Ukweli mchungu katika malezi ya watoto

Ukweli mchungu katika malezi ya watoto

h120

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2012
Posts
2,545
Reaction score
3,370
21728321_1744810895550884_7737776949623724391_n.jpg


Ujumbe murwa kabisa kwa kina baba fulani na kina mama fulani, malezi bora hayanunuliwi hutengenezwa na walezi/wazazi, kumnunulia mtoto nguo za thamani, michezo, shule za gharama hazitoshi kukamilisha malezi bora.
Tumia muda kukaa na watoto ujue mienendo yao, nini wanataka, wafahamu uwepo wa baba na mama, kwa kufanya hivyo utakuwa umetimilisha wajibu wako kama mzazi bora.

Watoto wanapobadilika tabia na kuharibikiwa kitu cha kwanza mzazi kulalamika ni gharama anazotumia kumlea mtoto, ""Yani nahangaika kazini ili msome shule nzuri....."" baadhi ya malalamishi.

Ewe mzazi jenga mazoea ya kuyaishi maisha ya uzazi halisi.
Tafakari chukua hatua.
 
Kwa hali ya sasa tumerud kuyaishi maisha ya uzazi....siku hizi had nakagua madaftar huku nikisubir taarifa ya habar ianze...
 
Sasa tufatanya Kazi saa ngapi
Dah..... Hii dunia kuna wanasayansi jamii....wanasayansi maumbo....wanasayansi uchumi...wanasayansi siasa.....ukiwasikiliza wote utaishiwa kuchanganyikiwa.....Pambana na hali yako[emoji13] [emoji13] [emoji87]
 
Umeanza vizuri sana mkuu ila hapo mwisho mwisho kama umetupunja kitu mkuu.

By the way, shukrani sana
 
Back
Top Bottom