Ukweli: Pombe inavyoufanya mwili wako

Ukweli: Pombe inavyoufanya mwili wako

uvugizi

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
1,348
Reaction score
1,097
.

Mtu anapokunywa pombe anahisi kujisikia raha Fulani , hata kuhisi kujiamini zaidi na mambo kama hayo , kunakomfanya asahau hata madhara yake.

Madhara ya pombe ni mengi mno, mfano ubongo kutiratibu vuzuri mambo ya fikra , poor judgements, mfadhaiko, hypothermia , kutapika tapika au kichefu chefu , kutopumua vizuri , kifafa cha pombe , kuchanganyikiwa , hasira na kushindwa kujipangilia .

Pombe unapokunywa 33% inaingia moja kwa moja katika damu kupitia kuta za utumbo mwembamba na mpana , na katika tissue zote za kibayolojia za mwili. Pombe inaingia haraka sana katika Mwili ( damu) na hapo kwa kadri unavyoongeza kiwango BAL yake inaongezeka ( BLOOD ALCOHOL LEVEL).

Madhara ya BAL kuongezeka ni mengi , kubwa ni kupungua uwezo kuchakata taarifa za vitu vinavyotembea na impaired vision / perceptions. Laws enforcers ( traffic police) duniani na hapa kwetu Tanzania wanasimamia hili la blood alcohol concentration kwa kutumia kifaa maalum kinachoitwa BREATHALYZER.

Kuwepo kwa alcohol nyingi katika damu ( BAL) kuna madhara makubwa kuliko watu wanavyofikiri . blood alcohol level ikizidi na kuzoea mwili , automatically wewe ni Mgonjwa wa pombe una ALCOHOLISM.. yaani unakuwa tena huwezi kudhibiti pombe ila pombe inakudhibiti wewe.

Katika Mwili wa mwanadamu kuna kitu kinaitwa GLUTATHIONE ( GSH),,,, hii ni antioxidant ya mwilini yaani ni chemical inayofanya mwili usidhurike na OXIDATION ,,, Mchakato wa oxygen katika mwili wetu . oxygen ina mazuri na mabaya yake kisayansi .

GLUTATHIONE ( GSH) ni kitu muhimu sana katika mwili wetu , mfano ..... Ndiyo inayofanya cell za mwili kugawanyika na kustawi vizuri mwilini kuepusha hata cancer, ,,,, kurepair na kulinda mfumo wa DNA,,,Kudhibiti kiasi cha protini na kusafirisha Amino acid vizuri .

GLUTATHIONE, ndiyo enzymes catalysis mechanism , yaani umeng'enywaji wa chakula unafikiwa vizuri GSH ikiwa safi.

GSH , inapambana na sumu zote zisizohitajika ( metabolisms of xenobiotics)

GSH inachakata hydrogen peroxide( H202), kama antioxidant kufanya Maji yeyote unywayo yasikuletee madhara .

Kwa ujumla madhara ni mengi kama mwili ukikosa GLUTATHIONE ( GSH) .

sasa kitu kinachofanyika katika Mwili wako ukinywa pombe ni kuwa GLUTATHIONE ( GSH) Inaondoka kabisa , hivyo kuuacha Mwili na maangamizi ya magonjwa mbalimbali, ambayo hata hospitality zetu hawajui pakuanzia kwani wanaacha msingi wa tatizo .

Mshangao wangu mkubwa ni kuwa kiasi kidogo cha GLUTATHIONE , huwa kinaoneka kwa wagonjwa wa UKIMWI na walevi wenye high BLOOD ALCOHOL LEVEL ..

Kama mtu wa kiroho biblia imeonya sana kuhusu pombe

Refer Mithali 20:1,, 21:17,,,:23:29-35 na Mithali 31:4

Paulo pia aliwaonya watakatifu kuhusu pombe waefeso 5:18 .

Be inspired
 
Lily Pesa zungusha round nyingine kwanza kuna mtu anatoa somo la pombe.
Utadhani tunaumwa na kufa walevi tu sasa kuna wale wanatusema kua pombe inatugharimu sana pesa zetu wakati wao bado wanapambana na baba mwenye nyumba mpaka kesho hua natamani kuwauliza hili.
 
Back
Top Bottom