South na North. Mpaka sasa Urusi imepeleka Reinforcement ya wanajeshi 50,000 kuelekea Bakhmut ili kuzuia majeshi ya Ukraine yanayosonga mbele South na North.