Ukweli kuhusu teknolojia ya solar

Pia kadri unavyounganisha mzigo mkubwa zaidi ndipo na battery inavyokwisha chaji kwa muda mfupi zaidi.Ndio maana unashauriwa kutumia vifaa vyenye umeme kidogo kama vile taa au tube light za energy saver n.k.
 
Jubilant ahsante ndugu na mimi nimedesa...

Pia nimehamia mbali na mpango wa TANESCO. Na hata ningekuwa karibu siwapendi. Mimi sijui kabisa sayansi ya umeme, kwa hiyo hata kujua idadi ya Watt ninazohitaji ni mtihani, ila najua vifaa ninavyohitaji. Najumlisha tu linearly Watt za kila kifaa au vp? Kutenganisha vifaa pia sijaelewa kivipi? Yaani niwe na panel tofauti kwa matumizi tofauti au?

Ombi langu, mi nilitaka kupata huduma ya mshauri kabla ya kuita mkandarasi wa kuweka huo umeme. Mshauri ningeongea nae mahitaji yangu ili afanye hayo mahesabu kisomi. Sijui kama wapo washauri wa umeme wa daraja la nyumba za kuishi au hadi yale yanayoitwa Towers tu?.

Kama yupo please nahitaji huduma hii.
 
Ni kweli kwanza inabidi ujue watts ngapi unahitaji. Rahisi kukadiria hizi kwa sababu vifaa vyote vya umeme huandikwa watts zake (au Amps na Volts - Ohm's law itakupatia Watts)

Nyumba ndogo inahitaji kama 3KWatt (nakisia hapa inategeme vifaa). Kwa kweli ni gharama kubwa kujitegemea kiumeme. Bila ya grid (Tanesco ) inabidi uwe na mchanganyiko wa solar, windmill na stand-by generator ili likikosekana jua au upepo utategemea generator.
Tatizo kubwa la umeme wa solar (au wind) ni jinsi ya kuuhifadhi umeme wakati unatengenezwa ili siku za mawingu au usiku uchote umeme kutoka kwenye hifadhi yako. Njia rahisi inayotumika kuhifadhi umeme ni kutumia deep-cycle batteries . Kawaida hizo huwa na uwezo wa 12V. Unatakiwa kutengeneza Battery Bank kwa kuzipangilia battery kama 4 mpaka 8 in parallel or series kutokana na mahitaji ya vifaa vyako.

Kwa ufupi vitu unavyohitaji:

1. Solar Panels (ziko aina nyingi hizi - Tahadhari na wabongo wasikuuzie vioo vya kichina)

2. Charge controller (kwa sababu ya kurekebisha umeme unaotoka kwenye panel usizidi na kuharibu battery)

3. Invertor - Kubadilisha umeme wa jua DC kwenda kwenye umeme wa nyumbani AC. Hizi ziko ambazo unaweka ukutani kwenye plug na ina-supply kwenye circuit yako ya nyumbani.

4. Deep cycle batteries ( hizi ziko kama battery za magari )

Ushauri wangu binafsi ni upate kama solar panels 3 au 4 za 250Watts/each na circuit yako iwe inakunywa umeme kwa matumizi ya taa, fans na vifaa vidogo vidogo. Achana na vifaa vikubwa kama vile Oven.

Kwa kweli ukishapata vifaa hivyo (ukimpta mdau akakutolea China bei poa) kufunga ni rahisi sana unahitaji elimu ya darasa la saba tu. Uchawi wa umeme wa jua ukishavifunga vifaa vyote basi unacheka tu kwasababu hamna bili tena na hivi
vitu hudumu kama miaka 30 hivi. Angalia mchoro hapo chini.

sysdiag_1_with12vbulb_400.jpg


¬K

Heshima kwako kuli,

Tafadhali naomba kuuliza swali dogo,nimeutazama mchoro kuna maswali mawili naomba kupata ufafanuzi kidogo.
[1] Mchoro unaonyesha bulbu inachukua umeme moja kwa moja kutoka kwenye charge controller bila kupitia kwenye Invertor.Kwa hiyo bulbu zitakuwa zinatumia umeme wa DC ?.

[2] Mchoro unaonyesha pia vifaa kama computor vitakuwa vinapata umeme uliobadilishwa kwa maana ya kupitia kwenye Inverter kutoka umeme wa DC kwenda umeme wa AC ?.Naomba kujuzwa kama niko sahihi au kuna mahali nimechemka ?.



 
[1] Mchoro unaonyesha bulbu inachukua umeme moja kwa moja kutoka kwenye charge controller bila kupitia kwenye Invertor.Kwa hiyo bulbu zitakuwa zinatumia umeme wa DC ?.

Hapana, hiyo bulb ni pilot na mara nyingi hutumika kupoteza umeme wa ziada wakati battery zimejaa charge. Bulb zote za nyumbani zinatumia umeme wa AC.

[2] Mchoro unaonyesha pia vifaa kama computor vitakuwa vinapata umeme uliobadilishwa kwa maana ya kupitia kwenye Inverter kutoka umeme wa DC kwenda umeme wa AC ?.Naomba kujuzwa kama niko sahihi au kuna mahali nimechemka ?.
Umeme unaotoka kwenye inverter ndio unaelekea kwenye circuit ya nyumba na una-power vifaa nyote vya nyumbani.

