Uchaguzi 2020 Ukoloni mamboleo ni agenda ya kampeni za mwaka 2020?

mwengeso

JF-Expert Member
Nov 27, 2014
9,219
6,650
Ukoloni mamboleo (neo-colonialism) ni nini?

Ukoloni mamboleo unaeleweka kwa mapana kama mwendelezo wa siasa ya kibepari ambayo inaziwezesha mamlaka za kibepari (baadhi ya mataifa yaliyoendelea na mashirika yake) kutawala mataifa maskini kupitia shughuli za kibepari km kuwekeza mitaji kwenye maeneo watakayofaidika badala ya njia ya utawala wa moja kwa moja.

Je, Tanzania bado iko kwenye ukoloni mamboleo na kama ipo ni jinsi gani taifa linaweza kujikomboa? Je, vyama vya siasa vina sera gani kuikomboa nchi kwenye ukoloni mamboleo?

Lissu, mgombea Urais wa tikiti ya CHADEMA, ameulizwa hilo swali, akipewa ridhaa ya kuongoza nchi hii, atachukua hatua gani kuikomboa kwenye ukoloni mamboleo? Akijibu swali hilo amesikika akisema, nanukuu: ni maneno ya wanaofuata mfumo wa kijamaa akina Nyerere na Nkurumah. ... katika uchumi wa dunia ya leo ambao ni interconnected (kufungamana) ni upuuzi, ujinga na upumbavu kuzungumzia ukoloni mamboleo. ... yaani kuwekeza mitaji yao kwenye uchumi wetu, ndio ukoloni maendeleo? ... Je, nchi yetu inaweza kuendelea kiuchumi bila uwekezaji huo?

Majibu ya swali hilo yako kwenye YouTube hii hapa. Ni majibbu yanayofikirisha kama Lissu, mgombea Urais, anajua siasa za kiuchumi au hajui kuwa hajui?


Je, anajua kuwa ukoloni mamboleo ni nchi kutawaliwa kiuchumi na mataifa ya nje? Je, anajua kuwa matokeo ya ukoloni mamboleo ni pale mitaji ya kigeni kutumika kwa ajili ya unyonyaji badala ya maendeleo ya nchi maskini duniani? Je, anatambua kuwa uwekezaji, chini ya ukoloni mamboleo huongeza, badala ya kupunguza, pengo kati ya nchi tajiri na maskini duniani?

Yawezekana ni tafsiri ya Sera ya Uchumi iliyoainishwa kwenye Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu, 2020. Kwamba Chadema kimejipanga kuutafsiri ukuaji wa uchumi kwa vitendo ili kuwepo kwa mabadiliko chanya katika maisha ya kila Mtanzania. Hili litawezekana kwa kufumua mfumo wa sasa wa uchumi wa kijamaa ambao umeshindwa kuboresha hali ya maisha ya Watanzania, na kuanzisha mfumo wa soko jamii ambao unalenga kufungua fursa kwa kila mtu kutumia vipaji vyake katika kuzalisha na kumiliki mali. Mfumo huu mpya wa uchumi wa soko utaambatana na kujenga, kuimarisha na kusimamia uchumi wa kitanzania kwa kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwa njia ya ubia na hisa na wawekezaji wenye mitaji mikubwa.

Kwa upande wake, katika Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu 2020, CCM inatambua umuhimu wa kujenga uchumi wa kitaifa ili kuhakikisha kwamba Watanzania ndio wanufaika wakuu wa uchumi na maliasili za nchi na ndiyo wenye kauli juu ya namna uchumi unavyoendeshwa. Kwa muktadha huo CCM itaelekeza Serikali kuendelea na juhudi za kuifanya Tanzania kuwa nchi inayojitegemea kiuchumi pamoja na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na nchi nyingine. Juhudi maalum zitaelekezwa kuhakikisha rasilimali za asili za nchi hii, hasa ardhi, madini, gesi asilia, mafuta, maji na misitu zinanufaisha wananchi na Taifa kikamilifu.

Tukikubaliana na dhana ya ukoloni mamboleo, kwa msingi kwamba nchi maskini bado hazijajikomboa kiuchumi, ni dhahiri kuwa Sera ya kuanza na maendeleo ya vitu kutachochea kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja, jamii na taifa. Km kuwepo kwa miundombinu imara ya usafirishaji kutamwezesha mzalishaji mali (mwenye kiwanda, mkulima, mvuvi, mchimbaji madini, nk) kuuza bidhaa zake nje ya eneo lake kwani ukubwa wa soko unaongezeka.
 
