Ukweli kuhusu narcissist

Ukweli kuhusu narcissist

Marmeid

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2024
Posts
528
Reaction score
1,219
Katika maisha ya kila siku, huwa tunakutana na watu wa aina mbalimbali—wenye upendo, huruma, upole, kujali, na pia wale ambao ni wakatili kimya kimya, wenye kujipenda kupita kiasi, wasiojua kupokea makosa, wala kuona umuhimu wa wengine. Hawa wa mwisho ndio mara nyingi huitwa "Narcissists" – yaani, watu wenye hulka ya kujipenda kupindukia na kutanguliza maslahi yao mbele ya kila kitu, hata kwa gharama ya wengine.

Narcissist ni Nani?
Mtu narcissist ni yule anayeonesha viwango vya juu vya kujiona bora kuliko wengine, anapenda sifa kupita kiasi, hapendi kuambiwa ukweli au kukosolewa, huwa hana huruma kwa hisia za wengine, na huona kuwa dunia yote inapaswa kumzunguka yeye.

Tabia Zinazomtambulisha Narcissist
1. Hujiona bora kuliko wengine– Hata bila sababu ya msingi, anaamini kuwa yeye ni wa kipekee zaidi.
2. Huhitaji sifa za mara kwa mara– Anataka kuambiwa kila mara kuwa ni mzuri, bora au wa kipekee.
3. Hukosa huruma– Hana uwezo wa kuelewa au kujali hisia za wengine.
4. Hudhibiti na kutawala wengine– Hutaka kila kitu kiwe kama anavyotaka yeye.
5. Hupinga kukosolewa– Mara nyingi hukasirika au hupuuza anapokosolewa.
6. Huwa na uhusiano wa kinafiki – Anaweza kuwa na watu kwa sababu ya faida, si kwa upendo wa kweli.

---

Madhara ya Narcissism Katika Maisha ya Kawaida

1. Uhusiano Mbovu na Watu Wengine
Watu narcissists mara nyingi hupoteza marafiki, familia au wapenzi kwa sababu ya tabia yao ya kujifikiria wenyewe pekee. Hawajali hisia za wengine, jambo ambalo husababisha migogoro ya mara kwa mara.

2. Upweke wa Kijamii
Ingawa hujionyesha kuwa wanafuraha au wamejitosheleza, narcissists wengi huishia kuwa wapweke kwa sababu watu huwachoka kutokana na tabia zao za kudharau na kuumiza wengine.

3. Kushindwa Kujifunza na Kukuwa
Kwa kuwa hawapokei ushauri au kukosolewa, wanashindwa kubadilika au kujifunza, hivyo hukwama kimaendeleo.

4. Migogoro Kazini au Shuleni
Katika mazingira ya kazi au masomo, narcissist hushindwa kushirikiana vyema na wengine, hupenda sifa zote kwao, na huchukia mafanikio ya wenzao.

---

Madhara ya Kuwa Katika Mahusiano na Narcissist

1. Kudhulumiwa Kisaikolojia (Emotional Abuse)
Mpenzi wa narcissist hujiona si wa thamani, huishi kwa hofu ya kukosolewa, hujiona hafai, na anaweza kuanza kujichukia mwenyewe kutokana na kudharauliwa na kukosolewa kila mara.

2. Kupoteza Utambulisho (Loss of Identity)
Muda mwingi mpenzi huishi ili kumfurahisha narcissist. Anajikuta hajitambui tena, hana sauti katika uhusiano.

3. Upweke Katika Uhusiano
Ingawa yupo kwenye mahusiano, mtu anaweza kujihisi mpweke kwa sababu hakuna upendo wa kweli, hakuna kuelewana, na mahusiano yanakuwa upande mmoja.

4. Kuvunjika kwa Uhusiano
Kwa sababu ya tabia za kujiona, uongo, ukosefu wa huruma, na udhibiti, mahusiano ya narcissist mara nyingi huwa mafupi au ya mateso hadi kufikia kuvunjika.

---

Je, Unawezaje Kukabiliana na Narcissist?

  • Tambua tabia zao mapema – Jifunze dalili za narcissist ili usiwe mtego wa mapenzi au urafiki usio na afya.
  • Weka mipaka – Usikubali kudhibitiwa au kuishi maisha yasiyo yako ili kumfurahisha.
  • Jiamini na jithamini – Usiruhusu mtu akufanye ujihisi hufai au hutoshi.
  • Omba msaada wa kitaalamu – Endapo umeumia kisaikolojia kutokana na kuwa karibu na narcissist, usisite kuzungumza na mshauri wa afya ya akili.

---

Hitimisho
Narcissism ni hali inayoweza kumharibu mtu mwenyewe na wale walio karibu naye. Hali hii ikiachwa bila kueleweka au kudhibitiwa, inaweza kuharibu maisha, mahusiano, na hata mustakabali wa mtu. Ni muhimu kujitambua, kuthamini utu wako, na kujifunza kuishi na watu kwa upendo na heshima. Jitahidi kuwa mkweli, mwenye huruma na mnyenyekevu – hayo ndiyo yanayofanya maisha yawe na maana ya kweli.
 
