Mtumishi Wetu
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 5,712
- 1,906
Wadau nina hakika wote tuna kiu ya kujua ukweli ni nini na nani hasa wahusika waliomtesa na kumpiga Daktari wetu Ulimboka. Sasa kwa vile serikali haitaki kama inavyo onyesha kuunda tume huru ya kupata ukweli halisi wa waliohusika na kuwachukulia hatua za kisheria basi wadau waunde tume huru ya kufanya uchunguzi. Interested parties kama madaktari, UN Human Wrights Commission waruhusiwe kuunda tume huru na kupewa hushirikiano ili ukweli halisi uweze kujulikana!!!Kama itatokea kuundwa bungeni vile vile ni sawa tu ila Watanzania tunahitaji kujua ukweli wa swala hilo. Kwa maana nchi yetu bado tunaamini ni ya amani na usalama sio rouge state inayoendeshwa kidekteta!!! Tunaomba Mhe Spika Anna Makinda na wasaidizi wake waache kabisa mtindo wa kuwa mawakili wa CCM na serikali wajue kuwa wamewekwa pale kwa maslahi ya wananchi wooote wa Tanzania si kwa niaba ya chama kimoja cha CCM!!! Wasimamie kuendesha mijadala huru kwenye bunge letu tukufu akitilia maanani kuwa wahusika wakuu kwenye mijadala ya bunge ni Watanzania na usalama wao, wasidharau matukio yanayomhusu Mtanzania yeyote kama Dr Ulimboka ilivyotokea Watanzania tunataka kujua ukweli!!!! Nawasilisha!!