Ukweli wa Kustaajabisha Kuhusu Nyota za Angani

Status
Not open for further replies.
Monstgala nina swali.Umetumia muda mwingi kuelezea heavenly bodies.Ni somo zuri sana lakini kuna kitu kinausumbua moyo wangu.Tumeshuhudia majanga ya asili mbalimbali duniani yanayotokana na maumbile ya dunia yenyewe.Do we have any significant threat from these heavenly bodies?Kubadilika tabia ya maumbile na kuleta majanga ni jambo ambalo dunia imeshuhudia sana na kuathirika,tena katika siku za hivi karibuni inasemekana frequency ya kutokea majanga ya asili imeongezeka gradually kuliko zamani,vitu kama global warming na hivi karibuni wanasayansi wanadhani wamegundua global cooling,ni sehemu tu ya mambo yaonyeshayo kuwa as time goes on,something is not right with mother nature.Inabidi kuchunguza kila kitu ili kujiridhisha kwamba haya yanayotokea ni haya tu,au kuna makubwa yanajitengeneza chini kwa chini.So,vipi huko angani,ni salama au wanasayansi wameshaforesee matatizo siku za usoni?
 
Last edited by a moderator:
Space is so massive,, why was i born on this slave planet,, outta all the places?
 
Monstgala nina swali.Umetumia muda mwingi kuelezea heavenly bodies.Ni somo zuri sana lakini kuna kitu kinausumbua moyo wangu.Tumeshuhudia majanga ya asili mbalimbali duniani yanayotokana na maumbile ya dunia yenyewe.Do we have any significant threat from these heavenly bodies?Kubadilika tabia ya maumbile na kuleta majanga ni jambo ambalo dunia imeshuhudia sana na kuathirika,tena katika siku za hivi karibuni inasemekana frequency ya kutokea majanga ya asili imeongezeka gradually kuliko zamani,vitu kama global warming na hivi karibuni wanasayansi wanadhani wamegundua global cooling,ni sehemu tu ya mambo yaonyeshayo kuwa as time goes on,something is not right with mother nature.Inabidi kuchunguza kila kitu ili kujiridhisha kwamba haya yanayotokea ni haya tu,au kuna makubwa yanajitengeneza chini kwa chini.So,vipi huko angani,ni salama au wanasayansi wameshaforesee matatizo siku za usoni?

Mkuu, nimeegemea sana kwenye heavenly bodies ili kubaki katika mada kwa kiwango fulani maana licha ya kwamba hii area ni pana sana basi ukiongeza na upande mwingine unaeza ukatoka nje ya mada kwa kiasi kikubwa sana labda ugusie kwa ufupi tu. Kwa global cooling ni phenomena mpya na sina ufahamu mzuri kuhusu hii kitu labda kuna watu wanaojua zaidi. Lakini upande wa pili wa global warming ni wazi sisi wenyewe binadamu tuko responsible na swala hili hasa katika upande wa kuzuia au kupunguza carbon emmissions. Lakini kumbuka pia ina criticisms za hii kitu kama chanzo halisi cha mabadiliko ya tabia nchi na baadhi ya wanayansi wamekaa mbali nayo kutokana na utata fulani.

Kuhusu uhusiano wa haya madude yaliyoko angani na majanga yanayoweza kutokea hili lipo na kuna posts nyingi kabla zimeelezea threats mbalimbali kubwa na ndogo. Kinachoapply mara nyingi ni ukaribu na nguvu ya mvutano hivyo kili kilichokaribu zaidi kina effects fulani kuliko kile kilicho mbali, hii pia katika ukubwa kwa mfano Jua au sayari kubwa. Jupiter imekuwa ikituokoa sana tusigongwe na vimwondo vkubwa kwa kuwa ni kubwa na ina mass kubwa basi vimwondo vingi huvutwa kule kabla ya kuingia kwenye orbit yetu. Jua kwa upande mwingine ndio nyota iliyokaribu yetu hivyo ndio inayowezesha uhai wetu lakini pia ndio ina threat kubwa zaidi kutokana na nature yake. Ni nuclear fussion ile mambo mengi makubwa yanatokea kama effect ya gas zinazoungua pale.

