Jana nilimsikia Katibu mkuu wa Ccm redio Clouds, nadhani alikuwa Tanga akisema kigezo cha kwanza kwa mgombea atakayeteuliwa na Ccm itakuwa ni uadilifu. Alisema pia wagombea wa Ccm wanaoutaka urais itabidi wajipime kwa kigezo hicho namba moja. Ni juzi tu Mzee Msuya alisema Lowassa kama anaenda upinzani aende lakini chama hakiwezi kumpitisha fisadi kugombea urais.
Kama ni mfuatiliaji wa mambo ya iasa za nchi hii utajua kwamba Lowassa alikuwa karibu sana na viongozi wa dini, lakini juzi tu walitoka hadharani na kumnanga kama 'fisadi msaka Ikulu'. Hawa ni watu wanaheshimika sana na mara nyingi wanakuwa taarifa nyeti toka hata Ikulu. Mtu kama Pengo ni figure kubwa nchi hii, anajua yaliyo uvunguni Ikulu.Kama angekuwa amedokezwa kwamba ndiye mgombea wa Ccm ajaye asingethubutu kumchana hadharani au maaskofu wenzake kumnanga!
Wale 'Team Lowassa' mjiandae kisaikolojia kutupwa kwa mgombea wenu maana tangu imeanza 2015, hali inazidi kuwa mbaya. Mashambulizi yanatoka kila pembe tena kwa watu wanaoheshimika. Baba Askofu Mokiwa, Baba Askofu Pengo, Nzigirwa, Mzee Msuya! Mlishajiuliza hivi karibuni Pengo alienda kufanya nini Ikulu?
Tafakari!
Kama ni mfuatiliaji wa mambo ya iasa za nchi hii utajua kwamba Lowassa alikuwa karibu sana na viongozi wa dini, lakini juzi tu walitoka hadharani na kumnanga kama 'fisadi msaka Ikulu'. Hawa ni watu wanaheshimika sana na mara nyingi wanakuwa taarifa nyeti toka hata Ikulu. Mtu kama Pengo ni figure kubwa nchi hii, anajua yaliyo uvunguni Ikulu.Kama angekuwa amedokezwa kwamba ndiye mgombea wa Ccm ajaye asingethubutu kumchana hadharani au maaskofu wenzake kumnanga!
Wale 'Team Lowassa' mjiandae kisaikolojia kutupwa kwa mgombea wenu maana tangu imeanza 2015, hali inazidi kuwa mbaya. Mashambulizi yanatoka kila pembe tena kwa watu wanaoheshimika. Baba Askofu Mokiwa, Baba Askofu Pengo, Nzigirwa, Mzee Msuya! Mlishajiuliza hivi karibuni Pengo alienda kufanya nini Ikulu?
Tafakari!