Ukweli kuhusu Reborn International

Ukweli kuhusu Reborn International

kayimukaa

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2014
Posts
494
Reaction score
669
Habari wakuu,
Nilituma maombi ya kazi reborn international, sasa leo wamenijibu kwa email kuwa nimechaguliwa na natakiwa niende kwenye mafunzo yao tarehe 22 mwez huu.

Sasa kilichonistua na kuja kuuliza hapa ni wao kuniambia niwatumie tsh 51000 kwa mpesa/tigo pesa au benki na vyeti vyangu kupitia email ili waweze kuvihakiki hivyo vyeti kupitia kwa mwanasheria/mtaalam wao kabla ya tarehe 15 mwezi huu wa 3.

Je wakuu mnaonaje, na kama kuna mwakilishi au yeyote anaejua kuhusu reborn international naomba unifahamishe maana naona kama kuna dalili za kuingizwa mjini/choo. Naombeni msaada wenu wakuu, nilipe hiyo hela au usanii tu.

=====================

Habari. Mnamo mwezi uliopita kuna organisation inajiita REBORN INTERNATIONAL walitangaza nafasi za kazi kwa malipo ya Tsh 4,530,000/= kwa miezi mitatu kwa position ya Civic and Voters Education Officers concerning with Tanzania Referundum Support Project. Mnamo jana wameanza kujibu waliomba na kuwaambia wamefanikiwa kupata nafasi hizo na kuwaambia kwamba wa scan vyeti vyao na kuvituma kwa mwanasheria wao vikiambatana na Tsh 51,500/= as a verification fee inayotumwa kwenye namba walizoweka ama kwenye akaunti ya Twiga Bancorp Bank.
PLEASE AND PLEASE WADOGO ZANGU MNAIBIWA SO MSITUME HIZO PESA. NAWASILISHA.

Tangazo hili halina dalili ya ukweli
  1. Tovuti zote walizotaja kwenye maombi ya kazi hazina uhusiano wa moja kwa moja na kazi wanazofanya na nyingine haijasajiliwa kabisa
  2. Tangazo kukimbilia kutaja mshahara(unaovutia maombi) na nafasi(idadi kubwa) kabla ya mambo ya msingi kwenye ajira husika kama vigezo na majukumu
  3. Cha zaidi, kama mleta mada alivyolileta. Kuambiwa atoe pesa kwanza na kwenda moja kwa moja kwenye mafunzo(ajira) bila kupitia mchakato wowote wa kupata hio ajira(angalau hata usaili wa ulaghai)
 
Habari wakuu,
nilituma maombi ya kazi reborn international, sasa leo wamenijibu kwa email kuwa nimechaguliwa na natakiwa niende kwenye mafunzo yao tarehe 22 mwez huu.
sasa kilichonistua na kuja kuuliza hapA ni wao kuniambia niwatumie tsh 51000 kwa mpesa/tigo pesa au benki na vyeti vyangu kupitia email ili waweze kuvihakiki hivyo vyeti kupitia kwa mwanasheria/mtaalam wao kabla ya tarehe 15 mwezi huu wa 3.
Je wakuu mnaonaje, na kama kuna mwakilishi au yeyote anaejua kuhusu reborn international naomba unifahamishe maana naona kama kuna dalili za kuingizwa mjini/choo. Naombeni msaada wenu wakuu, nilipe hiyo hela au usanii tu.
ni majambazi,waambie ufanye kazi kwa mwezi mmoja afu uwape mshahara wote
 
Kaz au interview yoyote ukiombwa hela huo ni utapeli...kuwa makini, km vp watafute ofisi yao uwaone physically

Siku hz matapeli (makanjanja) wanatumia tatzo la ukosefu wa ajira kutengeneza matangazo na tovuti feki ili kuwatapeli watu.
 
Tangazo la kaz hili linishaliona ukweli ni kwamba ni utapeli...!!!usijribi kutuma hela wewe..kuna vyombo vya kisheria vinaakiki vyeti sio lazima wanasheria wao
 
Habari wakuu,
nilituma maombi ya kazi reborn international, sasa leo wamenijibu kwa email kuwa nimechaguliwa na natakiwa niende kwenye mafunzo yao tarehe 22 mwez huu.
sasa kilichonistua na kuja kuuliza hapA ni wao kuniambia niwatumie tsh 51000 kwa mpesa/tigo pesa au benki na vyeti vyangu kupitia email ili waweze kuvihakiki hivyo vyeti kupitia kwa mwanasheria/mtaalam wao kabla ya tarehe 15 mwezi huu wa 3.
Je wakuu mnaonaje, na kama kuna mwakilishi au yeyote anaejua kuhusu reborn international naomba unifahamishe maana naona kama kuna dalili za kuingizwa mjini/choo. Naombeni msaada wenu wakuu, nilipe hiyo hela au usanii tu.
Mkuu hiyo kazi uliomba online?manake utapeli huu huwa upo kwa kazi amabzo application zilifanyika online.....wpotezee washenzi hao kama ni kazi utapata uvumulivu ndio kitu cha msingi mkuu....
 