Kutoka kwenye Jua kuna hatari nyingi zinaweza kuikumba dunia iwapo kusingekuwa na magnetic field, ozone layer, cirrus clouds etc. Mfano wa hizi threats ni Solar wind, solar flairs, solar magnetic field, solar radiations etc.

Magnetic field, au magnetosphere ya dunia, hatuioni kwa macho lakini inaanzia katikati ya dunia (kwenye core) inaenda mpaka kwenye space, ambapo inakutana na solar wind. Solar wind ni upepo wa anga za mbali unaokuja na particles zenye charge ya umeme kutoka kwenye jua. Sasa hapa hiyo magnetic field inatukinga na hizi charge zinazotokana na mwenendo wa activities za jua. Kama hizi zingekuwa zinafika bila pingamizi ni hatari isiyokuwa ya kawaida.

Alafu kuna plasma, hii inatulinda na mkondo mkubwa wa umeme kutoka kwenye jua. Jua kama bodies nyingine zote lina magnetic field yake ambayo hii inatokea kuna wakati inaungana na ile ya dunia (magnetic reconnections) hapo kunatokea dunia kupigwa na mkondo mkubwa wa umeme kutoka kwenye jua. Vifaa vingi vilivyo angani hupata matatizo na vimbunga na tufani vinasababishwa hili linapotokea. Plasma inapunguza mkondo huu kwa hiyo yanayosababishwa kama matokeao yana kuwa ni kiasi kidogo.

Alafu kuna cirrus clouds, haya mawingu hutambaa na kuziba sehemu kubwa ya anga la dunia kama vile theluthi moja na yanakuwa juu sana zaidi ya mawinguu mengine. ndege nyingi za abiria mara nyingi zinapita chini ya mawingu haya na yale yanayokuwa chini ni aina tofauti. Haya mawingu ni muhimu sana na yana-infulence global climate na kuzuia joto lisipotee kutoka kwenye dunia. Bila haya mawingu radiation na miale mikali kutoka kwenye jua ingekuwa inatua moja kwa moja na kusabaisha joto kali na pia matatizo kwa viumbe. Kuna research zinazoonesha human activities zinasababsha kuanza kubadilika kwa compostion ya mawingu ya aina hii na kuna mineral dusts ambazo ni wazi zitakuwa zinatokana na viwanda.
Zaidi ya hatari hizi ni zile za vimwondo na mambo mengine tuliyoongelea lakini kuna technology za kuangalia hatari inayoweza kutokea ghafla mfano Pan-STARRS, na nyingine nyingi.

Nimejaribu kugusia vitu vichache kwa ufupi lakini kuna mengineyo mengi kwa namna fulani.
 
Kuna swali nilikuuliza kuhusu tabia au tunatambuaje hii ni galaxy yetu na ile ni nyingine.
Kama inavyoeleweka kutoka sayari moja mpaka nyingine kuna utupu, kama ambavyo kuna utupu kutoka nyota moja hadi nyingine. Je, tunahitimisha vipi kwamba hapa ndo mwisho wa galaxy yetu na kwamba inafuata galaxy nyingine?

Pili, kwenye moja ya picha hapo juu umeeleza kuwa hata hicho kidoti kidogo sana cha mwanga inamaanisha galaxy nyingine, ni vipi galaxy iwe na mwanga wa kipekee kana kwamba ni dude moja lililoungana?
 