Nadharia ya ukoloni mamboleo, nadharia ya mabeberu iliasisiwa na wajamaa baada ya kushindwa kuwaletea waafrika maendeleo pindi walipowafukuza wakoloni weupe kwa mbwembwe kwamba tunaweza jitawala. Baada ya kushindwa kujitawala huku wakizifukarisha nchi zao kwa aibu ili wasionekane hawawezi yaani wameshindwa wajamaa Kama kina Nyerere wakawatumia kina Walter Rodney kuja na machapisho ya kuwatupia lawama wazungu na kuwaita majina Kama mabeberu, ukoloni mamboleo Kama njia ya kujifichia udhaifu wa kushindwa kwao binafsi. Swali huo ukoloni mamboleo au mabeberu wapo afrika pekee why Asia, Vietnam, Brazil, falme za kiarabu, Korea kusini, Malaysia, India wao wameendelea japo sote tulitawaliwa?
 
Unategemea wazungu kwa kila kitu, huo ukoloni mamboleo utakuachaje?
Bila ukoloni mamboleo tungepata ARVs na mengineyo?
 
..ukoloni mamboleo ni hoja ya KIPUMBAVU.
Inaitwa kushift burden Ni sawa na Adam kumsingia Hawa kwa kusema si huyu mwanamke uliyeniletea.Ukoloni mamboleo Ni syllabus za waliosoma zamani miaka ya 70 wengi akili zao zilifungwa kwenye box wasiwe na mawazo ya kuwazidi akili watawala.
Kizazi cha sasa kina global thinking nikiamini huwezi endelea kwa kuwa kisiwa.Huna raslimali umekaa nazo zinakusaidia nn Sasa Kama uzitimii eti unazilinda.Maendeleo Ni sawa na kucheza draft huwezi funga bila kuliwa.Nchi zote zilizoendelewa zinaliwa na nchi zingine.
Waliowekeza USA sio wamarekani Ni watu toka mataifa mengine mfano china,uk,France,nk wanaitafuna USA hivyo hivyo waliowekeza china , USA,uk Ni kutoka mataifa mengine mfano USA,nk yaani we unachuma toka kwetu nasi tunachuma toka kwenu.
 
Ukoloni mamboleo, mabeberu ni nadharia za watawala walioshindwa kuwaletea maendeleo watu wao sawa na mbaazi kusingizia jua
 
Hili ni miongoni mwa thread bora nilizowahi kusoma kuhusu neo colonialism aisee kumbe lisu aingizwe kwenye orodha ya magreat thinker bcoz anafikiria vitu ambavyo huwez kudhan an
 
Ukoloni mamboleo (neo-colonialism) ni nini?

Ukoloni mamboleo unaeleweka kwa mapana kama mwendelezo wa siasa ya kibepari ambayo inaziwezesha mamlaka za kibepari (baadhi ya mataifa yaliyoendelea na mashirika yake) kutawala mataifa maskini kupitia shughuli za kibepari km kuwekeza mitaji kwenye maeneo watakayofaidika badala ya njia ya utawala wa moja kwa moja.

Je, Tanzania bado iko kwenye ukoloni mamboleo na kama ipo ni jinsi gani taifa linaweza kujikomboa? Je, vyama vya siasa vina sera gani kuikomboa nchi kwenye ukoloni mamboleo?

Lissu, mgombea Urais wa tikiti ya CHADEMA, ameulizwa hilo swali, akipewa ridhaa ya kuongoza nchi hii, atachukua hatua gani kuikomboa kwenye ukoloni mamboleo? Akijibu swali hilo amesikika akisema, nanukuu: ni maneno ya wanaofuata mfumo wa kijamaa akina Nyerere na Nkurumah. ... katika uchumi wa dunia ya leo ambao ni interconnected (kufungamana) ni upuuzi, ujinga na upumbavu kuzungumzia ukoloni mamboleo. ... yaani kuwekeza mitaji yao kwenye uchumi wetu, ndio ukoloni maendeleo? ... Je, nchi yetu inaweza kuendelea kiuchumi bila uwekezaji huo?

Majibu ya swali hilo yako kwenye YouTube hii hapa. Ni majibbu yanayofikirisha kama Lissu, mgombea Urais, anajua siasa za kiuchumi au hajui kuwa hajui?


