Kawaida magari yanayoenda Bunda ni yale magari yanayoishia Musoma(Dar- Musoma).Mkuu magari ya Musoma yanaondoka Ubungo saa 12:00 asubuhi.Kuna njia mbili ya kwanza ambayo ndiyo inayotumika sana ni ile inayopitia Mwanza (Dar-Pwani-Moro-Dodoma-Singida-Tabora-Shinyanga-Mwanza-Simiyu-Mara+Bunda)ambayo ndiyo inayoanzia Ubungo.Zamani magari yalikuwa yakifika Mwanza saa nne na nusu hadi saa tano usiku na Bunda yalikuwa yakipita saa saba na nusu hadi saa nane usiku.Sasa hivi inakubidi ulale Mwanza ambapo kufika ni saa sita au sitana nusu usiku(posibly mtalala Nyegezi au Buzuruga bus stand).Kesho asubuhi saa kumi na mbili mnaanza safari ya Musoma kupitia Bunda,hivyo Bunda tarajia kufika saa mbili au saa mbili na nusu asubuhi.Njia ya pili ni ile ya kutokea/kupitia Arusha hata hivyo hakuna gari linaloanzia Ubungo, itakubidi upande magari ya Dar-Arusha (Dar-Pwani-Tanga-Kilimanjaro-Arusha-Manyara-Mara)kisha unalala Arusha,kesho yake unapanda magari ya Arusha-Musoma.Mabasi yanayoenda huko kutokea Arusha ni Kimotico na Coast line yanafika Bunda saa tisa(Mgeta) au saa kumi(Nyamswa).Safari hii inapitia mbugani serengeti hivyo unaweza kuinjoy mbuga ya wanyama lakini sehem kubwa ya safari njia haina lami na unachelewa kufika Bunda. Safari ni ndefu hivyo jiandae na uchovu.Karibu sana Bunda sokolo!!