Monstgala shukrani mkuu.Uko deep eneo hili mkuu,nadhani nimepata mtu sahihi wa kumpa ombi langu.Ukiwa na muda natoa pendekezo uanzishe uzi kuhusu aina, historia na nafasi ya majanga ya asili katika dunia.au kama kuna mwana Jf yeyote anayeweza shughuli hiyo atutayarishie.mie napenda kuwa mchangiaji tuu kutokana na ufinyu wa muda nilio nao na huwa sipendi kukurupuka na kuongea vitu shallow hadharani.Watu mbalimbali wengi wanapita hapa JF,ni vema wenye JF yetu tukawapa "huduma" stahiki kama hii uliyoanzisha mkuu.big up.
 
Last edited by a moderator:
Kuna swali nilikuuliza kuhusu tabia au tunatambuaje hii ni galaxy yetu na ile ni nyingine.
Kama inavyoeleweka kutoka sayari moja mpaka nyingine kuna utupu, kama ambavyo kuna utupu kutoka nyota moja hadi nyingine. Je, tunahitimisha vipi kwamba hapa ndo mwisho wa galaxy yetu na kwamba inafuata galaxy nyingine?

Pili, kwenye moja ya picha hapo juu umeeleza kuwa hata hicho kidoti kidogo sana cha mwanga inamaanisha galaxy nyingine, ni vipi galaxy iwe na mwanga wa kipekee kana kwamba ni dude moja lililoungana?

Mkuu platozoom, Galaxy ni group kubwa la nyota na linatambulika pale mkusanyiko huo unapoishia. Ndio, kunakuwa na nafasi kati ya galaxy moja hadi nyingine na nafasi hii ni kubwa sana. Kuna utaalamu unaohitajika katika utambuzi ni iwapo utakuwa unaangalia kwa macho. Mfano Andromeda ni spiral galaxy kama ilivyo Milkyway hivyo umbo la mkusanyiko wa nyota zake unajulikana na unaweza kuutambua unapoangalia katika telescope ukiwa na utaalam. Hitimisho la wapi mwisho wa galaxy yetu linatokana na vipimo, utambuzi na technolojia husika.

Picha ile ya ultra deep space imepigwa kutoka katika satelite na mitambo yenye lenzi zenye nguvu sana zinaoendeshwa kwa mifumo ya computer. Kwa macho na hata kwa telescope image ile ya eneo la mbali kabisa katika space, haionekani angani. Kwa kuwa lile ni eneo la mbali sana basi mwanga pekee ulioweza kuonekana katika mitambo ile ni wa galaxies. Nyota iliyo mbali kiasi kile kama iko peke yake nje ya galaxy basi mwanga wake haujafika duniani bado au hautafika kabisa. Ndio mkusanyiko wa vyanzo vingi vya mwanga unafanya image iwe kama kitu kimoja inapoangaliwa kutoka mbali sana.

Image hii hapa chini ni ya miji miwili ya India (Mumbai na Pune) iliyopigwa picha kutoka kwenye space station wakati upande huu ulipokuwa usiku. Unaweza kuona maeneo mawili yenye mwanga mkubwa actually kila eneo ni mji mzima. Source ya mwanga ni taa ndogo ndogo za umeme katika barabara, majumba, magari etc lakini mkusanyiko huo unaleta image ya umbo kubwa lenye mwanga mkali. Kama picha hii ingechukuliwa mbali zaidi basi hata miji hii miwili ingeweza kuonekana kama vidoti viwili vya mwanga. Nadhani umenipata mkuu platozoom.

mumbai-pune.jpg
 
HAYA MAMBO UKIYAFUATILIA SAAAANA NI MWANZO WA KUPATA UWENDA WAZIMU:angry:

Pole sana mkuu.it's a normal thing for madness to be confused with genius.Imagine wale ndugu zetu wa enzi zile waliokuwa wakimwona Newton akirusha mawe juu halafu yakirudi chini,anayashangaa na kubaki akiyatazama mdomo wazi huku anatafakari kwa kina!hapo ni baada ya kumwona akipatwa na mstuko wa ajabu baada ya kuangukiwa na apple kichwani,akalishika na kulirusha tena juu,likarudi,mwanaume mdomo wazi,ha ha haa!bila shaka waswahili wangekuwepo karibu yake mungesema kapigwa kipapai.Mawe ni kitu cha kushangaa?!halafu anayarusha juu yakirudi chini anashangaa mdomo wazi!mungesema huu mtambo umepigwa kipapai "mawe",kumbe, thinking outside the box mwanaume anagundua maforces na magravity na maenergy....
 
