Ukweli kuhusu ugaidi

Ukweli kuhusu ugaidi

Joined
Jul 22, 2019
Posts
5
Reaction score
5
Ugaidi ni miongoni mwa majanga makubwa yanayo ikumba dunia hivi sasa.Na cha kusikitisha zaidi ni kua janga hili limeambatanishwa na dini na kila tendo la kigaidi litokeapo,hufungamanishwa na dini hasa uislamu.

Amini nawaambieni,mtu yeyote anaweza kufanikisha azma yake yoyote,iwapo kutakuwepo na nadharia iwezayo kumhalalishia au kuhalalisha mambo yanayo husu hiyo azma yake.Nadharia humpa mtu some sort of inspiration kw a lile alilo na azma nalo.bila hiyo nadharia,Mtu huyu hufeli,kwa kukosa kichocheo kinacho mshinikiza kufanikisha azma yake.Huu ni ukweli mtupu hata katika nyanja nyingine za kibinadamu.Na huu ndio ukweli unao husu ugaidi.

Naam,yapo mataifa yaliyo jikita katika kuuangamiza ugaidi kwa kuutumia uislamu,kwa vifaa vikali na vya kisasa zaidi na wanajeshi lukuki,lakini hili peke yake halitosaidia kuuangamiza ugaidi moja kwa moja.Licha ya kua magaidi huwa nao wamejiandaa kisilaha huwa wamejiandaa kinadharia pia.

Na hii nadhari ndio muhimu zaidi kwa sababu ndio ipelekayo kila kitu.Sasa,hapa sio ishu ya bunduki kwa bunduki bali inafaa iwe ishu ya nadharia kwa bunduki.Jambo lolote huanzia ndani ya bongo,hivyo kuupiga ugaidi itatupasa tung'oe mizizi yake katika mabongo yetu,hivyo tupaswa tuje na nadharia itakayo tuwezesha kuipiga nadharia ya kigaidi.

Na nadharia hii ni nadharia ya Amani.Tukumbuke kua,hata taifa liwe na nguvu kiasi gani haliwezi afford vita vya Mara kwa Mara,bali magaidi wanaliweza hili.Kwa sababu wao malengo yao sio ushindi peke yake Bali pia kifo ni katika malengo yao makubwa.Gaidi ana amini akifa anaenda peponi moja kwa moja,hivyo ushindi na kifo vyote vina hadhi sawa.Hivyo kivyovyote wao wanaamini ni washindi

Karibuni waungwana,michango yenu ni muhimu zaidi,na naomba muniwie radhi nilianza bila kuwasalimu.
 
Wanaopinga ugaidi ndio hao hao wanaoutengeneza ugaidi ili tu kusambaratisha kitu kinachowakwamisha ktk mambo yao kwa faida yao.

Na maeneo mengi yenye upinzani mkubwa na mabeberu wa magharibi yana rasilimali,, sasa ili mabeberu wapate izo rasilimali ndo wanakuja na propaganda ya ugaidi ili wajipatie uhalali wa kujitwalia izo rasilimali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
-Kuna slogan ya kusamehe saba mara sabini.
-Pia kuna slogan ya usidhulumu wala usikubali kudhulumiwa, tena hapa unasisitizwa kabisa ukifa hali ya kua unapigania haki yako uliyo dhulumiwa unaingia peponi.
-Kuna vijana aliojikatia tamaa ya maisha kwakukosa ajira na shughuli za kuwaingizia kipato, wakiwa brain washed kidogo na kupewa kiasi kidogo cha pesa, hushawishika kirahisi hutumiwa kufanya ugaidi kwa manufaa ya wengine.
 
Back
Top Bottom