Tangazo la kaz hili linishaliona ukweli ni kwamba ni utapeli...!!!usijribi kutuma hela wewe..kuna vyombo vya kisheria vinaakiki vyeti sio lazima wanasheria wao

Boss unajua nami nimeomba kazi kwenye tangazo hilo sasa ukisema ni waongo unanitisha maana mpunga walioutangaza sio wa kawaida nadhan ilikua 4.53m sasa kuna haja ya kujua ukweli wao, binafsi namshauri atafute ofisi zilipo akapata uhakika zaidi mana huenda ikawa kweli na ukajikuta umepiga teke fuko la hela, ahsante
 
Mkuu kwani kazi gani hiyo uliyoiomba? Au ndiyo ile ya civic and voter education officer?
 
Hiyo imekaa kiwiziwizi! Achana nayo kabisa, wewe unatafuta kazi halafu unaambiwa utume pesa? Kwanza uhakiki wa vyeti ni jukumu la anaekuajiri sio lako! Waambie wakuite ufanye kazi mwisho wa mwezi utawalipa hiyo pesa ya uhakiki wa vyeti ukipokea mshahara!
 
Wale walikuwa matapeli wa ajira mkuu usijaribu kutuma chochote
 
Mnamo tar11-14 feb kuna tangazo la kazi katika mitandao mingi kutoka kwa kampuni inayoitwa REBORN INTERNATIONAL nafasi 100.
Tangazo hili hapA. http://www.zoomtanzania.com/ListingUploadedDocs/Job_Adverts.pdf

Wametoa majibu lakini cha ajabu na kushangaza ni kwamba unatakiwa kutuma fedha kwa ajili ya uthibitisho wa vyeti. Sh 51500
Kipande cha Email waliyotuma

Ningependa kujuzwa nadhani sio mimi tuu bali na wengine wengi waliokumbwa na hili

Je hi kampuni ni ya ukweli? Au ni matapeli?
 
sisi wenyewe hatujui ni ya ukweli au ni matapeli, ila akili kichwani kwako!
 
Email yenyewe hii hapa
 

Attachments

  • 1425384751242.jpg
    1425384751242.jpg
    43.1 KB · Views: 417
Mnamo tar11-14 feb kuna tangazo la kazi katika mitandao mingi kutoka kwa kampuni inayoitwa REBORN INTERNATIONAL nafasi 100.
Tangazo hili hapA. [url]http://www.zoomtanzania.com/ListingUploadedDocs/Job_Adverts.pdf [/URL]

Wametoa majibu lakini cha ajabu na kushangaza ni kwamba unatakiwa kutuma fedha kwa ajili ya uthibitisho wa vyeti. Sh 51500
Kipande cha Email waliyotuma

Ningependa kujuzwa nadhani sio mimi tuu bali na wengine wengi waliokumbwa na hili

Je hi kampuni ni ya ukweli? Au ni matapeli?
Sasa mkuu fanya hivi ili kurahisisha mambo na siku nyingine usisumbuke kuuliza watu jf. Wewe chukua hiyo elfu 51 kisha tuma halafu sikilizia majibu ndiyo utapata uhakika kama ni kweli au sio kweli. Humu jf wengi wababaishaji tu hawatakupa jibu kamili
 
Walikijaga kama hao wakala 50, 50 za watu wakasepa mi nilikoswa koswa. Now wengine tena kazi kwako.
 
Sasa mkuu fanya hivi ili kurahisisha mambo na siku nyingine usisumbuke kuuliza watu jf. Wewe chukua hiyo elfu 51 kisha tuma halafu sikilizia majibu ndiyo utapata uhakika kama ni kweli au sio kweli. Humu jf wengi wababaishaji tu hawatakupa jibu kamili

Nataka ushauri kutoka kwa watu. Huwezi jua. Yawezekana ni kweli na wapo wenye vithibitisho au ni uongo na uthibitisho wa uhakika ukawepo. Kuuliza si ujinga japo kuna kuangalia
 
Back
Top Bottom