Monstgala shukrani mkuu.Uko deep eneo hili mkuu,nadhani nimepata mtu sahihi wa kumpa ombi langu.Ukiwa na muda natoa pendekezo uanzishe uzi kuhusu aina, historia na nafasi ya majanga ya asili katika dunia.au kama kuna mwana Jf yeyote anayeweza shughuli hiyo atutayarishie.mie napenda kuwa mchangiaji tuu kutokana na ufinyu wa muda nilio nao na huwa sipendi kukurupuka na kuongea vitu shallow hadharani.Watu mbalimbali wengi wanapita hapa JF,ni vema wenye JF yetu tukawapa "huduma" stahiki kama hii uliyoanzisha mkuu.big up.

Shukrani, nikipata muda nitajaribu kuandika kwa urahisi mada hiyo ili tujifunze mambo mengi zaidi. Nashukuru kwa mchango wako na maswali.
 
Mkuu,najaribu kupitia post za nyuma taratibu,samahani kama maswali haya yatakuwa yameshajibiwa,hivi Nebula ni kitu gani?pili,kuna hii theory ya unirvesal expansion,kwamba ulimwengu unatanuka kwa kadri miaka iendavyo.Kama unaifahamu hebu tutupie kidogo mkuu ufahamuvyo.tatu,ningeomba ingawa ni somo zito,ila kama inawezekana utuelezee kisayansi ni nini kinashikilia hizi heavenly bodies.Physics iliyopo pale japo kwa ufupi tu,kiduuchu,kwa lugha rahisi kabisa.nasisitiza kiduuchu mkuu,usije ukatupasua vichwa.
 
Mkuu,najaribu kupitia post za nyuma taratibu,samahani kama maswali haya yatakuwa yameshajibiwa,hivi Nebula ni kitu gani?pili,kuna hii theory ya unirvesal expansion,kwamba ulimwengu unatanuka kwa kadri miaka iendavyo.Kama unaifahamu hebu tutupie kidogo mkuu ufahamuvyo.tatu,ningeomba ingawa ni somo zito,ila kama inawezekana utuelezee kisayansi ni nini kinashikilia hizi heavenly bodies.Physics iliyopo pale japo kwa ufupi tu,kiduuchu,kwa lugha rahisi kabisa.nasisitiza kiduuchu mkuu,usije ukatupasua vichwa.

Mkuu, Nebula ni mkusanyiko wa mavumbi ya gesi mbali mbali kwa wingi sana na hapa ndipo nyota nyingi huzaliwa. Hebu kabla hatujaenda mbali angalia post no 243, 249 na 253 expansion imegusiwa kidogo.

Na pia utaona katika posts tofauti jinsi nguvu tofauti za mvutano zinavyoelezewa kushikilia kila kitu kwa uwiano tofauti. Mfano dunia inashikilia mwezi kwa maana ya kwamba mwezi unaizunguka dunia kwa kutegemea centrifugal force. Sayari nyinginezo pia zinashikilia "mwezi" au "miezi" yao kama inakuwepo. Sayari zinashikiliwa na nyota kwa kuwa nyota zina mass kubwa. Kwetu nadhani solar system ni mfano mzuri. Nyota nazo zinashikiliwa na massive black holes katika center za galaxies (mostly). Na galaxies ingawa ni kubwa sana lakini kuna nguvu nyingi zinazofanya ziwe katika mwendo na shape zilizopo. Na ulimwengu mzima unaweza kuwa unashikiliwa na dark matter. Hii ipo, hatuijui vizuri lakini uwepo wake unafafanua maswali magumu. Ulimwengu au universe imeumbwa kwa asilimia kubwa ya hii kitu isiyoonekana au kupimwa kwa urahisi.
 