¬K
 
Nisaidie ili kama siyo nione uwezekano wa kuitumia kwa pasi pia.

Bishoke,

Unaweza kutumia kifaa chochote cha umeme kwa kutumia umeme wa jua. Ili kufanya hivyo unahitaji uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa umeme. Vilevile gharama za matengenezo inapokuja kwenye large scale ni kubwa na unahitaji mtu mwenye expertise kushughulikia batteries na controllers. Kwa matumizi makubwa ya nyumbani (Pasi, Heater, AC nk) Tanesco bado ni rahisi sana kwenye uwekezaji mpaka kuupata umeme. Mfano naelewa wakati fulani TRC walikuwa wanatumia solar energy kwenye mitambo ya mawasiliano. Kwenye kila solar panel kama nakumbuka sawasawa walikuwa na battery banks mbili, ya volts 48 kila moja yenye battery 24 za 2V/600AH. Ukiweza kupata battery/proper solar panel na controllers unaweza kuzalisha umeme wa kutosha kwa matumizi yeyote nyumbani, Swali ni je inalipa?
 
Binafsi natumia solar power kwa miaka miwili sasa na tanesco hata sitaki kuwasikia hata kidogo na nimeshauri marafiki zangu nao wamefunga solar
Solar power inategemea na load utakayo funga
nakushauri ukisie mahitaji yako halafu upost na mie niakupa data zote na contacts numbers za wapi unawaza pata at whole sale prices
Naomba utupatie specs ya hiyo installation yako. Natanguliza shukrani.
 
Mmh itabidi niwatembelee Umeme Jua,vitu kama friji itabidi nitafute zinazotumia mafuta ya taa sijui zama hizi kama zipo,kama kuna ndugu anajua wapi naweza kupata friji ya mafuta ya taa jamani atujuze hapa,siku hizi mgao upo wa kinyemela hapa bongo.
''Maisha bora kwa kila Fisadi''
 
Mimi naombeni data wapi nitapata mitambo ya 'wind energy' hapa kwangu kuna upepo mwingi tu 24x7!

Kuna wachina fulani walikuwa nayo wakati wa maonesho ya Sabasaba mwaka jana. Ngoja niangalie kama naweza kupata brochure yao niloyochukua. Otherwise Nakushauri u-google nina uhakika utapata somewhere in this small world.
 
Naamini umeme wa jua ni mzuri sana kwani ni kama unagarimia mara moja (one time investment) na unaendelea kufaidika kwa muda mrefu. Hata hivyo unahitaji fundi makini wa kukushauri ubora wa vifaa vya kununua na jinsi ya kuvifunga.

Nasema hivyo kwani mwishoni mwa mwaka 2008 nilifunga solar nyumbani kwangu kwani umeme wa TANESCO haijulikani wataleta lini pamoja na kuwa imeshapita miaka wamepima. Nilipofunga kwa mara ya kwanza tulikuwa na uwezo wa kuwasha taa kwa masaa kama manne mpaka sita. TV tulikuwa na uwezo wa kuangalia mpaka masaa matatu. Lakini kadri muda ulivyokwenda ndivyo nguvu ilipungua. Mpaka ikafika kipindi baada ya mwaka mmoja hata taa zilikuwa zinawaka kwa saa moja na TV ndo kabisa haiwaki. Tulipomuuliza fundi aliyetuwekea kasema kuwa ni kwa sababu ni kipindi cha baridi (Eneo lenyewe ni Arusha). Hali hiyo ikaendelea mpaka ikafika hata taa kuwaka ni shida ndipo tukaamua kumuuliza fundi mwingine.

Huyu fundi mwingine alipokuja akashangaa jinsi huyo fundi wa kwanza alivyounganisha (wiring) na akasema tayari battery haina kazi (it was a dry battery). Akarekebisha wiring na kutushauri kununua battery mpya.

Baada ya kununua battery mpya umeme sasa unawaka usiku kucha na TV tunaangalia mpaka tunaenda kulala bado ina nguvu. Kwa hiyo ni vizuri kupata fundi wa uhakika kwenye suala hili naamini utasahau kama kuna bill ya TANESCO.

Hata hivyo fundi wa sasa ameshangaa kuwa tukinunua battery mpya (dry) tunaichaji kwani ndiyo ulikuwa ushauri wa huyo fundi wa kwanza. Sasa sijui wataalamu hapa wanipe ushauri battery mpya ya dry tunaicharge kabla ya kuifunga au hakuna haja ya kuicharge na je ukifunga dry battery ni baada ya muda gani itatakiwa kubadirishwa?
 
Binafsi natumia solar power kwa miaka miwili sasa na tanesco hata sitaki kuwasikia hata kidogo na nimeshauri marafiki zangu nao wamefunga solar
Solar power inategemea na load utakayo funga
nakushauri ukisie mahitaji yako halafu upost na mie niakupa data zote na contacts numbers za wapi unawaza pata at whole sale prices

Mkuu nini madhara ya kuchaj betri bila charger control. .?
Ukiwa unachaj n shart ulegeze mifuniko kwa betri za maji..?
 
Back
Top Bottom