Je, anajua kuwa ukoloni mamboleo ni nchi kutawaliwa kiuchumi na mataifa ya nje? Je, anajua kuwa matokeo ya ukoloni mamboleo ni pale mitaji ya kigeni kutumika kwa ajili ya unyonyaji badala ya maendeleo ya nchi maskini duniani? Je, anatambua kuwa uwekezaji, chini ya ukoloni mamboleo huongeza, badala ya kupunguza, pengo kati ya nchi tajiri na maskini duniani?

Yawezekana ni tafsiri ya Sera ya Uchumi iliyoainishwa kwenye Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu, 2020. Kwamba Chadema kimejipanga kuutafsiri ukuaji wa uchumi kwa vitendo ili kuwepo kwa mabadiliko chanya katika maisha ya kila Mtanzania. Hili litawezekana kwa kufumua mfumo wa sasa wa uchumi wa kijamaa ambao umeshindwa kuboresha hali ya maisha ya Watanzania, na kuanzisha mfumo wa soko jamii ambao unalenga kufungua fursa kwa kila mtu kutumia vipaji vyake katika kuzalisha na kumiliki mali. Mfumo huu mpya wa uchumi wa soko utaambatana na kujenga, kuimarisha na kusimamia uchumi wa kitanzania kwa kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwa njia ya ubia na hisa na wawekezaji wenye mitaji mikubwa.

Kwa upande wake, katika Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu 2020, CCM inatambua umuhimu wa kujenga uchumi wa kitaifa ili kuhakikisha kwamba Watanzania ndio wanufaika wakuu wa uchumi na maliasili za nchi na ndiyo wenye kauli juu ya namna uchumi unavyoendeshwa. Kwa muktadha huo CCM itaelekeza Serikali kuendelea na juhudi za kuifanya Tanzania kuwa nchi inayojitegemea kiuchumi pamoja na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na nchi nyingine. Juhudi maalum zitaelekezwa kuhakikisha rasilimali za asili za nchi hii, hasa ardhi, madini, gesi asilia, mafuta, maji na misitu zinanufaisha wananchi na Taifa kikamilifu.

Tukikubaliana na dhana ya ukoloni mamboleo, kwa msingi kwamba nchi maskini bado hazijajikomboa kiuchumi, ni dhahiri kuwa Sera ya kuanza na maendeleo ya vitu kutachochea kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja, jamii na taifa. Km kuwepo kwa miundombinu imara ya usafirishaji kutamwezesha mzalishaji mali (mwenye kiwanda, mkulima, mvuvi, mchimbaji madini, nk) kuuza bidhaa zake nje ya eneo lake kwani ukubwa wa soko unaongezeka.

Wachina, wahindi, wazungu ndo wenye biashara za mitani mikubwa, sijui CCM miaka yote walikuwa wapi?

Wachina ndo wanajenga flyo over, na miradi ya baraba ya DMDP

Wazungu ndo wanachimba dhahabu na almasi

Waturuki ndo wanajenga SGR

Wamisri ndo wanajenga Stiglers

Alafuu mpuuzi mmoja analeta story za neoclonialim
 
Ukoloni mamboleo (neo-colonialism) ni nini?

Ukoloni mamboleo unaeleweka kwa mapana kama mwendelezo wa siasa ya kibepari ambayo inaziwezesha mamlaka za kibepari (baadhi ya mataifa yaliyoendelea na mashirika yake) kutawala mataifa maskini kupitia shughuli za kibepari km kuwekeza mitaji kwenye maeneo watakayofaidika badala ya njia ya utawala wa moja kwa moja.

Je, Tanzania bado iko kwenye ukoloni mamboleo na kama ipo ni jinsi gani taifa linaweza kujikomboa? Je, vyama vya siasa vina sera gani kuikomboa nchi kwenye ukoloni mamboleo?

Lissu, mgombea Urais wa tikiti ya CHADEMA, ameulizwa hilo swali, akipewa ridhaa ya kuongoza nchi hii, atachukua hatua gani kuikomboa kwenye ukoloni mamboleo? Akijibu swali hilo amesikika akisema, nanukuu: ni maneno ya wanaofuata mfumo wa kijamaa akina Nyerere na Nkurumah. ... katika uchumi wa dunia ya leo ambao ni interconnected (kufungamana) ni upuuzi, ujinga na upumbavu kuzungumzia ukoloni mamboleo. ... yaani kuwekeza mitaji yao kwenye uchumi wetu, ndio ukoloni maendeleo? ... Je, nchi yetu inaweza kuendelea kiuchumi bila uwekezaji huo?