Mkuu DSN, Ni kweli wanasayansi wamethibitisha kwamba licha ya kwamba galaxies, nyota zilizomo, sayari, vimwondo, mavumbi na hata blackholes viko kwenye mwendo, lakini pia mwendo huo unaongezeka kasi. Hii concept ni muhimu sana maana inachangia/ilichangia kussuport Big-Bang theory kwa maana ya kwamba ule mlipuko lazima usababishe expansion. Katika moja ya matokeo ya hii kitu ina maana itafika kipindi baada ya muda mrefu sana galaxies zote na zitakuwa zimesafiri mbali sana na kutawanyika kiasi ambacho hatutaweza kuona galaxy nyingine karibu.

Kinachotisha au kushangaza ni kuwa mwendo huu unaongezeka zaidi na zaidi na hivyo kuna muda ambao haya madude yatakuwa kwenye mwendo mkali zaidi na kuachana zaidi. Mwisho wa hii hali haujatambulika vizuri lakini kuna theories nyingi juu yake na kwamba kutakuwa na upweke mkubwa kabisa baada ya mtawanyiko huu. Pia kuna concept zinazopendekeza kwamba baada ya muda fulani basi hizi galaxies zinaweza kuanza kurudi au kuvutwa mpaka pale kila kitu kitakapokandamizwa pamoja na kuwa kitu kimoja (singularity ) Na theory hii imeitwa Big crunch. Hii haina nguvu kwa sasa baada ya ungunduzi wa kwamba kasi hii ya ulimwengu kupanuka haipungui bali inaongezeka.

Lakini nini kinapelekea kasi iongezeke? Maana kwa kawaida ilitakiwa mwendo upungue kama kawaida ya mlipuko wowote. Sheria za kifizikia ni zile zile kwa jambo hili. Kwa kuwa ile nguvu ya msukumo uliotokana na mlipuko inapungua basi na galaxies na universe nzima ilitakiwa nayo ipungue kasi ya kutawanyika. Lakini kinyume na hili ulimwengu unapanuka tena kwa mwendo unaoongezeka na hili lilithibitishwa na wataalamu ambao walipata tuzo za Nobel kwa ugunduzi huu.

Sasa hapa kuna concepts nyingine zinazojaribu kufafanua nguvu hii kubwa sana ya ajabu inayovuta au kusukuma kila kitu katika universe mbali au kufanya universe ipanuke kwa mwendo unaoongezeka. Baadhi yake ni dark energy ambayo ndio maarufu yenye kuelezea hypothetically kuwepo kwa nguvu kubwa isiyoonekana ambayo either imejaa tu katika ulimwengu wote au kuna maeneo fulani katika ulimwengu kwa jinsi unavyopanuka na muda unavyoongezeka basi maendo haya yanakuwa na nguvu hii. Zaidi ya hii kuna Dark fluid na Phantom energy zote katika kujaribu kufafanua kilichopo nyuma ya kasi inayoongezeka ya kupanuka kwa universe.

Kuhusu jina hilo kama unavyoona imebidi nibadili maana linatumika kiuhalisia na kuna mtu analitumia. Ili kuepusha mgongano fulani imekuwa busara kubadili.

