BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Mkuu habari za kuwajibika ndugu yangu, mi nipo poa kabisa, ila hizi habari kwa uoni wangu hazijitosherezi kabisa, yaani waandishi kumi...! Mwandishi mmoja angetosha sana kutuhabarisha mkuu.
Nashukuru ndugu yangu na nafurahi kusikia uko poa kabisa. Hili la waandishi wa habari wengi kushughulikia article moja nimeliona pia katika mashirika ya habari ya nje hasa kutokana na ukubwa wa habari yenyewe, kwa mfano hii habari ya kasheshe la BP. Kama walivyosema wachangiaji wengine huko nyuma kwa kweli jiji la Dar ni kubwa sana hivyo labda wao wenyewe au muajiri wao aliona ni muhimu kuyagawa maeneo ya jiji ili kumaliza mapema ngwe yao na kuwataarifu wasomaji wao.
Ukichukulia Dar ilivyokuwa kubwa na foleni za magari mwandishi mmoja au wawili itawawia vigumu kumaliza mapema kupita katika kila sehemu yenye tatizo kubwa la uhalifu. Hili swala la uhalifu Dar wiki chache zilizopita karibu liniguse kwa karibu mno lakini namshukuru sana Muumba wetu.