Kiukweli ukitazama jamii ya sasa na tukasemwa tufanyiwe diagnosis ya tabia, wanawake watabainika kuwa ni Narcissist kwa wingi sana.

Hizi tabia umeongelea hapa ni character ambazo unaweza zipata zote ndani ya mwanamke m'moja.

Kupenda attention. Wanawake wengi wanapenda sana attention isiyo na ulazima. Sawa wewe ni mzuri,sasa ndio ujitangaze mitandaoni tena kwa picha za mitego ili iweje na ukitongozwa unajifanya kama hautaki.

Kujiona bora kuliko wengine. Hii tabia ipo 100% kwa wanawake. Anatoka familia ambayo haina hata pikipiki na baba yake huwa asubuhi anawahi kazini kwa kutumia daladala,mama yake ni mama wa nyumbani au ni mama ntilie. Huyu binti anaetoka familia ya hivi anakutaka na kijana ambae amepambana ana miliki IST au Passo anaishi nyumba ya sebule,jiko,vyumba viwili vya kulala,amejiweka vizuri. Anamtaka yeye anamuonyesha ni levels za akina Kim Kardashian kuwa anadate na wanaume ma'CEO wenye makampuni watakao mpangishia apartments masaki. Hebu nambie kuwa wanawake wasasa wengi hawapo hivi?

Kupenda sifa, wanawake wa sasa na sifa ni chipsi na tomato. Popote walipo wanataka sifa ziwazunguke sifa hata ambazo hawastaili. Mtu kaweka wigi (nywele feki) mwanaume ukimtazama na kukaa kimya ana nuna ukimuuliza anasema "ina maana haujaona nywele zangu? Hizo nywele bandia ni zako kivipi ng'ombe wewe?🤔

Kukosa huruma: hii sifa sidhani hata kama natakiwa kuelezea maana hata mashosti zao wanajua. Hawa wanawake wa sasa anaweza kukuomba hela ya saloon wakati umetoka kumwambia mama yako anaumwa yupo hospital na asifeel hata chembe ya huruma. Anaweza kukubambikia mimba ambayo si yako anakutazama unavyohangaika kulea mtoto si wako yeye kimya na ana amani kabisa. Anaweza kukudump kimahusiano baada ya kumaliza chuo kwasababu kakutana na mwanaume ambaye kamuahidi ajira, makazi mapya na simu mpya therefore anaona wewe huna umuhimu tena anakudump fasta.

Kidhibiti na kutawala wengine. Hii ipo very common kwa wanawake. Ushawahi kuona vile vigrupu vyao utadhani wachawi. Sasa tongoza rafiki yake uone namna wanavyouvaa huo uhusiano na kutaka kumcontrol rafiki yao afanye wanavyotaka wao. Watazame hata katika mahusiano yao,hela hatoi hata kidogo ila yeye ndie anataka apange mkaishi wapi,mtoke out mara ngapi,muende wapi,umnunulie nini,ujiskie vipi,upumue mara ngapi kwa siku, anataka kila kitu kiende anavyopanga au kujiskia yeye in the name of "happy wife happy life". Nambie hawa sio naturally born Narcissists.

Kupinga kukosalewa. Tazama katika mahusiano mengi nani huchukua majukumu na kuwajibika hata ambapo hajakosea? Mwanamke anaweza kutaka mwanaume awe na pesa ila akachukizwa na ubusy wake halafu akatumia tena kuwa kisingizio cha kujitongozesha kwa rafiki za huyo mume wake,then akistukiwa mwanaume akamkosoa mwenendo wake anaanza kujiliza na kuchukia kukosolewa. Hata hapa JF mnaona tukiwakosoa tabia zao mfano kuzaa nje ya Ndoa,kupenda kudanga, na maviburi yao utaona namna wanavyokuwa defensive na kutopenda kukosolewa na kugeuza mijadala uwanja wa mabishano.

Kuwa na mahusiano ya kinafiki. Hii hata haiitaji mtu kuwa na cheti cha form 4 kuona. Wengi wa wanawake wanahitaji sababu za kimaslahi kuwa katika uhusiano na ndio maana wengi wao hawawezi kudeal na mwanaume m'moja sababu ya huo unafiki. Wanawake wengi sababu zinazowafanya kutokuwa waaminifu kimahusiano hazina uhusiano na mapenzi ya kweli ila zinauhusiano wa moja kwa moja na maswala ya kifedha na kupenda vitu ambavyo havipatikani kirahisi na kwa muda mfupi bali vinataka subira,muda na jitihada kuvipata.

Kimsingi Narcissist anaweza kuwa yoyote, mwanaume au mwanamke. Ila ukifanya analysis na uchambuzi wa kitabia utagundua wanawake kwa idadi yao 90% ni Narcissist tena by default. Wanaanza kuwa Narcissists at age 16 kwenda juu.