Aisee!kumbe kuna post hii humu!haa ha haa ha haa haa haaa,haa,haaa,haaa,upf,upf,upf,tihi hi hi hi hi ha ha haaa!haaa haa haaa,haaa!aisee libarikiwe tumbo lililokuzaa wewe kijana!aisee napitwa na maudambwidambwi hivi,jamaani!tuache utani haka kapost kamependeza kweeli,eti Eiyer Mkuu wa chuo Ntuzu munakaonaje jamani,ha ha haa haaa!aisee mleta mada wala huna haja kutaja jina,we endelea kutumia hiyo terminology ya dark energy tunaelewa tuu,usije ukaingia matatizoni na "watu wangu waangamiao kwa kukosa maarifa" kama haya hapa,ha haaa Eiyer anawajua,huangaika nao kila siku humu,wamemsababishia hadi matatizo ya afya kumlaza saa tisa usiku daily,hadi vitamin zimepungua mwilini haa ha haa!aisee kapost mbona sijakaona siku zote haka,jamaaaani!yaani ni kazito kuliko hata mada yenyewe,hata zile nyota ndogo zinazozaliwa kutokana na mkusanyiko wa "kunde"hazifikii uzito wa hii post,post bora ya mwaka huu jf ni hii!mods muturuhusu kutupia like zaidi ya moja kwa post jamaaani,jamaaani,mwe!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu platozoom, Galaxy ni group kubwa la nyota na linatambulika pale mkusanyiko huo unapoishia. Ndio, kunakuwa na nafasi kati ya galaxy moja hadi nyingine na nafasi hii ni kubwa sana. Kuna utaalamu unaohitajika katika utambuzi ni iwapo utakuwa unaangalia kwa macho. Mfano Andromeda ni spiral galaxy kama ilivyo Milkyway hivyo umbo la mkusanyiko wa nyota zake unajulikana na unaweza kuutambua unapoangalia katika telescope ukiwa na utaalam. Hitimisho la wapi mwisho wa galaxy yetu linatokana na vipimo, utambuzi na technolojia husika.

Picha ile ya ultra deep space imepigwa kutoka katika satelite na mitambo yenye lenzi zenye nguvu sana zinaoendeshwa kwa mifumo ya computer. Kwa macho na hata kwa telescope image ile ya eneo la mbali kabisa katika space, haionekani angani. Kwa kuwa lile ni eneo la mbali sana basi mwanga pekee ulioweza kuonekana katika mitambo ile ni wa galaxies. Nyota iliyo mbali kiasi kile kama iko peke yake nje ya galaxy basi mwanga wake haujafika duniani bado au hautafika kabisa. Ndio mkusanyiko wa vyanzo vingi vya mwanga unafanya image iwe kama kitu kimoja inapoangaliwa kutoka mbali sana.

Image hii hapa chini ni ya miji miwili ya India (Mumbai na Pune) iliyopigwa picha kutoka kwenye space station wakati upande huu ulipokuwa usiku. Unaweza kuona maeneo mawili yenye mwanga mkubwa actually kila eneo ni mji mzima. Source ya mwanga ni taa ndogo ndogo za umeme katika barabara, majumba, magari etc lakini mkusanyiko huo unaleta image ya umbo kubwa lenye mwanga mkali. Kama picha hii ingechukuliwa mbali zaidi basi hata miji hii miwili ingeweza kuonekana kama vidoti viwili vya mwanga. Nadhani umenipata mkuu platozoom.

mumbai-pune.jpg

Kwa hii post nimeshiba, ingawa nimepata tena njaa ghafla. Nitakuja na viswali vingine muda ukipatikana. Unatusaidia sana siye tuliokimbia 'Sayansi' mapema sana.
 
Pole sana mkuu.it's a normal thing for madness to be confused with genius.Imagine wale ndugu zetu wa enzi zile waliokuwa wakimwona Newton akirusha mawe juu halafu yakirudi chini,anayashangaa na kubaki akiyatazama mdomo wazi huku anatafakari kwa kina!hapo ni baada ya kumwona akipatwa na mstuko wa ajabu baada ya kuangukiwa na apple kichwani,akalishika na kulirusha tena juu,likarudi,mwanaume mdomo wazi,ha ha haa!bila shaka waswahili wangekuwepo karibu yake mungesema kapigwa kipapai.Mawe ni kitu cha kushangaa?!halafu anayarusha juu yakirudi chini anashangaa mdomo wazi!mungesema huu mtambo umepigwa kipapai "mawe",kumbe, thinking outside the box mwanaume anagundua maforces na magravity na maenergy....
Hahahaha mkuu juve umenifurahisha sana kwa hii post na ulichoongea hapo ni kweli kabisa.
 