Majibu ya swali hilo yako kwenye YouTube hii hapa. Ni majibbu yanayofikirisha kama Lissu, mgombea Urais, anajua siasa za kiuchumi au hajui kuwa hajui?


Je, anajua kuwa ukoloni mamboleo ni nchi kutawaliwa kiuchumi na mataifa ya nje? Je, anajua kuwa matokeo ya ukoloni mamboleo ni pale mitaji ya kigeni kutumika kwa ajili ya unyonyaji badala ya maendeleo ya nchi maskini duniani? Je, anatambua kuwa uwekezaji, chini ya ukoloni mamboleo huongeza, badala ya kupunguza, pengo kati ya nchi tajiri na maskini duniani?

Yawezekana ni tafsiri ya Sera ya Uchumi iliyoainishwa kwenye Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu, 2020. Kwamba Chadema kimejipanga kuutafsiri ukuaji wa uchumi kwa vitendo ili kuwepo kwa mabadiliko chanya katika maisha ya kila Mtanzania. Hili litawezekana kwa kufumua mfumo wa sasa wa uchumi wa kijamaa ambao umeshindwa kuboresha hali ya maisha ya Watanzania, na kuanzisha mfumo wa soko jamii ambao unalenga kufungua fursa kwa kila mtu kutumia vipaji vyake katika kuzalisha na kumiliki mali. Mfumo huu mpya wa uchumi wa soko utaambatana na kujenga, kuimarisha na kusimamia uchumi wa kitanzania kwa kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwa njia ya ubia na hisa na wawekezaji wenye mitaji mikubwa.

Kwa upande wake, katika Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu 2020, CCM inatambua umuhimu wa kujenga uchumi wa kitaifa ili kuhakikisha kwamba Watanzania ndio wanufaika wakuu wa uchumi na maliasili za nchi na ndiyo wenye kauli juu ya namna uchumi unavyoendeshwa. Kwa muktadha huo CCM itaelekeza Serikali kuendelea na juhudi za kuifanya Tanzania kuwa nchi inayojitegemea kiuchumi pamoja na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na nchi nyingine. Juhudi maalum zitaelekezwa kuhakikisha rasilimali za asili za nchi hii, hasa ardhi, madini, gesi asilia, mafuta, maji na misitu zinanufaisha wananchi na Taifa kikamilifu.

Tukikubaliana na dhana ya ukoloni mamboleo, kwa msingi kwamba nchi maskini bado hazijajikomboa kiuchumi, ni dhahiri kuwa Sera ya kuanza na maendeleo ya vitu kutachochea kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja, jamii na taifa. Km kuwepo kwa miundombinu imara ya usafirishaji kutamwezesha mzalishaji mali (mwenye kiwanda, mkulima, mvuvi, mchimbaji madini, nk) kuuza bidhaa zake nje ya eneo lake kwani ukubwa wa soko unaongezeka.

Tunaita utopia au Ujiinga na Upumbavu tu. hizo theory za darasani huku field hazi work, unapambanaje na neoclonialism wakati huna mitaji huna technology
 
Tunahitaji katiba mpya ambayo haitakuwa na kipengele kinachosema Tanzania ni nchi ya kijamaa. Itoshe kusema kwamba Tanzania ni nchi ya demokrasia ya vyama vingi.
Itikadi itakayofuatwa na nchi itategemea chama kipi kimeshinda uchaguzi.
 
Hata hizi habari za kujisifu Mara Uchumi wa Kati,Uchumi unakaua zote hizo ni njama za Mabeberu!
Afu tunasema Lisu anatumiwa!
Mabeberu wakitusifu ...washirika
Wakiyukosoa ...mabeberu
Rais Lissu upo sahihi ...kuleta Dhana ya Ubeberu katika Dunia ya Leo ,Ni ujinga na Upumbàvu
 
Kwanza ni aibu hata kutaja neno tu 'ukoloni mamboleo' miaka 60 baada ya uhuru. Baada ya kulea na kufuga UFISADI na kutopenda kubadilisha mfumo utakaotokomeza ufisadi tunatafuta na kuokoteza viji-dhana ambavyo viliishapitwa na wakati kama kisingizio!!! Hakuna cha baba wa ukoloni mamboleo wala mtoto wa mabeberu bali ni uzembe (au pengine mbinu ya makusudi) wetu wa kukumbatia mfumo wa kifisadi (kleptocracy) ambao unalindwa vizuri sana na Katiba yetu kongwe na chovu.
 
Back
Top Bottom