Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,356
Katika maisha kuna changamoto nyingi tunapitia. Bahati nzuri ni kuwa kuna maendeleo ya sayansi na tekinelojia inasaidia maisha yaendelee. Wengine walipata mimba za utotoni lakini kwa msaada wa familia na jamii waliweza kuendelea na shule na sasa hivi wana ujuzi unawawaezesha kujitegemea, wengine wana magonjwa sugu lakini yako controlled na madawa na wanaweza kuendelea na maisha. Wengine wali pata majanga ya picha zao za ngono kusambaa kwenye mitandao ya kijamii au mpenzi wa zamani alizihifadhi.
Pale unapokutana na mpenzi mpya, mpaka atake namba yako ya simu au kuomba akutoe kwa chakula ni lazima kuna aliyovutiwa na wewe. Pale pale mwanzo wa kujuana, ukimuona muelekeo wake na umeanza kumuamini, mueleze yale ya muhimu ambayo hayafichiki katika maisha yako kama hayo niliyoyataja hapo juu.
Unavyo yaacha itakuuia vigumu kuyaeleza huko mbele. Fikiria mtu anajipanga akatoe mahari kwenu ndiyo anajua kuwa unawatoto wawili, una HIV au cancer, anaonyeshwa picha zako za ngono za miaka 5-10 iliyopita. Huyu mtu hatakuamini tena. Ni wachache wanaoweza kukuelewa.
Hakuna aliyekamilika lakini mapenzi yanahitaji watu wawili wanaoweza ku compromise hitilafu zao na kuishi pamoja kwa amani.
Pale unapokutana na mpenzi mpya, mpaka atake namba yako ya simu au kuomba akutoe kwa chakula ni lazima kuna aliyovutiwa na wewe. Pale pale mwanzo wa kujuana, ukimuona muelekeo wake na umeanza kumuamini, mueleze yale ya muhimu ambayo hayafichiki katika maisha yako kama hayo niliyoyataja hapo juu.
Unavyo yaacha itakuuia vigumu kuyaeleza huko mbele. Fikiria mtu anajipanga akatoe mahari kwenu ndiyo anajua kuwa unawatoto wawili, una HIV au cancer, anaonyeshwa picha zako za ngono za miaka 5-10 iliyopita. Huyu mtu hatakuamini tena. Ni wachache wanaoweza kukuelewa.
Hakuna aliyekamilika lakini mapenzi yanahitaji watu wawili wanaoweza ku compromise hitilafu zao na kuishi pamoja kwa amani.