Chunguza hii utanambia.
 
Kiukweli ukitazama jamii ya sasa na tukasemwa tufanyiwe diagnosis ya tabia, wanawake watabainika kuwa ni Narcissist kwa wingi sana.

Hizi tabia umeongelea hapa ni character ambazo unaweza zipata zote ndani ya mwanamke m'moja.

Kupenda attention. Wanawake wengi wanapenda sana attention isiyo na ulazima. Sawa wewe ni mzuri,sasa ndio ujitangaze mitandaoni tena kwa picha za mitego ili iweje na ukitongozwa unajifanya kama hautaki.

Kujiona bora kuliko wengine. Hii tabia ipo 100% kwa wanawake. Anatoka familia ambayo haina hata pikipiki na baba yake huwa asubuhi anawahi kazini kwa kutumia daladala,mama yake ni mama wa nyumbani au ni mama ntilie. Huyu binti anaetoka familia ya hivi anakutaka na kijana ambae amepambana ana miliki IST au Passo anaishi nyumba ya sebule,jiko,vyumba viwili vya kulala,amejiweka vizuri. Anamtaka yeye anamuonyesha ni levels za akina Kim Kardashian kuwa anadate na wanaume ma'CEO wenye makampuni watakao mpangishia apartments masaki. Hebu nambie kuwa wanawake wasasa wengi hawapo hivi?

Kupenda sifa, wanawake wa sasa na sifa ni chipsi na tomato. Popote walipo wanataka sifa ziwazunguke sifa hata ambazo hawastaili. Mtu kaweka wigi (nywele feki) mwanaume ukimtazama na kukaa kimya ana nuna ukimuuliza anasema "ina maana haujaona nywele zangu? Hizo nywele bandia ni zako kivipi ng'ombe wewe?🤔

Kukosa huruma: hii sifa sidhani hata kama natakiwa kuelezea maana hata mashosti zao wanajua. Hawa wanawake wa sasa anaweza kukuomba hela ya saloon wakati umetoka kumwambia mama yako anaumwa yupo hospital na asifeel hata chembe ya huruma. Anaweza kukubambikia mimba ambayo si yako anakutazama unavyohangaika kulea mtoto si wako yeye kimya na ana amani kabisa. Anaweza kukudump kimahusiano baada ya kumaliza chuo kwasababu kakutana na mwanaume ambaye kamuahidi ajira, makazi mapya na simu mpya therefore anaona wewe huna umuhimu tena anakudump fasta.

Kidhibiti na kutawala wengine. Hii ipo very common kwa wanawake. Ushawahi kuona vile vigrupu vyao utadhani wachawi. Sasa tongoza rafiki yake uone namna wanavyouvaa huo uhusiano na kutaka kumcontrol rafiki yao afanye wanavyotaka wao. Watazame hata katika mahusiano yao,hela hatoi hata kidogo ila yeye ndie anataka apange mkaishi wapi,mtoke out mara ngapi,muende wapi,umnunulie nini,ujiskie vipi,upumue mara ngapi kwa siku, anataka kila kitu kiende anavyopanga au kujiskia yeye in the name of "happy wife happy life". Nambie hawa sio naturally born Narcissists.

Kupinga kukosalewa. Tazama katika mahusiano mengi nani huchukua majukumu na kuwajibika hata ambapo hajakosea? Mwanamke anaweza kutaka mwanaume awe na pesa ila akachukizwa na ubusy wake halafu akatumia tena kuwa kisingizio cha kujitongozesha kwa rafiki za huyo mume wake,then akistukiwa mwanaume akamkosoa mwenendo wake anaanza kujiliza na kuchukia kukosolewa. Hata hapa JF mnaona tukiwakosoa tabia zao mfano kuzaa nje ya Ndoa,kupenda kudanga, na maviburi yao utaona namna wanavyokuwa defensive na kutopenda kukosolewa na kugeuza mijadala uwanja wa mabishano.

Kuwa na mahusiano ya kinafiki. Hii hata haiitaji mtu kuwa na cheti cha form 4 kuona. Wengi wa wanawake wanahitaji sababu za kimaslahi kuwa katika uhusiano na ndio maana wengi wao hawawezi kudeal na mwanaume m'moja sababu ya huo unafiki. Wanawake wengi sababu zinazowafanya kutokuwa waaminifu kimahusiano hazina uhusiano na mapenzi ya kweli ila zinauhusiano wa moja kwa moja na maswala ya kifedha na kupenda vitu ambavyo havipatikani kirahisi na kwa muda mfupi bali vinataka subira,muda na jitihada kuvipata.

Kimsingi Narcissist anaweza kuwa yoyote, mwanaume au mwanamke. Ila ukifanya analysis na uchambuzi wa kitabia utagundua wanawake kwa idadi yao 90% ni Narcissist tena by default. Wanaanza kuwa Narcissists at age 16 kwenda juu.

Chunguza hii utanambia.
Zemanda head stomer 💉 💯
 
Back
Top Bottom