Hayo manguvu yasiyojulikana na ni vigumu kuyachunguza/ dark forces Nishajua chanzo chake. Mungu muumba wa mbingu na dunia na yooote yanayoonekana na yasiyoonekana mwacheni tu aitwe Mungu.
Cc; eiyer
 
Aisee!kumbe kuna post hii humu!haa ha haa ha haa haa haaa,haa,haaa,haaa,upf,upf,upf,tihi hi hi hi hi ha ha haaa!haaa haa haaa,haaa!aisee libarikiwe tumbo lililokuzaa wewe kijana!aisee napitwa na maudambwidambwi hivi,jamaani!tuache utani haka kapost kamependeza kweeli,eti Eiyer Mkuu wa chuo Ntuzu munakaonaje jamani,ha ha haa haaa!aisee mleta mada wala huna haja kutaja jina,we endelea kutumia hiyo terminology ya dark energy tunaelewa tuu,usije ukaingia matatizoni na "watu wangu waangamiao kwa kukosa maarifa" kama haya hapa,ha haaa Eiyer anawajua,huangaika nao kila siku humu,wamemsababishia hadi matatizo ya afya kumlaza saa tisa usiku daily,hadi vitamin zimepungua mwilini haa ha haa!aisee kapost mbona sijakaona siku zote haka,jamaaaani!yaani ni kazito kuliko hata mada yenyewe,hata zile nyota ndogo zinazozaliwa kutokana na mkusanyiko wa "kunde"hazifikii uzito wa hii post,post bora ya mwaka huu jf ni hii!mods muturuhusu kutupia like zaidi ya moja kwa post jamaaani,jamaaani,mwe!

brother juve haya mafagio yako kwa mleta mada,yanamyima raha sana yule kaka yetu naniliyu.hapendi kuona kuna watu wanajua zaidi yake.ha ha ha.
 
Last edited by a moderator:
brother juve haya mafagio yako kwa mleta mada,yanamyima raha sana yule kaka yetu naniliyu.hapendi kuona kuna watu wanajua zaidi yake.ha ha ha.

Ha ha haa!mkuu acha uchokozi bhana!bila shaka hili kombora umelielekeza kwa kaka yangu "hakuna naniliu" teh teh!
 
Kwa hii post nimeshiba, ingawa nimepata tena njaa ghafla. Nitakuja na viswali vingine muda ukipatikana. Unatusaidia sana siye tuliokimbia 'Sayansi' mapema sana.

Ndugu yangu unatisha kwa Sayansi sasa mimi nina swali" hivi karibuni nilisikia katika kituo cha habari cha BBC kwamba wanasayansi huko marekani kwa kutumia darubini yako kubwa zaidi wameweza kugundua uwepo wa nyota ifananayo na jua ila hiyo ni kubwa maradufu ya jua letu hili na ina mwanga mkali zaidi pia! Sijui kama unaweza kunielezea vizuri juu ya hili jambo nikaelewa vizuri"'
 
Ndugu yangu unatisha kwa Sayansi sasa mimi nina swali" hivi karibuni nilisikia katika kituo cha habari cha BBC kwamba wanasayansi huko marekani kwa kutumia darubini yako kubwa zaidi wameweza kugundua uwepo wa nyota ifananayo na jua ila hiyo ni kubwa maradufu ya jua letu hili na ina mwanga mkali zaidi pia! Sijui kama unaweza kunielezea vizuri juu ya hili jambo nikaelewa vizuri"'

Cheki post uliyo-quote, mimi si mwanasayansi mkuu!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom