Kipenzi Changu
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 58,072
- 134,443
Chadema mkoa wa Rukwa wamesisitiza kwa kutoa tamko zito la kuungana na Kamati Kuu kwa kutekeleza maandamano na kufanya mikutano ya amani mkoani humo. Mwenyekiti wa Chadema amesema kuwa operesheni ukuta itapiga mikutano 449 siku ya Septemba 1.Mwenyekiti amewaomba wanachama na watanzania wote waliotelekezwa na CCM kujitokeza kwa amani.Naye katibu amesema hamasa ni kubwa sana mkoani humo.Amesema pia kuwa mikutano itakuwa katika namna zote,kwa mikutano mikubwa,ya kijiji kwa kijiji au hata penye watu watano watafanya mikutano